Monday, December 21, 2015

MBUNGE WA MLALO ATIMIZA AHADI YAKE KWA WANAMLALO

 Katika utekelezaji wa ahadi zake Mbunge wa jimbo la Mlalo Rashid Shangazi amekabidhi mabati 40 ya geji 28 kwa wanajimbo la Mlalo  kwaajili ya  kwa ajili ya jengo la Maabara shule ya Sekondari Mtae pamoja na Mifuko 10 ya sementi kwaajili ya kwa ajili ya ukarabati msikiti mkuu wa makose. Alikabidhi vitu hivyo mwishoni mwa wiki mkoani Tanga.
Wana Mlalo wakishusha Mifuko ya Sementi 10  kwa ajili ya ukarabati msikiti mkuu wa makose, kutoka kwenye gari pamoja na Mabati 40 kwa shule ya Mtae wishoni mwa wiki katika jimbo la Mlalo mkoani Tanga.
sambamba na hilo alikabidhi mifuko ya Sementi 30 kwa ajili ya kukarabati  jengo la maabara shule ya sekondari kalmere na mifuko ya  sementi 10 kwa ajili ya ukarabati msikiti mkuu wa makose,hii ni kupelekea kuhakikisha mlalo inasonga mbele katika maendeleo ya jamii.