Wednesday, September 28, 2011

Kampeni za helikopta Igunga za nini??

Helkopta ya itakayotumiwa na mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF) ikiwasili katika uwanja wa Barafu uliopo Igunga Mjini kwa ajili ya kampeni za mgombea ubunge katika jimbo hilo jana.

Helikopta iliyokodishwa Chadema, ikipita juu ya Anga ya Igunga baada ya kuwasili jana alasili kwa ajili ya mikutano ya mwisho ya kampeni ya chama hicho.
Helikopta ya iliyokodishwa na CCM ikitua katika uwanja wa Sabasaba mjini Igunga jana kwa ajili ya kampeni za mwisho za chama hicho.
Hivi resources zote hizi zinazotumika kukampeni huko jimbonio Igunga zingetumika kununulia madawa, kusaidia elimu, barabara na kadhalika katika kipindi cha kabla na baada ya kampeni si ingekuwa ni bora zaidi kuliko ilivyo sasa, hivi wananchi wa Igunga wanahitaji helikopta kweli, je wananchi wa Igunga ni washamba kiasi hicho?
Ni kweli baadhi ya maeneo yapo mbali sana na si rahisi kuyafikia,lakini maswali ni mengi mno kuliko majibu. Ujio wa helikota hizi unaonyesha kuna tatizo kubwa sana la kisiasa na kijamii nchi mwetu. Uongozi unatafutwa kwa fedha nyingi sana mpaka inatisha.

Tuesday, September 27, 2011

Chadema Igunga: Pepople's Powerrrrrrr


Mwenyekiti wa Chama cha Chadema Freeman Mbowe akihutubia mkutano wa kampeni katika Kata ya Nkinga wa kuwania kiti cha Ubunge cha jimbo la Igunga baada ya kuwasili na Helkopta jana.Picha na Fidelis Felix

IGP Mwema apata ajali


IGP Said Mwema ((Pichani aliyenyoosha mkono) amenusurika katika ajali ya gari iliyotokea jana (Pichani) iliyotokea barabara ya Kivukoni front mbele ya ofisi za takwimu na wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa majira ya saa 8 mchana. Gari ya IGP ilikuwa inatokea magogoni iligongana na gari dogo (Saloon) T 960 AYK gari ya IGP iliumia sana upande wa mbele kushoto.
Picha na: DEUSDEDIT MOSHI WA DM.PHOTO SOLUTIONS (TZ)

Monday, September 26, 2011

Rais Kikwete arejea nchini


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda muda mfupi baada ya kuwasili kutoka New York Marekani ambapo pamoja na mambo mengine alihutubia baraza la Umoja wa Mataifa. Kushoto no Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick
(picha na Freddy Maro).

Friday, September 23, 2011

Michael Sata ni Rais mpya wa Zambia

Kiongozi wa upinzani Micheal Sata ametangazwa kuwa rais mpya wa Zambia mapema hii leo baada ya uchaguzi uliokumbwa na vurugu zilizosababisha vifo vya watu wawili.

Tume ya taifa ya uchaguzi nchini humo ilisema Sata alishinda asilimia 43 ya kura dhidi ya asilimia 36 za rais anayeondoka Rupiah Banda licha ya kuwa vituo 7 kati ya 150 vya upigaji kura nchini humo vilikuwa bado vinaendelea kuhesabu kura hizo.

Tume hiyo ya uchaguzi ilisema kuwa idadi ya wapiga kura katika maeneo hayo ni ndogo ikilinganishwa na kura laki moja elfu 88 zilizo watofautisha wagombea hao wawili. Wagombea wengine 8 waligawanya kura zilizosalia.

Jaji mkuu Ernest Sakala alimtangaza Micheal Chilufya Sata kuwa rais aliyechaguliwa wa jamhuri ya Zambia.

Punde baada ya kutolewa tangazo hilo muda mfupi baada ya saa sita usiku kuamkia leo, wafuasi wa Sata walimiminika barabarani katika mji wa Lusaka wakisherehekea huku wakipiga honi za magari.

Polisi ya kupambana na fujo ilikuwepo ikitazama wafuasi hao wakisherehekea.

Ilisema kuwa watu wawili waliuawa hapo jana katika vurugu zilizozuka baada ya wafuasi wa Sata kulalamikia utaratibu na udanganyifu katika zoezi la kuhesabu kura hizo.

Waangalizi wanasema hawajapata ushahidi wa kuthibitisha tuhuma hizo za udanganyifu huku waangalizi wa Umoja wa Ulaya wamekilaumu chama cha Banda MMD, kwa kutumia vibaya rasilimali za serikali, zikiwemo vyombo vya habari na magari wakati wa kampeni.

Hii ilikuwa ni mara ya nne kwa Sata kugombea wadhifa wa rais na ushindi wake unakifanya chama chake cha Patriotic Front kuwa chama cha tatu pekee kuingia uongozini tangu nchi hiyo kujinyakulia uhuru kutoka kwa Uingereza mnamo mwaka 1964.

Chama cha Banda ambacho Sata alikuwa mwanachama hadi mwaka 2001 kufuatia mzozo wa uongozi, umekuwa uongozini kwa miongo miwili.

Licha ya kuwa kiongozi huyo mpya ni mwenye umri wa miaka 74, mvuto wake ulikuwa zaidi kwa vijana nchini humo na watu wasiokuwa na ajira, wanaoona kuwa wametengwa kutoka biashara ya uchimbaji madini ya shaba nchini humo iliyoufanya uchumi wa nchi hiyo kuwa mojawapo ya unaofanya kazi vizuri Afrika.Biashara hiyo imesaidia kuundwa nafasi laki moja za ajira nchini Zambia na serikali imejenga madaraja, viwanja vya ndege hospitali kutoka fedha zinazopatikana kwa uchimbaji madini ya shaba.

Sata alikuwa gavana wa jimbo na waziri bungeni, alishindwa kwenye uchaguzi mnamo mwaka 2001 na pia mwaka 2006 kwa Levy Mwanawasa wa chama hicho cha MMD. Na baadaye mwaka 2008 wakati Mwanawasa alipofariki kutokana na kiharusi, Sata alishindwa na Banda ambaye aliyekuwa makamu wa rais wa Mwanawasa, kwa tofauti ndogo ya kura kwenye uchaguzi maalum uliofanyika.

Rais Kikwete akisalimiana na kiongozi wa serikali ya mpito ya Libya Bw. Mustafa Abdel-Jalil

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika maongezi mafupi na kiongozi wa serikali ya mpito ya Libya Bw. Mustafa Abdel-Jalil
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na kiongozi wa serikali ya mpito ya Libya Bw. Mustafa Abdel-Jalil jijini New York ambako wote wanahudhuria mkutano wa 66 wa Umoja wa Mataifa
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimtabulisha Balozi wa Kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa Mh Ombeni Sefue kwa kiongozi wa serikali ya mpito ya Libya Bw. Mustafa Abdel-Jalil
kwa kina hebu watembelee
http://mawasilianoikulu.blogspot.com/2011/09/rais-kikwete-akisalimiana-na-kiongozi.html

Wednesday, September 21, 2011

Ubalozi wa Marekani wadhamini wasanii washiriki wa tamasha la Mtemi Milambo


Wasanii wa muziki wa asili walioshiriki Tamasha la tatu ta Mtemi Milambo mwaka huu lililofanyika Julai 8-10,201 katika viwanja vya Uyui sekondari Tabora na kufunguliwa na aliyekuwa mkuu wa mkoa huo Mhe.Abeid Mwinyimussa wamepata udhamini wa kurekodi nyimbo za muziki wa asili za makabila ya Kisukuma na Kinyamwezi.
Wasanii waliofanya vizuri mwaka huu Ali Mango,Asha Kaombwe,Hamis Mpiga,Paulina Muhala,Paul Magadala wataungana na wasanii wengine wa miaka iliyopita na kuunda bendi ya muziki wa asili iitwayo Mwana Milambo ambayo itakuwa inapiga muziki huo katika mahoteli,maharusi na kumbi mbalimbali za burudani.
Nyimbo zitakazorekodiwa ni Kamnyagara kane, Usoga wi kuwa, Kushoke kukaya, kana nabuta, Sensema malunde, Ng,ombe yalala, Wela wa kulya, Nzagamba ya Sukuma na Miaka hamsini ya Uhuru
Lengo kuu ni kuzihifadhi nyimbo mbalimbali zilizotumiwa na wazee wetu wa kale katika vita, kilimo, harusi,na mazishi.
Nyimbo hizi nyingi huimbwa sehemu mbalimbali lakini ni muhimu kuzirekodi kwa ajiri ya faida ya vizazi vya baadae.
Nyimbo hizo zote zitarekodiwa katika studio ya Aegies chini ya muandaaji maarufu Peter John a.k.a Nice P.
Aksanteni kwa kunisikiliza.
Amon Mkoga
Mkurugenzi Mtendaji wa Chief Promotions.
www.chiefpromotions.or.tz
0755 638 004/0655 638 004

MAGONJWA YASIYO AMBUKIZI YANAONGEZA UMASKINI-TANZANIA


Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeungana na mataifa mengine duniani katika majadiliano ya kufatufa njia muafaka na zenye gharama nafuu za kuudhibiti na kutibu magonjwa yasiyo ambukizi.
Akizungumza kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Kikwete. Waziri wa Afya na maendeleo ya jamii kutoka Serikali ya mapinduzi Zanzibar, Mhe. Juma Duni Haji, amesema , magonjwa yasiyo ambukizi yanaendelea kuwa mzigo mkubwa hususani kwa familia maskini.
Wakuu wa Nchi na Serikali kutoka nchi 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa, wamekutana kwa siku(jumatatu na jumanne) mbili kujadiliana na kubadilishana uzoefu kuhusu magonjwa manne ambayo si ambukizi. Magonjwa hayo ni Kansa, Kisukari, Ugonjwa wa Moyo na Ugonjwa wa Mapafu.
“Gharama za kutibu magonjwa haya ni mkubwa mno. Karibu kila familia ambayo imeathirika na moja ya magonjwa haya inatumia asilimia 40 ya kipato chao kugharamia matibabu. Haya ni magonjwa yanayosababisha familia nyingi kuwa maskini” akasema Waziri Duni ambaye ni kati ya mawaziri watatu walioambatana na Mhe. Rais Kikwete kuhudhuria Mkutano Mkuu wa 66 wa Umoja wa Mataifa ambao unaanza siku ya jumatano..
Mkutano wa Kilele kuhusu magonjwa yasiyo ambukizi ni kati ya mikutano kadhaa ya kilele ambayo inafanyika kabla ya Mkutano Mkuu.
Kutoka na gharama kubwa ya kutibu magonjwa hayo, Waziri Juma Duni amesema, Tanzania inasisitiza umuhimu wa magonjwa hayo kuingizwa katika ajenda za Kimataifa za Maendeleo.
Akasisita kuwa ongezeko la magonjwa yasiyo ambukizi kumesababisha changamoto kubwa katika mfumo uliopo wa utoaji wa huduma za afya.
Akizungumzia uzoefu wa Tanzania , Waziri amesema serikali ilizindua mwaka 2009 mkakati wa kitaifa kuhusu magonjwa yasiyo ambukizi. Mkakati huo unalenga pamoja na mambo mengine kuhakikisha upatikanaji wa huduma za afya pamoja na utudhibiti wa magonjwa hayo.
Aidha akaainisha kwamba kama nchi, Tanzania inakabiliwa na changamoto mbili kwa pamoja. Changamoto hizo ni kukabiliana kwanza, na magonjwa yasiyo ambukizi na ya pili ni kukabiliana na magonjwa ambukizi.
Kutokana na changamozo hizo, Waziri Duni anasema kuwa si vema basi aina moja ya ugonjwa ikatiliwa mkazo na kupewa kipaumbele dhidi ya ugonjwa mwingine kwa kuwa yote yanashabihiana.
Aidha amezitaja changamoto nyingine zinazoikabili Tanzania kuwa ni ongezeko la kansa ya shingo ya uzazi, ongezeko la wagonjwa wa kisukari wa asilimia tano, uvutaji wa sigara kwa asilimia 10, ongezeko la watu wenye utizo wa kupita kiasi, unywaji wa pombe na maelfu ya watoto wanaozaliwa wakiwa na matatizo ya sickle –cell kila mwaka.
Mwishoni wa Mkutano huo, viongozi wa kuu wa nchi na serikali walipitisha tamkio la kisiasa ambalo licha ya kukiri kwamba magonjwa hayo manne ni changamoto ya katika karne ya 21.Pia wamemtaka Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na Mtendaji Mkuu wa Shirika la Afya Duniani ( WHO)na wadau wengine kuandaa taarifa itakayowasilishwa kwa viongozi hao katika Mkutano Mkuu wa 67 wa Umoja wa Mataifa.
mwisho

Tuesday, September 20, 2011

Rais Kikwete apata tuzo,pia ashiriki shughuli mbalimbali New York

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiikabidhi tuzo hiyo kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernard Membe baada ya kuipokea. Nyuma ya Mh. Membe ni Balozi wa Kudumu katika Umoja wa Mataifa Mh Ombeni Sefue (kushoto) na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mh Mwanaidi Maajar
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipewa tuzo na Waziri Mkuu wa Antigua and Barbuda Mh. Winston Baldwin Spencer kwa mchango wake mkubwa katika sekta ya afya, teknolojia na maendeleo kwenye hafla ya chakula cha usiku iliyoandaliwa na taasisi ya South-South katika hoteli ya Waldorf Astoria jijini New York Jumatatu usiku. (Picha kwa hisani ya Ikulu)

Dk Kafumu akikampeni Igunga


Mgombea ubunge jimbo la Igunga mkoani Tabora, kwa tiketi ya CCM, Dk Dalaly Peter Kafumu akihutubia mkutano wa kampeni jana katika kata ya Mwisi jimboni humo.

Chadema wawashabikia waliomvamia DC



Wanachama wa CHADEMA mjini Igunga, jana walijawa na furaha kubwa wakati wakiwapokea wabunge wao waliokamatwa hivi karibuni na kuwekwa rumande mjini Igunga na baadae kuhamishiwa kituo cha polisi mkoani Tabora kwa kosa la kumsukasuka mkuu wa Wilaya ya Igunga, Fatuma Kimario. Wabunge hao ni Sylivester Kasulumbai, mbunge wa Maswa Mashariki, Suzani Kiwanga, ambae ni mbunge wa viti maalumu.

Monday, September 19, 2011

Rais Ali Mohammed Shein awapa pole Mtambwe


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,akizungumza na wananchi wa familia 70 wa Kisiwani Piki na Mzambaun Takao,waliofiliwa na jamaa zao katika ajali ya Meli ya Mv Spice Islander,hivi karibuni, akiwa katika ziara maalum ya kuwapa pole wananchi waliofili na jamaa zao katika kisiwa cha Pemba.

Waziri wa Ardhi,Makaazi,maji na Nishati Mhe Ali Juma Shamuhuna,akiwapa pole wananchi wa Mtambwe Daya waliofiliwa na jamaa zao katika ajali ya Meli ya Mv Spice Islander,iliyozama katika mkondo wa Nungwi kaskazini Unguja ikielekea Pemba,hivi karibuni

Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwamamwema Shein,akiwapa pole wananchi wa Mtambwe Daya waliofiliwa na jamaa zao katika ajali ya Meli ya Mv Spice Islander,iliyozama katika mkondo wa Nungwi kaskazini Unguja ikielekea Pemba,hivi karibuni.

ATUHUMIWA KESI YA MELI WAPEWA DHAMANA BILA KUJUA TAREHE YA KWENDA TENA KORTINI


Watuhumiwa wa kesi ya mauajia ya meli ya Mv Spice iliyotokea Septemba 10 mwaka huu katika eneo la Nungwi Kisiwani Unguja Mjini Zanzibar na kuuwa watu zaidi ya 200,wakifikishwa Mahakama Kuu ya Zanzibar,wa mbele ni Nahodha Msaidizi wa meli hiyo Abdalla Moh'd Ali (30) katikati ni Yusufu Suleiman Jussa (47) ambaye ni mmiliki wa meli hiyo na mwisho ni Simai Nyange Simai (27) ni msimamizi wa bandari ya Malindi .Picha na Jackson Odoyo

****************************
Watuhumiwa watatu kati ya wanne waliofikishwa kwenye Mahakama Kuu Mjini Zanzibar wiki iliyopita wakikabiliwa na kosa la uzembe na kusababisha vifo vya watu 203 waliokuwa wakisafiri kwa Meli ya MV Spice Islander na kuzama katika bahari ya Hindi, Septemba 10 2011, wamepewa dhana na haikutaja siku ya kurejea tena Mahakamani hapo.

Watuhumiwa waliopewa dhamana ni Abdallah Mohammed Ali(30) mkazi wa Bububu, ambaye ni Afisa Mkuu wa Meli ya MV Spice Islander, Yussuf Suleiman Jussa(47), mkazi wa Kikwajuni ambaye pia ni Mmoja wa Wamiliki wa Meli na Msimamizi Mkuu wa Mizigo katika meli hiyo na Simai Nyange Simai(27) mkazi wa Mkele, ambaye ni Mfanyakazi wa Mamlaka ya Mamlaka ya Usafiri Baharini anayehusika na usalama wa abiria melini.

Watuhumiwa hao, Ijumaa iliyopita walirejeshwa rumande baada ya kuzuka mabishano ya kisheria ya kutaka wapewe dhama ama wasipewe, ambapo Mrajisi wa Mahakama Kuu Zanzibar Mh. George Kazi, aliamuru warejeshwe rumande hadi leo Jumatatu atakapotoa uwamuzi wake.

Walipofikishwa Mahakamani hapo hii leo, Wakili wa Utetezi Bw. Hamidi Ali Saidi Mbwezeleni aliiomba Mahakama iwaachie huru watuhumiwa hao ili tume iliyoteuliwa na Rais kuchunguza chanzo cha kuzama kwa meli hiyo iendelee na kazi yake la sivyo tume isitishe kazi yake hadi pale kesi itakapomalizika.

Wakili huyo amesema kuwa kutakuwa na utata kama watuhumiwa wataendelea kubaki rumande kwani watakosa haki yao ya msingi katika tume iliyoundwa na Rais wa Zanzibar wakati ikiendelea na kazi yake endepo itataka kupata taarifa ama maoni kutoka kwa watuhumiwa hao hivyo wakiwa mahabusu watakosa haki yao ya kujieleza mbele ya tume hiyo.

Amesema hivi sasa inaonekana kuna makundi mawili yanayofanya kazi moja kwa maana ya Mahakama na Tume jambo ambalo alisema litakuwa na utata na lenye makusudio ya kuwalinda baadhi ya watu fulani.


Waziri Maghembe afanya ziara ya ghafla sokoni


Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika, Profesa Jumanne Maghembe akinunua sukari ya kilombero katika Soko la Kipati, Mbagala Jijini Dar es Salaam leo. Sukari hiyo ilikuwa ikiuzwa Shilingi 1,900 kwa kilo moja.

Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika, Profesa Jumanne Maghembe akipata maelezo kutoka kwa Bwana Harshid Chavda mwakilishi wa Kiwanda cha Sukari Kilombero kuhusu kiwango cha uzalishaji kwa siku na kiasi kinachouzwa kwa wasambazaji katika Mkoa wa Dar es Salaam kwa kila siku wakati Waziri alipofanya ziara ya dharura katika ofisi za kiwanda hicho, Gerezani Jijini Dar es Salaam.

Sunday, September 18, 2011

Soko jingine laungua Mbeya


Soko hilo likiungua kwa moto ambao bado haujafahamika chanzo chake.

SOKO dogo lililopo eneo la Forest ya zamani, karibu na Chuo Kikuu cha Mzumbe na Chuo Kikuu Huria jijini Mbeya, limeteketea kwa moto jana usiku. Inadaiwa moto huo ulianza majira ya saa 3 za usiku na kudhibitiwa na zimamoto kabla ya kuleta madhara zaidi.

Tukio hili limetokea ikiwa ni siku moja kutoka soko lingine la Mwanjelwa eneo la SIDO kuteketea kwa moto na kusababisha hasara kubwa. Matukio haya yanayotokea jijini Mbeya yanaacha maswali mengi kwa wananchi kiasi cha kuhoji 'KUNANI MBEYA ?'

Picha kwa hisani ya Mbeya Yetu Blog

Dua wa kuwaombea wahanga wa Mv Spice Island


Viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini wilayani Arusha wakiwa katika dua ya pamoja katika ukumbi wa CCM mkoa wa Arusha ili kuwaombea marehemu na waathirika wa ajali ya meli ya MV Spice Island iliyotokea mjini Zanzibar wiki iliyopita na kusababisha vifo vya watu 204 na kujeruhi zaidi ya 500,katika dua hiyo pia jumla ya shilingi milioni 3.6 ilichangishwa kama rambirambi ya ajali hiyo(Picha na Happy Lazaro).

Mambo ya vurugu Igunga


Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM (NEC) ambaye pia ni mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde akimuonyesha afisa wa polisi kioo cha nyuma cha gari aina ya Toyota Prado T 888 ALL lililorushiwa mawe jana katika kijiji cha Nkinga kati na vijana wanaodhaniwa ni wafuasi wa Chadema. (Picha na Daniel Mjema)

Friday, September 16, 2011

Wakuu wa mikoa wapishwa

Daniel Ole Njoolay na Stella Manyanya
Rais Kikwete akimkabidhi buku Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Fatma Mwassa
Rais Kikwete akimkabidhi buku Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro

Picha ya Rais Kikwete pamoja na wakuu wa mikoa ya Tanzania bara


RAIS Jakaya Kikwete jana aliwaapisha wakuu wa mikoa 21 huku kila mmoja akieleza namna alivyopata mstuko kufuatia uteuzi huo.
Wakuu wa mikoa walioapishwa

Wakuu wa mikoa walioapishwa ni mikoa yao kwenye mabano ni Mwantumu Mahiza (Pwani), Ludovick Mwananzila (Shinyanga) na Joel Bendera (Morogoro).

Wengine ni Parseko Kone (Singida), John Tupa (Mara), Said Mwambungu (Ruvuma), Chiku Galawa (Tanga), Leonidas Gama (Kilimanjaro) na Dk Rehema Nchimbi (Dodoma)

Wengine walioapishwa ni Erasto Mbwilo (Manyara), Kanali Fabian Massawe (Kagera), Fatuma Mwasa (Tabora), Ali Rufunga (Lindi), Ernest Ndikilo (Mwanza) na Magesa Mulongo (Arusha).

Wengine ni Abbas Kandoro (Mbeya) Issa Machibya (Kigoma), Joseph Simbakalia (Mtwara).

Soko la Mwanjelwa-2 lateketea kwa moto





SOKO la Sido lililojengwa na kutumika baada ya kuungua moto kwa Soko kuu la Mwanjelwa jijini Mbeya mwaka 2006, nalo limeteketea kwa moto, kujeruhi watu 20 na kusababisha upotevu mkubwa mali.

Tukio hilo lililosababisha vilio, simanzi na hofu kwa wafanyabishara sokoni hapo limekuja takriban miaka minne na nusu tangu soko la Mwanjelwa liungue moto Desemba, 2006.

Habari zimeeleza kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa 3 asubuhi baada ya eneo la katikati ya soko kulipuka na kuwaka moto katika kipindi ambacho tayari wafanya biashara wameanza kufungua bidhaa zao.

Mashuhuda wa tukio hilo waliklieleza gazeti hili kuwa waliona moto huo katikati ya soko na wafanyabiashara wakijitahidi kuuzima bila mafanikio.

“Kwa kweli moto ni mkubwa na hatujui chanzo chake nini kwani ghafla tumeona moto ukiwaka eneo la soko upande wa katikatika wa soko hilo hivyo kila mtu anashangaa ulikoanzia moto huu,”alisema mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Francis James

Alisema kuwa magari ya zimamoto ya halmashauri ya jiji la mbeya yamefika eneo la tukio lakini yameshindwa kuuzima moto huo baada ya kuonesha kuongezeka kwa kasi kuwa mkubwa na badala yake wananchi kufanya juhudi ya kuokoa mali zao.

“Kwa sasa tayari jeshi la polisi limefika hapa kwa ajili ya kuwasaidia wananchi kuokoa mali zao ikiwa ni pamoja na kuzuia vibaka kuiba mali za watu kwani hali ni mbaya wafanyabiashara na wananchi wengi wamechanginikiwa kutokana na magari hayo kushindwa kuzima moto huo,”alisema

Akizungumza na Mwanachi Katibu wa soko kuu la zamani la Mwanjelwa Godfrey Haule alisema kuwa uwezekano wa kuuzima moto ni mgumu kutokana na moto kuendelea kuongezeka kwa kasi na kwamba gari la zimamoto limeondoka eneo la tukio baada ya kuishiwa maji na kwenda kuongeza maji.

Haule alisema kuwa moto huo ulianza kuwaka katika ya soko katika vibanda vya wakina mama lishe (mama ntilie) ambapo moto huo ungeweza kuzimwa mapema lakini walishindwa kufanya hivyo kutokana na kukosa maji kwa sababu mabomba ya yaliyopo katika soko hilo hayatoi maji na hivyo kusubiria magari ya ziamoto ambayo pia yameshindwa kuuzima moto huo.

“Mabomba ya soko yangekuwa yanatio maji tungefanikiwa kuuzima moto mapema lakini tulishindwa baada ya kwenda kungulia mabomba hayo yakakawa hayatoki maji na lilikuja hapa gari la zimamoto pia limeshindwa kuuzima moto huo kutokana na kuwa mkubwa walivhoambulia na kiushiwa maji katioka gari na kwenda kuongeza mengine,”alisema

Thursday, September 15, 2011

Meli zingine mbili zazima injini zikitokea bara na Zanzibar

Boti zazimika baharini
Boti ya Sea Star iliyokuwa imebeba abiria 134 na kuanza safari ya kutoka Unguja kuelekea Pemba, ilitumia dakika 20 tu baharini kabla injini yake moja kuzimika muda mfupi kabla ya kufika eneo la Chumbe.

Mkuu wa gati ya abiria ya Malindi Zanzibar, Basha Haji Salehe alisema baada ya kutokea kwa hitilafu hiyo, nahodha wa boti hiyo alipiga simu bandarini na akamriwa akatishe safari.

Afisa wa usafirishaji wa boti hiyo, Mussa Salum Ali alisema hitilafu ilitokana na mafuta yaliyotumika siku hiyo ambayo baadaye walibaini kuwa yalikuwa yamechanganywa na maji.

Alisema tayari wametoa taarifa katika kituo ambacho wamechukua mafuta hayo na uchunguzi unaendelea na kwamba ikithibitika watarejeshewa gharama zao.

Kwa upande wake, Boti ya Sea Bus II iliyokuwa inatoka kisiwani Pemba kuelekea Unguja, ililazimika kukatisha safari kutokana na injini yake moja pia kuzimika.

Boti hiyo iliyokuwa na abiria 138, ilikatisha safari katika kisiwa cha Matumbini na kulazimika kurudi Mkoani ambako iliagizwa boti nyingine ya kampuni hiyo ya Sea Bus III kwa ajili ya kuwasafirisha abiria waliokwama.

Jiji la Dar es Salaam

Hapo ni eneo la katikati ya jiji
Posta ya zamani eneo la kihistoria pengine hii ndo alama pekee ukiacha St Joseph na Azania Front zinazoitambulisha Dar es Salaam.
Hapo ni eneo la Wizara ya Ardhi na kwa nyuma yake jengo la wizara ya Ardhi
Ferry Kigamboni

Jiji la Dar es Salaam linakua kwa kasi ni miongoni ma majiji 10 yanayokua kwa kasi duniani, Dar ni ya tisa,
Kukua kwa jiji hili kumeongeza changamoto kila kukicha

Wednesday, September 14, 2011

Dr Hawa Juma Ngasongwa off to US

Kenneth LuePhang, Contracting Officer for USAID at the U.S. embassy in Dar es Salaam presents a ticket to an International Visitors Leadership Program (IVLP) participant Dr. Hawa Juma Ngasongwa, a Medical Officer at the Department of Internal Medicine and member of the Tanzanian People's Defense Force who will participate in the Public Health and Infectious Disease Education and Prevention Program in the United States of America.

Kampeni za CCM Igunga


Wananchi wa Ziba Igunga Mkoani Tabora wakimsikiliza mgombea wa ccm Dk Dalaly Peter Kafumu kwenye mkutano wa kampeni za CCM za uchaguzi mdogo jimbo la Igunga. picha na Fidelis Felix

kampeni za Chadema Igunga

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Kinungu, katika mkutano wa kampeni za ubunge wa jimbo la Igunga jana.
Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki, Sylvester Kasulumbai akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Kinungu, ikiwa ni sehemu wa kampeni za ubunge wa jimbo la Igunga jana.

Tuesday, September 13, 2011

Rais Jakaya Kikwete afanya mabadiliko ya Wakuu wa Mikoa nchini

RAIS Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya Wakuu wa Mikoa nchini.
Katika mabadiliko hayo, amewateua Wakuu wa Mikoa wapya 15, kuwabadilisha vituo vya kazi Wakuu wa Mikoa watano na wengine saba wamestaafu kwa mujibu wa taratibu. Mkuu wa Mkoa wa Singida amebaki kwenye kituo chake cha kazi wakati Wakuu wa Mikoa wengine wanne watapangiwa kazi nyingine.

Aidha, Wakuu wa Mikoa mipya minne ya Simiyu, Geita, Katavi na Njombe itakayoundwa baada ya taratibu kukamilika watatangazwa baadaye.

Kwa mujibu wa mabadiliko hayo, Wakuu wa Wilaya 11 wamepandishwa Vyeo na kuwa Wakuu wa Mikoa kama ifuatavyo: Bw. John Gabriel Tupa ambaye anakuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara; Bw. Saidi Thabit Mwambungu (Ruvuma); Bi. Chiku S. Gallawa (Tanga); Bw. Leonidas T. Gama (Kilimanjaro); Dk. Rehema Nchimbi (Dodoma); Bw. Elaston Mbwillo (Manyara); Kanali Fabian Massawe (Kagera); na Bibi. Fatma Abubakar Mwassa (Tabora). Wakuu wa Wilaya wengine walioteuliwa ni Bw. Ali Nassoro Rufunga, (Lindi); Eng. Ernest Welle Ndikillo, (Mwanza); na Bw. Magesa Stanslaus Mulongo Mkuu wa Mkoa (Arusha).

Walioteuliwa nje ya nafasi hizo ni Eng. Stella Manyanya (Rukwa); Bibi Mwantumu Mahiza, (Pwani); Bw. Joel Nkaya Bendera (Morogoro) na Bw. Ludovick Mwananzila (Shinyanga).

Waliobadilishwa vituo vya kazi ni Bw. Abbas Kandoro anayekwenda Mbeya akitokea Mwanza; Bw. Said Mecki Sadiki anayekwenda Dar es Salaam akitokea Lindi; Bibi Christine Ishengoma anayekwenda Iringa akitokea Ruvuma; Lt. Kanali Issa Machibya anayekwenda Kigoma akitokea Morogoro; na Kanali Joseph Simbakalia anayekwenda Mtwara akitokea Kigoma. Dk. Parseko Ole Kone ataendelea kuwa Mkuu wa Mkoa wa Singida.

Waliostaafu ni Bw. Mohammed Babu, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera; Bw. Isidore Shirima aliyekuwa Arusha; Kanali (mst.) Anatory Tarimo aliyekuwa Mtwara; Bw. John Mwakipesile, aliyekuwa Mbeya. Wengine ni Kanali Enos Mfuru aliyekuwa Mara; Brig. Jen. Dk. Johanes Balele aliyekuwa Shinyanga; na Meja Jen. Mst. Said S. Kalembo aliyekuwa Tanga.

Wakuu wa Mikoa wanne waliostaafu ambao watapangiwa vituo vingine vya kazi ni Bibi Amina Mrisho aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani; Dk. James Msekela aliyekuwa Dodoma; Bw. Abeid Mwinyimusa aliyekuwa Tabora na Bw. Daniel Ole Njoolay aliyekuwa Rukwa.

Wakuu wote wa Mikoa waliopo sasa wameagizwa kuandaa Hati za Makabidhiano (Handing Over Notes) katika muda wa siku 14 kuanzia siku ya kuapishwa kwa Wakuu wapya wa Mikoa. Aidha Wakuu wa Wilaya ambao wamepandishwa vyeo kuwa Wakuu wa Mikoa nao wanapaswa kufanya hivyo hivyo kwa ajili ya Wakuu wa Wilaya watakaopangiwa vituo vitakavyokuwa vimeachwa wazi kutokana na uteuzi wao.

Wakuu wa Mikoa ile minne mipya na Wakuu wa Wilaya watakaoteuliwa hapo baadaye nao watatakiwa kuandaa Hati za Makabidhiano ndani ya siku 14 tangu kuapishwa.

Makabidhiano hayo lazima yahusishe pia kutembelea kwa pamoja baadhi ya maeneo na miradi ambayo ni muhimu kama sehemu ya makabidhiano yao.

Wakuu wote wa Mikoa walioteuliwa na Wakuu wa Mikoa minne mipya wakaoteuliwa pamoja na Wakuu wote wa Wilaya watakaoteuliwa baada ya zoezi kukamilika watatakiwa kuhudhuria mafunzo ya wiki tatu kwenye Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo, Dodoma kwa lengo la kuwajengea uwezo zaidi wa kiuongozi na kiutendaji.

Wakuu hao wapya wa mikoa wataapishwa siku ya Ijumaa, Septemba 16, 2011 saa 4.00 asubuhi kwenye viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam.
Wakuu hao wapya wa mikoa; vituo wanavyokwenda na vituo walivyotoka ni kama ifuatavyo:

Na.
JINA LA MKUU WA MKOA
KITUO AENDAKO
KITUO ATOKAKO
1.
Bw. Saidi Mecki Sadiki
DAR ES SALAAM
RC - Lindi
2.
Bw. John Gabriel Tupa
MARA
DC - Dodoma
3.
Bw. Saidi Thabit Mwambungu
RUVUMA
DC - Morogoro
4.
Kanali Joseph Simbakalia
MTWARA
RC Kigoma
5.
Bi. Chiku S. Gallawa
TANGA
DC - Temeke
6.
Bw. Abbas Kandoro
MBEYA
RC Mwanza
7.
Bw. Leonidas T. Gama
KILIMANJARO
DC – Ilala
8.
Dkt. Parseko Ole Kone
SINGIDA
RC Singida
9.
Eng. Stella Manyanya
RUKWA
Mbunge V/Maalum
10.
Bibi Christine Ishengoma
IRINGA
RC Ruvuma
11.
Dk. Rehema Nchimbi
DODOMA
DC - Newala
12.
Bw. Elaston John Mbwillo
MANYARA
DC – Mtwara
13.
Col. Fabian I. Massawe
KAGERA
DC - Karagwe
14.
Bibi. Mwantumu Mahiza
PWANI
Mbunge/NW Mstaafu
15.
Bibi. Fatma A. Mwassa
TABORA
DC - Mvomero
16.
Bw. Ali Nassoro Rufunga
LINDI
DC - Manyoni
17.
Eng. Ernest Welle Ndikillo
MWANZA
DC - Kilombero
18.
Lt. Col. Issa Machibya
KIGOMA
RC Morogoro
19.
Bw. Magesa S. Mulongo
ARUSHA
DC - Bagamoyo
20.
Bw. Joel Nkaya Bendera
MOROGORO
Mbunge/NW Mstaafu
21.
Bw. Ludovick Mwananzila
SHINYANGA
Mbunge/NW Mstaafu

Maafa ya Zanzibar

Katibu Mkuu kiongozi Philemon Luhanjo akitoa tamko la serikali kuhusiana na ajali ya meli ya Spice Islander iliyotokea mwishoni mwa wiki.
Rais Dkt.Jakaya mrisho Kikwete akitoa salamu zake za pole mara baada ya kumalizikia kwa dua ya pamoja iliyokuwa maalumu kuwaombea marehemu waliofariki katika ajali ya meli iliyotokea Unguja mwishoni mwa wiki.

Baadhi ya wananchi wa Zanzibar wakiswali wkati wa dua maalumu ya kuwaombea marehemu waliofariki katika ajali ya meli ya Spice Islander iliyotokea mwishoni mwa wiki eneo la Nungwi, Unguja. Swala hiyo ya pamoja ilifanyika jana Septemba 12 katika viwanja vya Maisara.
Balozi wa Marekani nchi Tanzania Alfonso Leinhardt akimfariji Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kufuatia ajali ya meli ya Spice Islanders iliyotokea huko Nungwi, Unguja juzi usiku ambapo watu zaidi 200 wamepoteza maisha na wengine 602 kuokolewa wakiwa hai.Picha na Freddy Maro
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwafariji na kuwapongeza wananchi wa kijiji cha Nungwi kufuatia juhudi zao za kujitolea kuwaokoa watu waliopata ajali katika meli ya MV Spice Islanders iliyotokea juzi usiku.Meli hiyo ilikuwa ikitokea Unguja kwenda Pemba amapo watu zaidi ya 200 wanahofiwa kufa maji.