Thursday, April 30, 2009

Chenge aongezewa shtaka

Marehemu Beatrice Costantine!

Marehemu Vicky Makanya!
Mzee wa vijisenti

MBUNGE wa Bariadi Mashariki, Andrew Chenge jana aliongezewa shtaka katika kesi inayomkabili ya mashtaka matatu ya kuendesha gari kizembe na bila tahadhari na kusababisha vifo vya watu wawili na uharibifu wa pikipiki ya matairi matatu, maarufu kama Bajaji.

Waziri huyo wa zamani wa miundombinu ambaye pia alikuwa mwanasheria mkuu wa serikali alifikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kinondoni jana na kusomewa mashtaka yake mapya ambayo sasa yanakuwa manne.

Chenge ameongezewa shtaka la kuendesha gari aina ya Toyota Hilux Double Cabin ambayo ilikuwa haina bima. Pia katika kesi hiyo ameunganishwa mmiliki wa Bajaji hiyo, Majid Ghalid, 26.

Chenge, ambaye alijiuzulu wadhifa wake wa Waziri wa Miundo Mbinu baada ya kutajwa kwenye kashfa ya ununuzi wa rada, alitinga mahakamani hapo tofauti kabisa na awali, akionekana kutokuwa na woga na alisalimiana na wananchi waliokuwa wamefurika mahakamani.

Akisoma hati ya shtaka la kwanza kwanza, mwendesha mashtaka wa polisi, David Mafwimbo alidai kuwa alfajiri ya Machi 27 mwaka huu Chenge alitenda kosa la kwanza kwenye makutano ya Barabara ya Haile Salasie na Karume alipoendesha gari hilo kwa uzembe kwenye makazi ya watu na kushindwa kuchukua tahadhari na kuigonga Bajaji kusababisha kifo cha Victoria Goerge.

Katika shtaka la pili, Mafwimbo alisema siku na wakati kama huo, Chenge alisababisha kifo cha Beatrice Constantine.

Mafwimbo alidai kuwa Chenge alitenda kosa la tatu katika muda na tarehe kama hiyo kwa kuendesha gari kwa uzembe na kusababisha uharibifu wa Bajaj iliyokuwa inatoka upande wa pili. habari imeandikwa na Kuruthum Ahmed.

Wednesday, April 29, 2009

Mabomu Dar balaa







HALI ni tete, Jiji la Dar es Saalam na vitongoji vyake, jana lilizizima kwa mishindo mkubwa na mitetemo ya mabomu na makombora yaliyolipuka kwa kupishana kutoka katika kambi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), 671 Mbagala.

Mtafaruku huo, pia uliyakumba maeneo jirani na kusababuisha vifo vya watu, mamia kujeruhiwa, nyumba kuungua, huku watoto 200 wakipotezana na familia zao.

Mamia ya wakazi wa jiji hilo hasa Mbagala na vitongoji vyake walionekana kuchanganyikiwa walikuwa wakihangaika kukimbia nyumba zao kwa lengo la kujiokoa.

Katika harakati za kujiokoa baadhi ya wananchi ho walitumbukia mtoni huku baadhi yao wakiwasahau watoto wao na vikongwe nyumba bila msaada wowote

Barabara ya Kilwa kuanzia eneo la uwanja wa Maonyesho ya Kimataifa ya Biashara, Kambi ya Jeshi ya Twalipo hadi Mbagala Kizuiani ilipo kambi hiyo ya kikosi cha 671, ilijaa askari wa JWTZ waliojipanga kando na kuongoza magari, huku wakizuia mengine kuelekea karibu na eneo la tukio.

Majira ya saa tano asubuhi mshindo mzito wa kwanza ulisikika na ambao ulitikisa takriban majengo yote katikati ya jiji, huku moshi mweusi ukionekana angani upenda wa barabara ya Kilwa na dakika chache baadaye magari ya vikosi vya zima moto, polisi, JWTZ na waandishi wa habari vilihangaika kuelekea kwenye tukio.

Hata hivyo misafara hiyo ilikwamishwa njiani na msururu mrefu wa magari na wananchi waliokuwa wakikimbia kutoka eneo karibu na tukio kuelekea katikati ya jiji, hivyo kulazimika kutafuta njia nyingine ya kufika eneo la tukio.

Vikosi vya zima moto viliwahi eneo la tukio, huku milipuko ilikuwa ikiendelea kwa mpishano wa dakika kati ya tatu na sita majira ya asubuhi na saa za jioni ilipugua kwa mpshano wa robo saa hadi dakika 20.

Breaking News: Mabomu yalipuka Dar

Habari zilizotufikia hivi sasa zinasema kuwa nyumba kadhaa zimeungua moto, mtu mmoja kufa na wengine kibao kujeruhiwa kutokana na mlipuko mkubwa wa mabomu umetokea katika jiji la Dar es salaam katika eneo la jeshi Mbagala Kizuiani.

Tuesday, April 28, 2009

watotooooo



Hebu cheki vijana wetu wanaotakiwa kuwapo shule angalau wakiperuzi mambo mawili matatu kwaajili ya mustakabali wa maisha yao lakini wao kutokana na shughuli nyingi za wazazi wau mitaa ya huku vijijini wanautumia muda huu muhimu katika maisha yao kwaajili ya kuchunga mifugo hebu fikiria angekuwa mtoto au mdogo wao ungefanyaje kusaidia. Picha ya mdau michael matemanga aliyekuwapo huko Singida hivi karibuni.

Mrema huyu ndo yule yuleeee

KUNDI la Wanachama wa Tanzania Labour Party (TLP), wametangaza kujiengua na uongozi wa chama hicho na kuteua viongozi wapya wa mpito kutokana na kutopewa haki zao za kidemokrasia katika uchaguzi mkuu uliofanyika juzi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam akiwa ameambata na wajumbe wa TLP kutoka mikoani, Mwenyekiti mteule wa Taifa, Maxmilliam Lyimo alisema kutokana na kutotendewa haki ya kidemokrasia katika uchaguzi wa juzi wajumbe wameteua viongozi wao wa mpito wa Taifa ili kukinusuru chama.

“Ndugu waandishi wa habari tumewaita ili kuelezea uchaguzi wa kihuni uliofanyika jana uliofanywa na Mrema akishirikiana na Kikwete ili wahakikishe tunashindwa uchaguzi” alisema Lyimo.

Pia Lyimo aliongeza kuwa; “Kutokana na hali hiyo ili kukinusuru chama ndipo kamati Mpya ya mpito wa mkutano mkuu umeteua viongozi wa mpito mpaka hapo utakapofanyika uchaguzi wa kidemokrasia”

Aidha, Lyimo aliwataja viongozi wapya wa mpito wateule wa Kitaifa watakaokuwa wanakiongoza chama hicho mpaka hapo utakapofanyika uchaguzi Mkuu na sio uchaguzi wa kihuni uliofanyika juzi Mbagala.
“Nafasi ya Mwenyekiti nimeteuliwa mimi, Joram Kinanda ameteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti, Benedicto Mtungirehi Katibu Mkuu na naibu Katibu ameteuliwa James Haule na pia wajumbe kutoka mkoani wamepita kuwa wajumbe,” alisema Lyimo.

Lyimo aliongezea kwa kutoa mpya kuwa Mrema ameletwa na serikali ili akivuruge chama na pia ni usalama wa Taifa na ushaidi anao kwani alishatangaza wakati akiwa kwenye mkutano na wananchi wa Umbwe Moshi Vijijini mwaka 1986. Taarifa imeandikwa na Felix Mwagara.

Monday, April 27, 2009

Mzee wa sumo apata ajali



MZEE wa Sumo kapata ajali akiwa njiani akirejea jijini Dar alikwenda huko katik maadhimisho ya siku ya Malaria ambapo msanii Yvone Machaka alikuwa mgeni mkubwa huko, ama kwa hakika ajali hiyo haikuwa ya kawaida lakini bahatai njema mzee wa sumo amesevu na anadunda kama kawa na unaweza kumpata kwa kumcheki hapa
katika mtandao wake gari yake ilibiringika mara kadhaa!!!! Kikubwa ni kwamba bado nipo hajafa na yupo mjini Lindi. lakini mchuma tuliokuwa tunasafiria ndio kwisha kazi!!!

Abdul mshindi wa Mil 10 shindano la maisha plus






MSHIRIKI kutoka Zanzibar Abdul juzi ameibuka mshindi katika shindano la maisha plus na kujinyakulia kitita cha fedha taslim shilingi millioni 10, baada ya kuishi kijiji kwa takribani siku 56.

Kwa matokea yaliyotolewa na majaji kwa kupitia ujumbe mfupi uliokuwa ukitumwa na wananchi ambao walikuwa wakifuatilia mchezo huo kupitia mtandaoni na televisioni ya taifa (TBC, 1)

Mshindi huyo kutoka Zanzibar, Abdul ambae alikuwa akishindana vikali na Mwanadada Upendo kutoka mkoani Mwanza ambae alijiwekea uwezo mkubwa sana lakini hadi kufikia mwisho wa mashindano mshiriki huyo hakuweza kuamini ukweli wa matokeo waliyoyatangaza majaji.

Katika ya mchezo huo ambao mshiriki kutoka Mwanza Upendo alikuwa hakionekana kuwa mshindi baada ya kuwa na pointi nyingi ambazo ziliweza hata kumshinda Abdul kwa kuwa na pointi nyingi hadikufikia wiki mbili za mwisho.

Wakati mshindi wa shindano hilo akikabidhiwa kitita cha sh mil 10 na baadae wote waliweza kupatiwa siku moja ya kukutana na kubadilishana mawazo katika mbuga za wanyama zilizopo Mikumi mjini Morogoro.

Kufuatia siku hiyo ya kutembelea mbuza za wanyama washiriki ambao watakaokuwa walengwa na wale wote ambao wamefanikiwa kuingia katika kinyanganyiro cha kumi bora.

Washiriki hao ambao wameingia kumi bora na baadae kubaki washiriki watatu na ndipo alipochaguliwa mshindi mmoja na kujinyakulia shilingi milioni kumi ambayo ataweza kuwekewa kwenye akaunti yake kwa ajili ya usalama zaidi.

Washiriki hao ambao waliweza kuingia kumi bora ni Abduli,Modersta,Steve,Hamis,Maulid, makala hii fupi imeandikwa na Zaina Malongo






.

Friday, April 24, 2009

Mzee Kabuye afariki dunia






Mzee Kabuye afariki dunia

Waandishi Wetu

ALIYEKUWA mbunge wa jimbo la Biharamulo Magharibi kwa tiketi ya chama cha TLP, Phares Kabuye amefariki katika ajali ya basi iliyotokea katika kijiji cha Magubike kata ya Berega wilaya ya Kilosa na kujeruhi watu 54.

Ajali hiyo ilitokea jana saa moja asubuhi katika kijiji hicho ikilihusisha basi la kampuni ya RS Investment lililokuwa likitokea Bukoba kwenda Dar es Salaam ambapo inadaiwa mbunge huyo alikuwa akiwahi mkutano mkuu wa chama cha TLP unaofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Akitangaza taarifa za kifo hicho, jana jioni wakati wa sehemu ya pili ya kikao hicho na Mwenyekiti wa Bunge, Job Ndugai alisema kuwa maiti alihifadhiwa katika Hospitali ya Misheni ya Berega.

Mwenyekiti huyo, ambaye alikuwa anaendesha kikao cha bunge jana jioni, alisema kuwa taratibu za mazishi zinafanywa na familia ya marehemu.

Alisema kuwa ofisi ya bunge itawatangazia wabunge juu ya ratiba ya mazishi mara tu baada ya familia kuwapatia utaratibu.

Taarifa hiyo ilipokewa kwa masikitiko makubwa na wabunge hao hasa wakimkumbuka kwa ucheshi na umahiri wake katika kujenga hoja enzi za uhai wake.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka eneo la tukio ambazo pia zimethibitishwa na kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro, Thobias Andengenye, ajali hiyo ilitokea baada ya uzembe wa dereva wa basi hilo ambaye jina lake halijapatikana kudaiwa kumuachia kondakta wake kuendesha basi hilo.

Taarifa hizo zimeeleza kuwa kondakta wa basi hilo ambaye pia jina lake halikupatikana alishindwa kulimudu basi hilo kutokana na mwendo kasi hivyo kusababisha basi hilo kupoteza mwelekeo na kupinduka ambapo watu wawili walikufa papo hapo.

Taarifa zilizopatikana zimesema Kabuye alifikwa na mauti baada ya kufikishwa katika hospitali ya Berega alikopelekwa kwa matibabu na kwamba miili ya marehemu wote watatu imehifadhiwa katika hospitali hiyo kwa ajili ya kutambuliwa na majeruhi wote wa ajali wamelazwa katika hospitali hiyo.

Baada ya kutokea kwa ajali hiyo inadaiwa dereva na kondakta wake walikimbia huku jeshi la polisi likiendelea na juhudi za kuwatafuta.

Phares Kabuye alizaliwa mwaka 1938 na alishawahi kuwa kada na mbunge wa chama cha mapinduzi mwaka 1977-1990 na baadae kuhamia katika chama cha TLP na kupata ubunge kwa tiketi ya chama hicho 2005 hadi alipovuliwa ubunge na mahakama mwaka juzi.

Imeandikwa na Samuel Msuya na Venance George wa Morogoro na Kizitto Noya, Dodoma wa Mwananchi.

Thursday, April 23, 2009

Zuma mambo safi


JOHANNESBURG, Afrika Kusini

Chama tawala nchini Afrika Kusini, Africa National Congress, ANC tayari kinaelekea kupata ushindi mkubwa, licha ya wasiwasi wa awali kuwa chama kipya cha Congress of the people au COPE kingetingisa ANC.

Jacob Zuma naye yupo kileleni kuwa rais mpya wa Afrika Kusini- hadhi ya juu ya kiongozi ambaye alikuwa amezongwa na mashtaka ya ufisadi wiki mbili tu kabla ya uchaguzi huu.

Matokeo ya awali baada ya kuhesabiwa kwa kura milioni sita yanaonyesha ANC imepata aslia mia 65 ya kura.

Tume ya uchaguzi nchini humo imesema aslia mia 77 ya watu walipiga kura katika uchaguzi wa jana. Katibu mkuu wa ANC Gwede Montasha anaeleza kuwa ANC itajibidiisha kuwatumikia raia wa Afrika Kusini.

Chama cha ANC hata hivyo kimepata upinzani mkubwa katika mkoa wa CAPE Magharibi. Chama rasmi cha upinzani cha Demokratic Alliance kinachoongozwa na Hellen Zille kimepata aslia mia 55 ya kura hadi kufikia sasa.

Matokeo ya awali yanakipa chama tawala cha ANC nchini Afrika Kusini ushindi mkubwa katika uchaguzi mkuu na hivyo kutoa nafasi kwa Jacob Zuma kuwa rais wa nchi hiyo.
Wafuasi wa ANC wamealikwa kusherehekea ingawa kuna kila dalili chama hicho kitashindwa kupata theluthi mbili ya kura zinazohitajika kwa ajili ya marekebisho ya katiba.

Huku robo ya kura zote zikiwa zimekwishahesabiwa, ANC kimejizolea asilimia 65 ya kura na chama cha Democratic Allience(DA) chenye upinzani mkubwa na ANC kimepata asilimia 19 ya kura.

Ka- Deci kengine haka hapa



IDADI kubwa ya wanachama waliokuwa katika taasisi kupanda na kuvuna pesa ya Development Entrepreneurships Community Initiative (Deci) wamejiunga na taasisi nyingine ijulinakayo ya Tumaini.

Taasisi hiyo ambayo makazi yake makuu ni Jijini Dar es Salaam inajishughulisha na shughuli kama za Deci ingawa kuna tofauti ndogo zilizojitokeza pindi wanachama hao wanapotaka kujiunga kwa sababu wanaambiwa kuwa waingize fedha zao katika akaunti yao iliyopo katika benki ya Dar es Salaam Community Bank(DCB).

Mmoja wa wanachama wapaya kutoka Deci ya mabibo alisema kuwa, riba inayotolewa na tumaini ni kubwa ambayo wanaamini kuwa inaweza kuwapunguzia makali ya maisha pindi wanapoitwa kuvuna.

“Tumeamua kujiunga na Tumaini, tumeambiwa kuwa wanatoa riba kubwa hasa unapoingiza fedha kuanzia kiasi cha Sh100,000 hadi 200,000 na kupata Sh500,000 faida ambazo ni nyingi na unaweza kupunguza baadhi ya majukumu ya kimaisha,”alisema mwanachama huyo ambaye hakutaka kutaja jina lake.

Aliongeza mpaka sasa zaidi ya wanachama 30 ambayo walikuwa wote katika taasisi ya Deci wameamua kujiunga na Tumaini ili waweze kufidia pesa zao zilizopo Deci ambazo mpaka sasa hawana uhakika kama watalipwa au la, jambo ambalo linawafanya watafute mbinu nyingine za kupata fedha.

Alisema baadhi ya wanachama waliowekeza Deci wengi wao walikuwa wamekopa, wakati serikali imetangaza kuzifunga akaunti za Deci wamechanganyikiwa kwa kuhofia madeni ambayo walitegemea kurudisha wakati wa mavuno, jambo ambalo linawafanya waishi katika mazingira magumu. Habari hii imeandikwa na Patricia Kimelemeta wa Mwananchi.

Wednesday, April 22, 2009

Afrika kusini wapiga kura leo



Wastahiki milioni 23 nchini Afrika Kusini leo wanapiga kura katika uchaguzi mkuu wa nne, ambapo chama kinachotawala ANC kinatarajiwa kushinda tena kwa kura nyingi.

Chama cha ANC kitakabiliwa na changamoto kubwa kutoka kwa vyama vya upinzani.Uchaguzi wa leo pia unatarajiwa kumpitisha rais wa chama hicho Jacob Zuma kuwa rais wa nchi vilevile.

Chama cha ANC kinatarajiwa kushinda katika uchaguzi huo mkuu na mgombe urais wa chama hicho Jacob Zuma pia anatazamiwa kupita kwa kura nyingi.

Watu walianza kupiga kura nchinini kote saa moja asubuhi kwenye vituo vya kupigia karibu alfu 20 katika zoezi litakalochukua muda wa saa 14.

Wake za marais wakutana Hollywood


Queen Inkhosikati LaMbikiza of Swaziland







(R-L) Her Excellency Salma Kikwete of Tanzania (United Republic of) and Sarah Brown

Her Excellency Salma Kikwete of Tanzania. Kwa taarifa zaidi bonyeza hapa
au hapa

Tuesday, April 21, 2009

Deci sasa mapande mapande


WANACHAMA wa tassisi Development Entrepreneurship Community Intiatives (Deci) wameonekana kupoteza mwelekeo baada ya kugawanyika katika makundi mawili, moja likiwa likitaka kuishtaki taasisi hiyo na jingine likitaka kufungua kesi dhidi ya serikali.

Vikundi hivyo, vikiwa na mitazamo tofauti, vinasema vinakamilisha taratibu za kisheria ili kufungua kesi mahakamani.

Mwenyekiti wa kamati ya wanachama wa Deci, Mchungaji Isaack Kalenge, ambaye juzi alikamatwa na polisi na baadaye kuachiwa, aliiambia Mwanachi kuwa taratibu za kuishitaki serikali zimefikia hatua za mwisho na kwamba wakati wowote watakwenda Mahakama Kuu kitengo cha biashara kufungua kesi ya madai.

Alisema serikali haikuwa na sababu za kuifunga Deci kwa sababu hakuna mwanachama hata mmoja aliyekwenda kulalamika serikalini kuwa amedhulumiwa haki zake.

“Hapa kila mtu alikuwa anapata haki yake... imekuwaje serikali kuja kuifunga,” alihoji Mch Kalenge.

Lakini kikundi kingine kimeshafungua jalada la kesi ya madai katika Kituo cha Polisi cha Kati jijini Dar es Salaam dhidi ya taasisi hiyokikidai kimepoteza imani na Deci. imeandaliwa na Geofrey Nyang’oro na Patricia Kimelemeta na Picha ya Silvan Kiwale wa Mwananchi.

Bajaj sasa ruksa


Muswada uliolenga kuruhusu bajaji zitumike kama vyombo vya usafiri nchini umepitishwa rasmi kuwa sheria.

Sheria hiyo ya Leseni za Usafiri ambayo ilikuwamo katika muswada wa marekebisho ya sheria mbalimbali wa mwaka 2009, umesainiwa rasmi na rais kuwa sheria Nmba 3 ya mwaka 2009.

Baadhi ya miswada hiyo iliyoidhinishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa sheria kuwa ni pamoja na Sheria ya Vyama vya Siasa Namba 7 ya mwaka 2009 na Sheria ya Wanyamapori Namba 5 ya mwaka 2009.

Spika wa Bunge Samuel Sitta ameliambia bunge mjini Dodoma jana kuwa miswada ambayo iliyojadiliwa na kupitishwa na bunge mwezi Februari mwaka huu sasa imetangazwa rasmi kuwa sheria.

Kupitishwa kwa sheria hizo ikiwemo inayoruhusu matumizi ya pikipiki za miguu mitatu katika usafiri wa umma kutasaidia kuondoa utata uliogubika matumizi ya usafiri huo hususan katika jiji la Dar es Salaam.

Hata hivyo matumizi hayo yatategemeana kwa kiasi kikubwa na kanuni zitakazosimamia utekelezaji wa sheria hiyo ambazo zitatungwa na wizara husika.

Sagula sagula Kariakoo




Kila mmoja katika jiji hili la maraha la Dar es salaam yuko bize na jambo lake, wapo wanakula raha kama vile wanaishi jijini New York, lakini wapo wengine wanaishi kama vile wapo Soweto ili mradi ni balaa tupu, hebu cheki hapa wabongo wanasagula sagula Kariakoo huku wengine wakitaabika na bidhaa zao juani.

Sunday, April 19, 2009

Byebye Deci


The Government has frozen the bank accounts operated by the Development Entrepreneurship for Community Initiative (Deci) directors.

Finance and Economic Affairs minister Mustafa Mkulo said yesterday that the move was meant to safeguard money deposited by thousands of Deci members.

Mr Mkulo said when presenting the Government’s official position on the Deci saga that authorities were looking for more bank accounts linked to the institution and its directors.

“We’re looking for more accounts because the amount of money deposited in the frozen accounts does not tally with the sum collected from depositors,” he said without specifying how much had been found in the seized accounts.

Mr Mkulo said Deci had only one account, adding that the bulk of the cash deposited by members had apparently been deposited in personal accounts operated by the institution’s managers. By Beatus Kagashe.

Si Yanga wala Simba


Kelele za wababe wa soka nchini Tanzania jana zilifikia ukingoni baada ya kila mmoja kutoka na lake. Kiufupi hakukuwa na mbabe walianza Simba wakapachika bao wakatamba wakaruka ruka na kuzomea, soka likatandazwa watu wakabaki midomo wazi, ikawa sasa wanavizia mtu akosee wazomee.

Jerry Tegete alizima kelele na shangwe za mashabiki wa Simba kwa kufunga bao la kusawazisha dakika za ziada na kufanya matokeo kuwa 2-2 kwenye mchezo uliochezwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana.

Mashabiki wa Simba walikuwa wakishangilia kipindi chote cha mchezo na furaha yao ilizidi baada ya winga wake Ramadhani Chombo 'Redondo' kuunganisha kwa kichwa krosi ya Henry Joseph dakika ya 23 kuandika bao la kwanza kwa wekundu hao.
Kuingia kwa bao hilo kuliamsha ari kwa Simba na kufanya mashambulizi na hadi mapumziko walikuwa wakioongoza kwa bao 1-0.

Mwanzoni mwa kipindi cha pili mshambuliaji wa kimataifa wa Kenya, Ben Mwalala aliisawazishia Yanga dakika ya 48 na kukimbilia eneo walipo mashabiki wa Simba na kuwafunga mdomo kitendo kilichowakera na kuanza kurusha chupa za maji.
Hata hivyo dakika ya 62, mchezaji bora wa mechi hiyo Haruna Moshi 'Boban' aliifungia timu yake bao la pili baada ya kuuwahi mpira ulipanguliwa na kipa Juma Kaseja baada ya kulitema shuti la Ramadhani Chombo.

Moshi alionyesha mchango mkubwa kwa timu yake jambo lilopelekea jopo la ufundi kumtangaza mchezaji bora wa mechi na kuzawadiwa shilingi 300,000 .
Bao hilo la Boban lilidumu hadi dakika 90 kabla ya Jerry Tegete kuzima furaha za mashabiki wa Simba baada ya kuunganisha krosi ya Mike Barasa kwa kifua na kumwacha kipa wa Simba, Ally Mustapha asijue la kufanya.

Jennifer Lopez na mambo yake



J-Lo got her big start on the TV comedy hit In Living Color as a Fly Girl dancer. But bigger and better things were on the horizon for Jenny as she moved onto the silver screen in Money Train (1995) and Selena (1997). And before we could say, "Hey, who's that hot Puerto Rican chick?" Jennifer released an album called On The 6. It was certified three times platinum, and every song and movie since (except for 2003's Gigli) has been J-Lo gold.

mambo ya Hasheem Thabeet supa








Connecticut's Hasheem Thabeet has decided to enter the NBA draft.

The 7-foot-3 center said Tuesday that he made the decision after speaking to family, friends and coach Jim Calhoun.

In a statement released by the school, Calhoun called Thabeet "one of the most dominant defensive players in the history of college Basketball," and said he believes he is ready to make the move to the NBA.

Thabeet, a two-time defensive player of the year in the Big East, averaged 13.6 points, 10.8 rebounds and 4.2 blocked shots per game in helping the Huskies to a 31-5 record and a Final Four berth.

Friday, April 17, 2009

Kaimu Jaji Mkuu


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Ali Mohamed Shein, akimuapisha Jaji Eusebia Nicholas Munuo kuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Ikulu Dar es salaam leo kufuatia kuondoka kwa Jaji Mkuu wa Tanzania Agostino Ramadhani ambae yupo Nje ya Nchi kikazi. Katikati ni Katibu Mkuu Utumishi George Yambesi

Thursday, April 16, 2009

mambo ya mugongo mugongo



Heee mambo ya Twangazzz hebu cheki walivyokuwa wakijituma hivi majuzi katika viwanja vya michezo vya eneo la Mkuza wilayani Kibaha katika mojawapo ya harakati za mashindano ya netiball taifa, aisee hawa jamaa wamekamata anga za muziki ile mbaya, hawana muchezo ni mugongo mugongo tu.