Friday, December 29, 2017

MAMIA WAMZIKA MWANDISHI MKONGWE MAYAGE S MAYAGE MAKABURI YA MBWENI MAPUTO JIJINI DAR








































 Ndugu,Jamaa na Marafiki wakishiriki kumzika mpendwa wao Mayage S Mayage jioni ya leo katika makaburi ya Mbweni Maputo,Kinondoni jijini Dar Es Salaam
 Sala ya Maziko ya Marehemu Mayage Steven Mayage ikiendelea katika Makaburi ya Mbweni Maputo,kabla ya kumlaza mpendwa wetu katika nyumba yake ya Milele,jioni ya leo.
 Wawakilishi kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,Ikulu John Chacha na Ankal Issa Michuzi kwa pamoja wakiweka shada la Maua juu ya kaburi la marehemu mara baada ya kufanyika maziko yake jioni ya leo katika makaburi ya Mbweni Maputo,Kinondoni jijini Dar Es Salaam.
 Mbunge wa Jimbo la Mtama,Mh Nape Nnauye akiweka shada la Maua juu ya kaburi la marehemu mara baada ya kufanyika maziko yake jioni ya leo katika makaburi ya Mbweni Maputo,Kinondoni jijini Dar Es Salaam.
 Mmoja wa aliyefanya kazi na Marehemu Mayage,Ndugu Haji Dillunga akiweka uwa juu ya kaburi la marehemu mara baada ya kufanyika maziko yake jioni ya leo katika makaburi ya Mbweni Maputo,Kinondoni jijini Dar Es Salaam.
 Safari ya Mwisho ya aliyekuwa Mwandishi Mkongwe hapa nchini,Marehemu Mayage Steven Mayage imefanyika jioni ya leo katika makaburi ya Mbweni Maputo,Kinondoni jijini Dar Es Salaamu








 Katibu NEC-Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole akitoa heshima za mwisho wakati wa kuaga mwili wa aliyekuwa Mwandishi mkongwe hapa nchini,Marehemu Mayage S. Mayage nyumbani kwake leo,Mbweni jijini Dar es Salaam.
Mchungaji akiongoza misa ya kuombea mwili wa marehemu Mayage S. Mayage aliyewahi kuwa mwandishi wa habari leo nyumbani kwake Mbweni jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wanafamilia wa marehemu, ndugu na jamaa wakiwa fuatilia ibada ya kuagwa kwa aliyekuwa mwandishi mkongwe Mayage S. Mayage nyumbani kwake Mbweni Kijijini leo.
 Neno la Mungu likisomwa 

Mbunge wa Mtama na Waziri wa zamani wa Habari, Nape Nauye na Katibu Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole pamoja na ndugu na jamaa wakiwa kwenye ibada ya mazishi Marehemu Mayage S. Mayage aliyewahi kuwa mwandishi wa habari leo nyumbani kwake Mbweni jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wakiwa kwenye ibada ya kuagwa kwa mwili wa Marehemu Mayage S. Mayage aliyewahi kuwa mwandishi wa habari leo nyumbani kwake Mbweni jijini Dar es Salaam.