Thursday, December 31, 2015

NAIBU WAZIRI WA ARDHI ANGELINA MABULA ATEMBELEA SHIRIKA LA NYUMBA (NHC)

1

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Mh. Angelina Mabula akiwasili Makao Makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa NHC Upanga jijini Dar es salaam huku akilakiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo Ndugu Nehemia Mchechu wakati waziri huyo akiwa katika ziara yake ya kujifunza na kusikiliza Changamoto na mafanikio mbalimbali yaliyofikiwa na shirika hilo.
2
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Mh. Angelina Mabula akiuliza jambo kwa mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Bw. Nehemia Mchechu wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua shughuli zinazofanywa na shirika hilo.
3
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Mh. Angelina Mabula akisaini kitabu cha wageni ofisini kwa  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Bw. Nehemia Mchechu wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua shughuli zinazofanywa na shirika hilo.
4
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Mh. Angelina Mabula akiwa katika kikao na wakuu wa vitengo mbalimbali  wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua shughuli zinazofanywa na shirika hilo.
5
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Mh. Angelina Mabula akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano makao makuu ya NHC , kulia ni  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Bw. Nehemia Mchechu .
6
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Mh. Angelina Mabula akifafanua jambo  kwa waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano makao makuu ya NHC  Upanga. 
7
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Mh. Angelina Mabula akifafanua jambo  kwa waandishi wa habari  hawapo pichani katika ukumbi wa mikutano makao makuu ya NHC  Upanga. 
8
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Bw. Nehemia Mchechu  akijibu baadhi ya maswali yalioulizwa na waandishi wa habari wakati Naibu Waziri Angelina Mabula alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea shirika hilo leo.
9
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Bw. Nehemia Mchechu akijadiliana jambo na Muungano Saguya katikati na kulia ni Yahya Charahani Maafisa kutoka shirika hilo la NHC.

No comments: