Wednesday, December 30, 2015

KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI AFUNGUA MAFUNZO YA AWALI KWA WATUMISHI WA IDARA YA WAKIMBIZI, LEO JIJINI DAR ES SALAAM

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil akizungumza  na washiriki  wa Mafunzo ya awali kwa Watumishi wa Mkataba wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi(hawapo pichani),wakati alipofungua mafunzo hayo yenye lengo la kuwajengea uwezo watumishi wapya, katika ukumbi wa mikutano wizarani hapo,jijini Dar es Salaam.Kulia ni  Kaimu Mkurugenzi Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, Numbilya Mpolo.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mbarak Abdulwakil akizungumza  na washiriki  wa Mafunzo ya awali kwa Watumishi wa Mkataba wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi wakati alipofungua mafunzo hayo yenye lengo la kuwajengea uwezo watumishi wapya, katika ukumbi wa mikutano wa wizara, jijini Dar es Salaam.Kulia ni  Kaimu Mkurugenzi Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, Numbilya Mpolo, kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa  Rasilimali Watu wa Wizara hiyo, Lilian Mapfa .

Washiriki wa Mafunzo ya awali kwa Watumishi wa Mkataba wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil(hayupo pichani), wakati alipofungua mafunzo hayo katika ukumbi wa mikutano wizarani hapo,jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa  Rasilimali Watu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Lilian Mapfa, akizungumza na washiriki wa Mafunzo ya awali kwa Watumishi wa Mkataba wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi(hawapo pichani),kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Utawala na Usimamizi wa Idara ya Wakimbizi, Deusdedit Masusu.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil(watatu kutoka kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Mafunzo ya awali kwa Watumishi wa Mkataba wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, muda mfupi baada ya kufungua mafunzo hayo katika ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam wanne kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa  Rasilimali Watu wa Wizara hiyo, Lilian Mapfa na wa pili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi  wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, Numbilya Mpolo .(Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,MOHA).Imeandaliwa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali-Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

No comments: