Friday, March 31, 2017

MIEZI MINNE BAADA YA UZINDUZI WA NDEGE MBILI ZA ATCL (BOMBARDIER), WAKUSANYA BILIONI TISA

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege la ATCL, Bw. Lasislaus Matindi anasema wamefanikiwa kukusanya Shilingi Bilioni 9 kwa Miezi minne tu kwa kutumia ndege hizo mbili zilizonunuliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli, nakuleta utata mkubwa na wapinzani wa siasa nchini waliodai kuwa hazikuwa na tija kwa Taifa. 
Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL) ilianzishwa mwezi Novemba 2002 baada ya Serikali kubinafsisha lililokuwa Shirika la Ndege la Tanzania (Air Tanzania Corporation, ATC); katika Shirika hilo, Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) lilinunua hisa asilimia 49 ndani ya ATC. Hata hivyo ubia kati ya ATCL na SAA ulikabiliwa na matatizo ya kiuendeshaji na kulazimika kusitishwa mwezi Agosti 2006 na ATCL kurejeshwa tena Serikalini kwa asilimia 100.
KUMBUKUMBU:
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwa na maafisa na viongozi wengine mbalimbali akikata utepe kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli pamoja na maafisa wengine waandamizi wakiwa kwenye ndege mojawapo baada kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam Jumatano Septemba 28, 2016. PICHA NA IKULU.

RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI AMPOKEA WAZIRI MKUU WA ETHIOPIA ALIYEWASILI MCHANA HUU JIJINI DAR

 Rais Dkt John Pombe Magufuli akimpokea mgeni wake ,Waziri Mkuu wa Ethiopia ,Hailemariam Dessalegn,aliyewasili hivi punde katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,jijini Dar Es Salaam.
 Waziri Mkuu wa Ethiopia ,Hailemariam Dessalegn akipewa maua ikiwa ni ishara ya kumkaribisha kwa upendo nchini Tanzania,mara baada kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere mapema leo mchana,na baadae kupokelewa na mwenyeji wake Rais Dkt John Pombe Magufuli,Waziri Mkuu Kassim Majliwa na viongozi mbalimbali wa Kitaifa.

Waziri Mkuu wa Ethiopia ,Hailemariam Dessalegn akishuka kwenye ndege mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere mapema leo mchana,na baadae kupokelewa na mwenyeji wake Rais Dkt John Pombe Magufuli,Waziri Mkuu Kassim Majliwa na viongozi mbalimbali wa Kitaifa.

Imeelezwa kuwa ujio wa Waziri huyo Mkuu wa Ethiopia ni pamoja na kukuza mahusiano mazuri yaliyopo baina ya Tanzania na Ethiopia pamoja ‎na kujadili fursa zaidi za ushirikiano katika maeneo mbalimbali ikiwemo uwekezaji na biashara.

 Mhe. Dessalegn atakutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa mazungumzo na kushuhudia uwekwaji saini wa mikataba ya ushirikiano kwenye maeneo mbalimbali kabla ya kuzungumza na Waandishi wa Habari.


JESHI LA POLISI NCHINI LAVUTIWA NA MIKAKATI YA NHC KUBORESHA MAKAZI

Meneja Mauzo wa Shirika la Nyumba la Taifa, Itandula Gambalagi akijadiliana jambo na Naibu Kamishna wa Bajeti wa Jeshi la Polisi nchini, Massawe kusiana na taratibu mbalimbali zinazohusu mauzo ya nyumba ni baada ya Shirika la Nyumba kuwasilisha mada kwenye mkutano huo wa Makamanda wa Jeshi la Polisi waliokuwa wakikutana mjini Dodoma. Katika mkutano huo Makamanda hao walivutiwa na juhudi mbalimbali zinazofanywa na Shirika la Nyumba katika kuhakikisha kunakuwapo makazi bora.
Meneja Mauzo wa Shirika la Nyumba la Taifa, Itandula Gambalagi akijadiliana jambo na Naibu Kamishna wa Jeshi la Polisi nchini, Silla ambaye pia alikuwa Katibu wa Kikao hicho kusiana na taratibu mbalimbali zinazohusu mauzo ya nyumba ni baada ya Shirika la Nyumba kuwasilisha mada kwenye mkutano huo wa Makamanda wa Jeshi la Polisi waliokuwa wakikutana mjini Dodoma.
Afisa Mauzo Mwandamizi wa Shirika la Nyumba la Taifa, Sophia Mwema akijadiliana jambo na Kamishna wa Polisi, Ahmed Msangi ambaye pia ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza hiyo ilikuwa mjini Dodoma jana.
 Makamanda wa Jeshi la Polisi nchi wakifuatilia kwa kina wasilisho lililikuwa likifanywa na Meneja Mauzo wa Shirika la Nyumba la Taifa, Itandula Gambalagi .
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Kamishna Jenerali Ernest Mangu na Wakuu wenzake wakifuatilia wasilisho hilo la Shirika la Nyumba la Taifa.
 Meneja Mauzo wa Shirika la Nyumba la Taifa, Itandula Gambalagi akiwasilisha mada kwenya mkutano wa viongozi wakuu wa Jeshi la Polisi nchini uliofanyika mjini Dodoma.
Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro akiuliza swali katika mkutano huo.

Thursday, March 30, 2017

WAZIRI ANGELLAH KAIRUKI APONGEZWA NA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE KWA KUSIMAMIA UTENDAJI WA TAASISI ZILIZO CHINI YA OFISI YA RAIS-MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akiwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha wa 2017/18 kwa ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Utawala wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). Wa kwanza kulia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma akimsikiliza kwa makini.

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, Mhe. George M. Lubeleje (Mb) akichangia hoja mara baada ya Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha wa 2017/18 ya Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Utawala wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, Mhe. Ahmed Juma Ngwali (Mb) akichangia hoja mara baada ya Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha wa 2017/18 ya Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Utawala wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, Mhe. Margaret S. Sitta (Mb) akichangia hoja mara baada ya Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha wa 2017/18 ya Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Utawala wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, Mhe. Saada Mkuya (Mb) akichangia hoja mara baada ya Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha wa 2017/18 ya Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Utawala wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa wakimsikiliza Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Mwanne I. Mchemba (Mb) (hayupo pichani) wakati akiongoza kikao cha kamati hiyo na Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora cha kupokea taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha wa 2017/18 ya Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora kilichofanyika Ukumbi wa Utawala wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akijibu hoja za wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa mara baada ya kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha wa 2017/18 katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Utawala wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa wakipitia kwa makini taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha wa 2017/18 ya Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora iliyowasilishwa na Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Utawala wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI YAFANYA MAPITIO YA BAJETI YAKE MJINI DODOMA KABLA YA VIKAO VYA BUNGE LA BAJETI KUANZA


Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Lameck Nchemba akitoa Maelekezo kwa Watendaji Wakuu wa Wizara yake wakati wa Kikao cha Mapitio ya Bajeti ya Taasisi ziliko katika Wizara hiyo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi muhimu kabla ya kuanza kwa Vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, linalotarajiwa kuanza mapema tarehe nne mwezi Aprili mwaka huu, Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira, Kikao hicho kimefanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.
Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Lameck Nchemba akiwa pamoja na Watendaji Wakuu wa Wizara yake wakati wa Kikao cha Mapitio ya Bajeti ya Taasisi ziliko katika Wizara hiyo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi muhimu kabla ya kuanza kwa Vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, linalotarajiwa kuanza mapema tarehe nne mwezi Aprili mwaka huu, wa kwanza kulia ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhandisi Hamadi Massauni na wa pili kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Hassan Simba Yahaya, Kikao hicho kimefanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.
Baadhi ya Watendaji Wakuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakipitia bajeti za taasisi zao, ikiwa ni sehemu ya maandalizi muhimu kabla ya kuanza kwa Vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, linalotarajiwa kuanza mapema tarehe nne mwezi Aprili mwaka huu, wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa [NIDA] Massawe, akifuatiwa na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dr. Anna Peter Makakala, watatu kushoto ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye na wanne ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Dr. Juma Malewa. Kikao hicho kimefanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.
Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Lameck Nchemba akiwa pamoja na Watendaji Wakuu wa Wizara yake wakati wa Kikao cha Mapitio ya Bajeti ya Taasisi ziliko katika Wizara hiyo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi muhimu kabla ya kuanza kwa Vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, linalotarajiwa kuanza mapema tarehe nne mwezi Aprili mwaka huu. Kikao hicho kimefanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.
Watendaji Wakuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakipitia bajeti zao, wakati wa Kikao cha Mapitio ya Bajeti ya Taasisi ziliko katika Wizara hiyo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi muhimu kabla ya kuanza kwa Vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, linalotarajiwa kuanza mapema tarehe nne mwezi Aprili mwaka huu. Kikao hicho kimefanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.
Baadhi ya Makamishna wa Uhamiaji, Magereza, na Zimamoto na Uokoaji pichani, wakipitia bajeti zao, wakati wa Kikao cha Mapitio ya Bajeti ya Taasisi ziliko katika Wizara hiyo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi muhimu kabla ya kuanza kwa Vikao vya Bunge la Bajeti la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, linalotarajiwa kuanza mapema tarehe nne mwezi Aprili mwaka huu. Kikao hicho kimefanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma. [PICHA ZOTE NA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YANCHI]



IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

JAJI WARIOBA AONGOZA VIONGOZI NA WASOMI KUJADILI MAENDELEO YA VIWANDA NCHINI

 Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba akitoa mada katika mdahalo ulioandaliwa na REPOA juu ya mapinduzi ya Viwanda,Jana jijini Dar
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara , Profesa Adolf Mkenda akitoa ufafnuzi juu ya nini kifanyike katika kufikia malengo ya mapinduzi ya Viwanda nchini
 Mzee Butiku akifuatilia mjadala huo ambao ulikuwa wa aina yake
 Mkurugenzi mkuu wa Benki ya CRDB nchini , Charles Kimei akizungumza namna mabenki yanavyoweza kutoa mchango mkubwa katika mapinduzi ya Viwanda nchini wakati wa mjadala ulioandaliwa na REPOA juu ya nini kifanyike kuelekea mapinduzi ya Viwanda kwa kushirikisha Tasisi,jana jijini Dar
 Waziri wa Fedha Mstaafu wa awamu ya nne ,Bazili Mramba akizungumzia juu ya nini kifanyike katika serikali kuu ili tuweze kufanikiwa katika maendeleo ya Viwanda
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara , Profesa Adolf Mkenda akiwa na baadhi ya washiriki mara baada ya kumalizika kwa mjadala huo

Tuesday, March 28, 2017

MAKAMISHNA WAPYA WA UHAMIAJI WAANZA KAZI DODOMA


 Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dr. Anna Peter Makakala ,akimvisha cheo kipya Kamishna wa Uhamiaji Utawala na Fedha,  Edward Peter Chogero  katika hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma. Anayeshuhudia ni Naibu Kamishna wa Uhamiaji Chrispin Ngonyani. Tukio hili linehudhuriwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali Projest Rwegasira  na Naibu  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi  Hassan Simba Yahaya.
 Kamishna mpya wa Uhamiaji Divisheni ya Sheria Hannerole Morgan Manyanga akila kiapo cha Utii mbele ya Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dr.  Anna Peter Makakala katika hafla iliyofanyika  leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma. Hafla hiyo imehudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara  ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali Projest Rwegasira   na Naibu  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Hassan Simba Yahaya.
 Kamishna wa Tume ya Maadili ya Utumishi wa Umma , Jaji Mstaafu Harold Nsekela wa kwanza kushoto akiwaongoza  Makamishna wapya wa Uhamiaji kuapa  kiapo cha Maadili ya Viongozi wa  Utumishi wa Umma baada ya Makamishna hao wapya kuvalishwa vyeo vipya katika hafla iliyofanyika  leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma. 
 Makamishna wapya wa Uhamiaji wakisaini Fomu za Maadili ya Viongozi wa Umma baada ya Makamishna hao kula kiapo cha Maadili ya Viongozi wa Utumishi wa Umma, katika hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara  ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali Projest Rwegasira   akizungumza jambo na Makamishna wapya wa Uhamiaji baada ya kumalizika shughuli ya kuapishwa Makamishna hao  leo katika viwanja vya Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma. 

Monday, March 27, 2017

WAFANYAKAZI NHC WAKUTANA KUJADILI MASUALA MBALIMBALI YA KIUTENDAJI KAZI

 Viongozi wa Chama cha wafanyakazi wa migodini na kazi za ujenzi (TAMICO) wa Shirika la Nyumba la Taifa akiimba wimbo wa Mshikamano kwa wafanyakazi katika kupigania maslahi ya wafanyakazi Mkutano ulifanyika siku ya Ijumaa.


Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakiimba wimbo wa Mshikamano kwa wafanyakazi katika kupigania maslahi ya wafanyakazi Mkutano ulifanyika siku ya Ijumaa.
 Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakiimba wimbo wa Mshikamano kwa wafanyakazi katika kupigania maslahi ya wafanyakazi Mkutano ulifanyika siku ya Ijumaa.
 Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakiimba wimbo wa Mshikamano kwa wafanyakazi katika kupigania maslahi ya wafanyakazi Mkutano ulifanyika siku ya Ijumaa.
 Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakifuatilia kwa karibu hoja zilizokuwa zikitolewa kwenye mkutano huo. Mkutano ulifanyika siku ya Ijumaa.
Mwenyekiti wa Chama cha wafanyakazi wa migodini na kazi za ujenzi (TAMICO) wa Shirika la Nyumba la Taifa, Lilian Reuben akizungumza  akiimba wimbo wa Mshikamano kwa wafanyakazi katika kupigania maslahi ya wafanyakazi Mkutano ulifanyika siku ya Ijumaa.

Sunday, March 26, 2017

Rais Magufuli atengua uteuzi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Prof. Justin Ntalikwa

SPIKA JOB NDUGAI NA WAJUMBE WA KAMATI ZA BUNGE ZA BAJETI NA NISHATI NA MADINI WATEMBELEA BANDARI YA DAR ES SALAAM


 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko akimpa muhtasari Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai ambaye ameongoza wajumbe wa Kamati za kudumu za Bunge za Nishati na Madini pamoja na Kamati ya Bajeti bandari ya Dar es salaam kujionea makontena yenye shehena ya mchanga kutoka migodini iliyokuwa imezuiwa kusafirishwa nje ya nchi kwa agizo la serikali leo Machi 26, 2017
Sehemu ya  makontena yenye shehena ya mchanga kutoka migodini ambayo imezuiwa  kusafirishwa nje ya nchi kwa agizo la serikali 
  Sehemu ya wajumbe wa Kamati za kudumu za Bunge za Nishati na Madini pamoja na Kamati ya Bajeti wakitembelea bandari ya Dar es salaam kujionea makontena yenye shehena ya mchanga kutoka migodini ambayo  imezuiwa kusafirishwa nje ya nchi kwa agizo la serikali leo Machi 26, 2017
  Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko akimpa maelezo  Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai na wajumbe wa Kamati za kudumu za Bunge za Nishati na Madini pamoja na Kamati ya Bajeti bandari ya Dar es salaam juu ya makontena yenye shehena ya mchanga kutoka migodini iliyokuwa imezuiwa kusafirishwa nje ya nchi kwa agizo la serikali leo Machi 26, 2017
 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akiwa na wajumbe wa Kamati za kudumu za Bunge za Nishati na Madini pamoja na Kamati ya Bajeti akiongea na wanahabari katika bandari ya Dar es salaam baada ya kujionea makontena yenye shehena ya mchanga kutoka migodini ambayo imezuiwa kusafirishwa nje ya nchi kwa agizo la serikali leo Machi 26, 2017