Tuesday, February 09, 2010

Wahariri wa Mwananchi wamvaa Spika


Spika wa Bunge, Samuel Sitta (kushoto) akisalimiana na Mhariri wa gazeti la
Mwananchi Jumapili, Daniel Mwaijega na Mhariri wa makala wa Mwananchi,
Rashid Kejo (katikati) walipotembelea Bunge mjini Dodoma jana. Picha na
Edwin Mjwahuzi

Monday, February 08, 2010

Majaji waipeleka puta serikali suala la mgombea binafsi




NAIBU Mwanasheria Mkuu wa Serikali jana alikuwa kwenye wakati mgumu mbele ya jopo la majaji saba wa Mahakama ya Rufaa wakati mabosi wa mhimili wa sheria hao walipohoji umakini wake katika kushughulikia rufaa dhidi ya uamuzi wa kuruhusu mgombea binafsi.

Wakiongozwa na Jaji Mkuu Augustine Ramadhani, majaji hao waliamua kuwa hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu ya kuruhusu mgombea huru ndiyo inayotambuliwa wakati wa uchaguzi mkuu wa Oktoba na baadaye hadi hapo itakapoamuliwa vinginevyo.

Ilifikia wakati Jaji Mkuu Ramadhan alisema: “Inasikitisha kuwa (Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju) unatoka kwenye ofisi ya AG (Mwanasheria Mkuu wa Serikali), lakini unalalamika kuwa hujasoma list of authorities. Sijui tunawapa mfano gani wengine!”

Mahakama Kuu iliruhusu mgombea binafsi baada ya mwenyekiti wa chama cha kisiasa cha DP, Mchungaji Christopher Mtikila kufungua kesi akidai kuwa sheria za nchi kuhusu haki ya kupiga kura na kupigiwa kura inapingana na katiba ya nchi kutokana na kutamka kuwa mgombea ni lazima apitishwe na chama.

Lakini tangu hukumu hiyo ilipotolewa mwezi Juni, 2006 ikitaka mchakato wa kutunga sheria ya kuruhusu mgombea binafsi ufanyike katika kipindi cha miezi sita, hakuna kilichofanyika na badala yake serikali ilikata rufaa ikipinga mamlaka ya Mahakama Kuu kutafsiri katiba. Imeandikwa na James Magai na Hussein Kauli

Zantel yavuna wateja milioni 1.4


BAADA ya kununua vifaa vya kisasa pamoja na kutumia teknolojia ya kisasa kwa gharama nafuu kupitia uhusiano wake na Etisalat yenye wateja zaidi ya milioni 95 barani Afrika, mashariki ya kati na bara la Asia kampuni ya simu ya Zantel imeongeza idadi ya wateja wake hadi kufikia 1.4 milioni.

Kwa mujibu wa Mkuu mpya wa kitendo cha Biashara Zantel, Norman Moyo alisema kuwa Kampuni hiyo ndani ya hiyo miezi 18 imewekeza zaidi ya dola za kimarekani milioni 140 katika kuboresha mtandao wake na mafanikio yaliyopatikana ni ishara ya uwekezaji huo.

"Uwekezaji huu umejihidhirisha kwenye huduma kwa wateja wa Zantel na wateja wetu wameongezeka kutoka laki 9 hadi milioni moja na laki nne (million 1.4) ndani ya miezi 3 iliyopita,"alisema.

Alidokeza kwamba bado kuna Watanzania wengi ambao wanahitaji huduma za simu na internet na muhimu ni kulenga jamii ambazo bado hazijapata hizi huduma badala ya kugombania wateja sehemu moja.

Moyo, alisema Zantel sasa inazingatia kuongeza thamani kwa wateja wake pamoja na kuongeza huduma na bidhaa mpya sokoni.

Aliongeza kusema Zantel itawekeza kwenye maendeleo ya vijana na kuhakikisha maendeleo ya nchi yanapewa kipaumbele kwa kuwawezesha vijana. Moyo pia alisema Zantel ina nia ya kuongeza huduma zake vijijini kuwawezesha vijana wanaoishi vijijini kupata fursa ya kutumia huduma zitakazowasaidia kuendeleza maisha yao.

“Zantel kuungana na Etisalat inatupa nguvu kiuchumi haswa kwenye masuala ya kukunua vifaa na mitambo mipya ya kisasa pamoja na simu za kisasa kwani tunanunua kwa pamoja na sio kama Zantel peke yake. Unafuu huu ni faida kwa wateja wetu kwani wanapata simu nzuri na kwa bei nafuu wakati huo huo wakitumia mtandao wa kisasa na uliosambaa Tanzania nzima,” aliongeza Moyo.

Norman Moyo ni moja ya viongozi wapya waliotambulishwa kwa nia ya kuibadilisha kampuni ya Zantel. Akiwa na umri wa miaka 36 mkuu huyu wa kitengo cha biashara na ana uzoefu mkubwa katika sekta ya mawasiliano haswa kwenye kuyageuza makampuni kutoka kwenye hasara kuyafikisha kwenye faida.

Moyo ni mmoja ya wale waliobadilisha taswira ya masiliano nchini Zambia akiwa kama Mkurugenzi wa Masoko wa Celtel Zambia na baadaye kuwa Mkuu wa kitengo cha Masoko Celtel Nigeria na uteuzi wake ulibadilisha kampuni ya Celtel Nigeria hadi kuwa namba mbili kutoka wateja milioni 4.5 hadi wateja milioni 17 ndani ya miaka miwili na nusu.

Mnikulu Kianda kuzikwa Same


Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimfariji Khadija Kianda mjane wa Marehemu Rajabu Kianda aliyekuwa mnikulu kufuatia kifo chake kilichotokea jumapili jijini Dar es Salaam.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji Khadija Kianda ambaye ni mjane wa Marehemu Rajabu Kianda aliyekuwa Mnikulu ambaye alifariki dunia Jumapili jijini Dar es Salaam.Rais Kikwete alikwenda nyumbani kwa marehemu eneo la Mikocheni jijini Dar es Salaam kuifariji familia ya marehemu ambaye anatarajia kuzikwa huko Kihurio Same,Mkoani Kilimanjaro.Pembeni ni Mama wa Marehemu ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza la aliyekuwa mnikulu Bwana Rajabu Kianda aliyefariki jana jijini Dar es Salaam.Marehemu Kianda anatarajiwa kuzikwa kesho nyumbani kwao Kihurio Same Mkoa wa Kilimanjaro.
(Picha na Freddy Maro)

**********************************************************************************************************


MNIKULU Rajabu Kianda, aliyefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu, atazikwa katika kijiji cha Kihurio wilayani Same, Kilimanjaro.
Kiyanda alifariki juzi mchana akiwa Hospital ya Taifa Muhimbili (MNH) alikopelekwa kwa matibabu.
Mwili wa Kianda uliagwa jana nyumbani kwake Mikocheni mara baada ya kumalizika kwa kisomo majira ya saa 8:00 mchana, kwa mujibu wa ndugu yake ambaye aliomba jina lake lisitajwe.
Kianda alianza kuugua tangu mwishoni mwa mwakaa jana nafasi yake inakaimiwa na Shabani Gurumo.
Kianda aliteuliwa kushika nafasi ya Mnikulu baada ya Anthony Itatiro kuhamishiwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Imeandikwa na Sadick Mtulya.

Sunday, February 07, 2010

Aliyeongoza kidato cha nne


Mwanafunzi wa St Marian iliyopo Bagamoyo mkoani Pwani, Immaculate Mosha aliyeibuka mshindi wa kwanza wa kidato cha nne mwaka huu, mwenye blauzi ya rangi ya khaki kwa mbali kama nyeupe, akifurahia ushindi wake na ndugu zake nyumbani kwa kaka yake Mwenge, jijini Dar es Salaam jana. Picha na Salhim Shao.

Mzimu wa vitambulisho vya taifa



SAKATA la lililoibua mjadala mkubwa mwaka jana la mradi wa vitambulisho vya taifa na kumlazimu Rais Jakaya Kikwete kuingilia kati na kuagiza lishughulikiwe kwa haraka huenda likaisha ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

Mradi huo wa vitambulisho vya taifa ulioanza maandalizi mwaka 1995 na kupitishwa na kikao cha Bazara la Mawaziri kilichoketi Februari, 2007, hivi karibuni umekuwa unaandikwa zaidi kwenye vyombo vya habari hasa ikiwamo kuachwa kwa Kampuni ya Sagem ya Uswisi katika hatua ya pili ya kuwachuja wazabuni hao.

Akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo hii, Mkurugenzi Mtendaji wa NIDA, Dickson Maimu (pichani) alisema miradi 14 ndiyo itakayogharimu kiasi cha Sh 200bilioni.

Wiki ya saratani


Meneja huduma ya uuguzi wa Hospitali ya Mission Mikocheni ya jijini Dar es Salaam Valentina Msechu akimuelekeza Lidia Kijoza jinsi ya kujipima mwenyewe saratani ya matiti, hiyo inafanyika ikiwa ni katika wiki ya saratani iliyoanza kuadhimishwa wiki iliyopita. Picha na Mussa Mkama

Mizengo ndani ya magwanda ya CCM



Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwapungia wananchi wa Mpwapwa baada ya kuhutubia mkutubia katika sherehe za miaka 33 ya CCM mkoa wa Dodoma zilizofanyika kimkoa kwnye uwanja wa michezo wa Mpwapwa. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Dodoma na Mbunge wa Bahi, William Kusila.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mtoto Hussein ambaye kichwa chake ni kikubwa kiasi cha kumfanya ashindwe kutembea vizuri katika sherehe za miaka 33 ya CCM mkoa wa Dodoma zilizofanyika kimkoa kwenye uwanja wa michezo wa Mpwapwa Februari 6, 2010. Kushoto kwake ni Mkuu wa MKoa wa Dodoma, Dr. James Msekella.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Kilio tupu Kipawa





Mwenyekiti wa wakazi wa Kipawa jijini Dar es Salaam jana,Magnus Mulisa akimfariji mdogo wake Grace Bakuza baada ya nyumba zao kubomolewa jana,kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege wa Julius Nyerere.Picha na Zacharia Osanga






Msichana mkazi wa Kipawa jijini Dar es Salaam, ambaye jina lake halikuweza kufahamika maramoja akiwa amejiinamia kwenye godoro,baada ya nyumba yao kubomolewa jana ikiwa ni kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege wa Julius Nyerere.Picha ndogo kulia ni Mwenyekiti wa wakazi wa Kata hiyo Magnus Mulisa.Picha na Zacharia Osanga

Friday, February 05, 2010

Umuhimu wa mambloga waanza kujionyesha Bongo


Wanalibeneke na vyeti vyao vya shukurani toka Serengeti ambao kwa mara ya kwanza wameonesha mfano wa kutambua umuhimu wa globu na kuwaenzi waendeshaji wake. Toka shoto ni Ankal wa Globu ya Jamii, John Bukuku wa Fullshangwe.blogspot, Geofrey Mwakibete wa Mohammeddewji.com, Muhidin Sufiani wa Sufianimafoto.blogspot.com na Michuzijunior wa Jiachie. Picha kwa hisani ya issamichuzi.blogspot.com

Breaking Newssss Jerry Muro Kizimbani

JESHI la Polisi limemfikisha mahakamani mwandishi wa habari , Jerry Muro, ambaye ni maarufu kwa kufichua uozo, baada ya kumkamata kwa tuhuma za kudai rushwa kwa nguvu.

Kafikishwa katika mahakama ya Kisutu asubuhi hii watu kibao wamemiminika kushuhudia tukio hilo lililogusa hisia za watu wengi.

Muro, mfanyakazi wa Shirika la Utangazaji (TBC), anadaiwa kutaka fedha kwa njia ya vitisho kutoka kwa mhasibu aliyesimamishwa wa Halmashauri ya Bagamoyo, Michael Wage.Taarifa zaidi tutawaleteeni baadaye.

----------------------------------------------------------------------------------

Jerry Muro apandishwa kizimbani

HATIMAYE mtangazaji wa kituo cha televisheni cha Shirika la Utengazaji (TBC1), Jerry Muro jana alipandishwa kizimbani akishtakiwa kwa mashtaka ya kula njama na kuomba rushwa ya Sh10 milioni.
Muro, ambaye ni mtangazaji wa kipindi maarufu cha Usiku wa Habari cha televisheni hiyo ya serikali, alifikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana baada ya kukamatwa Jumapili iliyopita katikati ya jiji la Dar es salaam.
Mtangazaji huyo, ambaye alichomoza kutokana na kuripoti habari zilizofichua rushwa inayofanywa na askari wa kikosi cha usalama barabarani, alipandishwa kizimbani akiwa na wenzake wawili ambao inadaiwa alishirikiana nao katika kutenda kosa hilo. Wawili hao walisomewa mashtaka matatu.
Washtakiwa hao wote walifikishwa mahakamani hapo wakiwa chini ya ulinzi mkali wa askari waliokuwa wamevalia nguo za kiraia.
Muro ameunganishwa na watu hao katika shtaka la kula njama na kuomba rushwa ya Sh10 milioni, lakini wawili hao walisomewa mashtaka mengine matatu ya kujifanya wafanyakazi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).
Wakili mwandamizi wa serikali, Boniface Stanslaus akishirikiana na mwendesha mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Ben Lincoln waliwataja washtakiwa wengine waliopandishwa kizimbani na Muro kuwa ni Edmund Kapama, maarufu kama Doctor, na Deogratias Mgasa ambaye ni maarufu kama Musa.
Stanslaus, ambaye aliisoma hati ya mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Gabriel Mirumbe, alidai kuwa Muro na wenzake walikula njama na kuomba rushwa ya fedha hizo mwezi Januari, jambo ambalo alisema ni kinyume cha kifungu cha 15 (1)(a) cha Sheria ya Kuzia ya Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007.
Wakili Stanslaus alidai katika shtaka la pili kuwa Januari 29 mwaka huu katika hoteli ya Sea Cliff wilayani Kinondoni, Jerry Muro, akiwa mwajiriwa wa TBC1, aliomba rushwa ya Sh10 milioni kutoka kwa mhasibu wa zamani wa Halmashauri ya Bagamoyo, Michael Wage Karoli.
Alidai Muro aliomba kiasi hicho cha fedha ili asitangaze habari za Kalori zinazohusu matumizi mabaya ya fedha za umma.
Kwa sasa Wega, na wafanyakazi wengine watatu wa halmashauri hiyo, amesimamishwa kazi kutokana na tuhuma za matumizi mabaya ya fedha za umma. Alisimamishwa kazi na Waziri Mkuu Mizengo Pinda alipotembelea wilaya hiyo baada ya ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG) kuonyesha mapungufu makubwa kwenye matumizi ya fedha.
Katika shtaka la tatu, Stanslaus alidi kuwa siku ya tukio washtakiwa Edmund Kapama na Deogratias Mgasa walijipachika nyazifa zisizokuwa zao.
Aliongeza kudai kuwa washtakiwa hao wakiwa katika hoteli hiyo ya Sea Cliff walimlaghai Wega kwa kuwa wao ni maofisa wa Takukuru huku wakijua ni uongo.
Baada ya kumaliza kuwasomea mashtaka hao, washtakiwa wote walikana na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
Hakimu Mirumbe aliwaachia huru washtakiwa Jerry Muro na Edmund Kapama baada ya kukamilisha masharti ya dhamana waliyopewa.
Washtakiwa hao waliachiwa mara baada ya kila mmoja kusaini dhamana ya Sh5 milioni na wadhamini wawili, kila mmoja akisaini dhamana ya kiasi hicho cha fedha.
Mshtakiwa wa tatu, Mgasa alirudishwa rumande kwa kushindwa kukamilisha masharti hayo ya dhamana.
Muro aliondoka mahakamani hapo saa 7:38 mchana akiwa kwenye gari aina ya Toyota RAV 4 lenye namba za usajili T607 ANM.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 10 mwaka huu.
Katika kesi hiyo Muro anatetewa na wakili Pascal Kamala

Thursday, February 04, 2010

Siku ya sheria duniani




RAIS Jakaya Kikwete amesema kuanzia mwaka ujao wa Fedha Mahakama itatengewa bajeti yake yenyewe, ili kuwa na uwezo wa kupanga na kutumia fedha yenyewe, bila kupitia Wizara ya Katiba na Sheria.

Rais Kikwete alitoa kauli hizo wakati akitoa salamu kwenye maadhimisho ya siku hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam, ikiwa ni ishara ya mahakama kuanza mwaka mpya wa shughuli zake.

“Kuanzia mwaka ujao wa fedha Mahakama itakuwa na bajeti yake ambapo itakuwa na uwezo wa kujipangia matumizi yake yenyewe bila kupitia wizara kama ilivyokuwa awali,” alisema Kikwete.

Hatua hiyo imekuja baada ya kilio cha muda mrefu cha mhimili huo ambapo pamoja na mambo mengine ulikuwa ukipendekeza kuwa na bajeti yao, mfuko wake na kuwa na mtendaji mkuu ambaye atakuwa anasimamia shughuli za kiutawala tofauti na ilivyo sasa.

“Kuanzia mwaka ujao wa fedha Mahakama itakuwa na bajeti yake ambapo itakuwa na uwezo wa kujipangia matumizi yake yenyewe bila kupitia wizara kama ilivyokuwa awali,” alisema Kikwete.

Awali mhimili mwengine wa dola ambao ni Bunge nao kwa muda mrefu walitoa kilio chao kwa serikali wakiomba watengewe bajeti yao kisheria jambo ambalo limefanikiwa na sasa mhimili huo umekuwa ukitengewa sehemu ya bajeti yake na kuwa na mtendaji mkuu ambaye ni Katibu Mkuu wa Bunge.

Kauli hizo za Rais zimekuja wakati ambapo kumekuwepo na kilio cha muda mrefu katika mhimili huo kutaka itengewe asilimia fulani kutoka kwenye baejti ya serikali kama ilivyo kwa mhimili mwingine wa dola (Bunge) ambalo hutengewa asilimia mbili ya bajeti ya serikali.

Kauli hiyo ya Kikwete ilitanguliwa na mapendekezo mbalimbali yaliyotolewa na Jaji Mkuu Agustino Ramadhani pamoja na ya wadau wengine wa sekta ya sheria waliopata nafasi ya kuhutubia katika sherehe hiz akiwemo Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) Jaji Fredrick Werema na Rais wa Chama cha Wanasheria nchini (TLS) Dk. Fauz Twaib.

“Mliyosema yote nimeyasikia na wadau wote wanaohusika wako hapa Sisi tutayafanyia kazi. Tutaweka kipaumbele stahiki katika bajeti ili muweze kuboresha miundombinu na kuongeza ajira kwa mahakimu na watumishi wengine,” alisema Rais Kikwete na kuongeza;

“Kuanzia mwaka ujao wa fedha mahakama itakuwa na mfuko wake wa fedha wakati tukiendelea na mipango ya kuiwezesha kuwa na bajeti yake ili iwe huru katika kupanga na kutekeleza majukumu yake. Tayari tumeshafanya hivyo kwa Bunge”.

Mambo ya Pwani




Wafanyabiashara wa samaki katika eneo la Pwani ya bahari ya Hindi mkoani Mtwara wakichuuza samaki wao hivi karibuni. Picha zimepigwa na Mussa Mkama na Hidaya Kivatwa.

Bomu Latelekezwa na Kupagawisha Wakazi wa Msasani Jijini


Wananchi wakishangaa bomu hilo lililobebwa na askari wa JWTZ likipelekwa sehemu maalumu kwa ajili ya uchunguzi zaidi.


Jeshi la polisi kutoka kikosi cha usalama kwanza ambao walifika mapema kabisa kwa ajili ya kulinda usamala wa wananchi eneo hilo,huku wakiwasubiri wataalamu kutoka jeshi la wananchi Tanzania JWTZ kwa ajili ya kulifanyia uchunguzi zaidi.

Bomu lililotelekezwa likiwa nje ya ukuta wa mkazi mmoja wa msasani bonde la mpunga mapema jana.
------------

Wakazi wa Msasani Bonde la Mpunga eneo la Maandazi Road jijini Dar es Salaam,jana walikumbwa na hofu baada ya mtu asiyejulikana kutelekeza bomu kwenye kichochoro kimoja mtaani hapo.Afisa Mtendaji wa Mtaa huo Bi. Rose Temu, alisema kijana mmoja alionekana mtaani hapo akitafuta mtu wa kumuuzia bomu hilo kama chuma chakavu lakini wanunuzi walionesha wasiwasi kuwa huenda ni bomu ndipo kijana huyo aliamua kulitelekeza mtaani hapo.Kufuatia tukio hilo kikosi cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania,kikosi maalum cha kutegua mabomu, kilifika eneo la tukio na kuthibitisha kuwa ni bomu hatari na kulichukua na kuondoka nalo. Picha kwa msaada mkubwa wa Ahmed Michuzi

Jeshi si mchezo


Mkuu wa kikosi cha JKT Mlale Meja Ahmed Ahmed akimtambulisha mkuu wa gwaride la wahitimu wa mafunzo ya awali ya kijeshi operesheni kilimo kwanza Meja Ally Aniu kwa mkuu wa mkoa wa Ruvuma Dk Christine Ishengoma mara baada ya kumaliza kukagua gwaride hilo jana chini ni wahitimu wa mafunzo hayo. Imeandikwa na Joyce Joliga.

Tuesday, February 02, 2010

Breaking newzzz Watu 24 wafa ajalini Tanga

WATU 24 akiwamo dereva wa basi wamekufa papo hapo na wengine zaidi 30 kujeruhiwa baada ya mabasi mawili kugongana uso kwa uso katika ajali ilyotokea Kijiji cha Kitumbi Wilayani hapa katika barabara kuu ya Segera - Chalinze.

Kwa mujibu wa habari za awali zilizopatikana na kuthibitishwa na maafisa wa polisi waliokuwepo katika eneo la ajali ni kuwa ajali hiyo ilitokea jana saa 8.50 mchana.

Walioshuhudia ajali hiyo muda mfupi uliopita walisema kuwa ajali hiyo ilihusisha basi la Kampuni ya Chatco iliyokuwa ikitokea Arusha kuelekea Jijini Dar es saalam lililovaana uso kwa uso na basi la Kampuni ya Mzuri Transport ambalo lilikuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Lushoto Mkoa wa Tanga na kwamba walishuhudia maiti nyingi zikiwa zimebebwa ndani ya lori.

Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar yakutana leo


Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Aman Abeid Karume, akifunguwa mkoba kutowa kabrasha kwa ajili ya kufunguwa Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar kilichokutana leo katika Ukumbi wa CCM Kisiwandui mjini Zanzibar. Kushoto ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein. Photos by Amour Nassor (VPO)

Wajumbe wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar Dk. Mohamed Gharib Bilal kushoto na Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Pandu Ameir Kificho kulia, wakijadiliana jambo wakati wa kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar kilichokutana leo katika ukumbi wa CCM Kisiwandui mjini Zanzibar.

Wajumbe wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar kupitia Umoja wa Vijana wa CCM Adila Hilal Vuai kushoto na Hawa Said Sukwa kulia, wakijadiliana jambo katika kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar kinachokutana leo katika Ukumbi wa CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar.

president Kikwete in Addis Ababa for 14th AU summit


President Jakaya Mrisho Kikwete in conversation with Gabon President Ali Ben Omar Bongo in Addis Ababa during the on-going 14th AU summit of Heads of State. Photos by Freddy Maro.

President Jakaya Mrisho Kikwete with FAO Director General Jaques Diouf at the United Nations Economic Commission for Africa Conference Centre (UNECA) in Addis Abeba Ethiopia Monday afternoon.

President Jakaya Mrisho Kikwete with the new African Union(AU) chairman President Bingu wa Mutharika during a luncheon he convened for African Leaders Malaria Alliance(ALMA) in Addis Ababa Ethiopia Monday afternoon.

Sunday, January 31, 2010

President Kikwete in Davos


President Jakaya Mrisho Kikwete(right) in conmversation with Vietnam Prime Minister Nguyen Tan Dung(centre) and the chariman of the New Delhi Television Roy Prannoy(left) who was also the moderator during the debate on Global Food Security held at Davos Congress Hall yesterday evening(photos by Freddy Maro)

President Jakaya Mrisho Kikwete in conversation with the the Microsoft founder and Chaiman of the Bill and Melinda Gates Foundation, Bill Gates shortly after participating in a debate on improving Food Security held in at Davos Congress Hall, yesterday afternoon.

President Jakaya Mrisho Kikwete speaks during a debate on improving agriculture production to boost food Security during the World Economic forum in Davos yesterday.On the left is Ellen Kullman Chair and CEO of of the US based DuPont company and on the right is Microsoft  Founder and Chairman Bill Gates.

mambo ya Kipanya

Jerry Muro matatani



HARAKATI za Mwanahabari Bora wa Jumla wa Mwaka 2009 Tanzania, Jerry Muro, za kupambana na kero ya rushwa na ufisadi jana zilimwingiza mwandishi huyo mikononi mwa jeshi la Polisi akituhumiwa kuomba na kupokea rushwa.

Muro, ambaye alikuwa mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha ITV na baadaye kuhamia kituo cha televisheni cha Taifa(TBC1), alikumbwa na mkasa huo leo majira ya saa sita mchana jijini Dar es Salaam katika hoteli ya Sea Cliff.


Akizungumzia suala hilo Kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema kuwa ni kweli mwandishi huyo amekamatwa na yuko polisi kwa mahojiano.

"Ni kweli yuko hapa na anahojiwa na mimi ndo ninapewa taarifa hivyo nitatoa taarifa kamili kesho saa sita,"alisema Kova.

"Kwa mujibu wa taarifa tulizozipata, Muro alikamatwa kufuatia mtego uliowekwa na askari polisi mara baada ya kuarifiwa na mfanyabiashara mmoja (jina tunalihifadhi) ambaye ndiye aliyetakiwa kutoa fedha hizo."

Bila kufafanua kwa undani sababu za Muro kutaka kupewa fedha hizo, taarifa zinadai kuwa Muro alikamatwa muda mfupi baada ya kukabidhiwa fedha hizo

“Muro alikuwa ameahidiana na mfanyabiashara ...., ili ampe Sh10milioni kama hongo, lakini mfanyabiashara huyo alitoa taarifa kwa Polisi na ndio leo (jana) wamefanikiwa kumkamata. Walimkamata mara baada ya kupokea fedha hizo,” alisema mtoa taarifa.

Mambo ya twanga







Twanga Pepeta wakiamua kufanya mambo wanafanya kweli hebu wacheki hapa, yaani hapatoshi wakiwa katika harakati zao kwenye ukumbi wakifanya vitu vyao hakika mwenye kuburudika anaburudika si mchezo swali linabadi jeee hawa wasanii wanakipata kile wanachokitaka, wanachokifanya ndicho mnachokitaka, mbona hawa wasanii wa kiume wamevaa vizuri kuliko wa kike au ndo tusemeeeee kazi kwenu.