Tuesday, December 29, 2015

WAZIRI MBARAWA ATEMBELEA TPA NA TRL LEO


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Prof. Makame Mbarawa akizungumza na uongozi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), wakati alipotembelea bandarini hapo leo jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Prof. Makame Mbarawa akiongozana na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Eng. Edwin Ngonyani pamoja na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Mussa Iyombe wametembelea Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), kwa mara ya pili tangu alipoapishwa jana.

Aidha Waziri Mbarawa katika ziara yake hiyo ametembelea pia na Shirika la Reli Tanzania (TRL), na kupokea taarifa ya utendaji wa kazi wa taasisi hizo kama picha zinavyoonesha:
 Maafisa wa Wizara na Watendaji wa Mamlaka ya Bandari wakimsikiliza kwa makini Mhe. Waziri Mbarawa alipokuwa akitoa maelekezo ya kazi katika ofisi za Meneja wa Bandari mkoa wa Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Prof. Makame Mbarawa (kushoto) na Naibu wa Wizara hiyo Eng. Edwin Ngonyani (kulia) wakipata maelezo kutoka kwa Kaimu Mtendaji Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRL), Eng. Mshana (katikati) mara walipowasili kwenye ofisi za Shirika hilo.
 Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Mussa Iyombe akifafanua jambo wakati wa upokeaji wa taarifa ya utendaji kazi wa TRL.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRL), Eng. Mshana (wa kwanza kushoto), akitoa taarifa ya changamoto zinazoikabili shirika hilo kwa Mhe. Waziri Mbarawa.
Waziri Mbarawa akisisitiza jambo alipokuwa akitoa maelekezo kwa watendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRL), jijini Dar es Salaam.

No comments: