Sunday, July 19, 2009

Jua kupatwa keshokutwa


wataalamu wanatuambua jua litapatwa mnamo julai 22 mwaka huu ambapo kuna sehemu mbalimbali duniani watashuhudia kupatwa kamili kwa jua. wadau mlio maeneo hayo tunasibiri taswira. maeneo yanayotabiriwa kuwa na kupatwa kamili kwa jua ni India, Nepal, Bangladesh, Bhutan, Myanmar, China, Japan na juu ya Kiribati. Vile vile sehemu za Marshall islands katika bahari ya Pacific.
Sehemu zingine ni Surat, Varanasi, and Patna in India, Thimphu huko Bhutan, Chengdu, Chongqing, Wuhan, Hangzhou na Shanghai huko China. Nchi karibu zote za Kusini Mashariki mwa Asia na visiwa kibao vya bahari ya Pacific. Visiwa vya Iwo Jima Kaskazini ndiko inasemekana wataona kupatwa kwa jua kwa muda mrefu kuliko sehemu nyingine.

Giraffe Ocean View



Hii ni sehemu mojawapo ya ukarabati mkubwa unaoendelea hivi sasa pale kwenye hoteli ya kitalii ya Giraffe Ocean View.

Friday, July 17, 2009

Mdigrii



kwa waliowahi kusoma hapa mlimani nadhani watakuwa wanaufahamu vizuri mti huu maarufu kama MDIGRII. Chini ya mti huu vichwa vilikuwa vikiumia na mambo mengi wakati huo hakika nimeukumbuka mdigrii, hivi sasa ndivyo unavyoonekana mti huu kama ulivyokutwa na mdau wetu, zamani tulikuwa tukibeba viti baadaye vikajengwa vijiwe tulivyovifahamu kama VIMBWETE kutokana na umaarufu wa aliyeanzisha mpango wa mabadiliko ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Professa Tolly Mbwete ambaye wakati huo alikuwa kitivo cha Uhandisi sasa ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Rais Kibaki ndani ya Bongo


Rais Jakaya Kikwete akimkaribisha nchini Rais wa Kenya Mwai Kibaki kwa ziara ya kiserikali.

Rais Jakaya Kikwete akiwa na mgeni wake Rais Mwai Kibaki wa Kenya wakilakiwa na akinamama wakazi wa Dar es Salaam baada ya Rais Kibaki kuwasili katika uwanja wa Kimataifa wa ndege wa Julius Nyerere Dar es Salaam jana kwa ziara ya kiserikali.

Wednesday, July 15, 2009

Daftari la Kudumu la Wapiga kura

Rais wa Usalama Barabarani akiwa katika kituo cha kuandikisha wapiga kura skuli ya Wingwi kusimamia zoezi hilo la uandikishaji. Licha ya hali kuwa shwari, kuna askari wengi wa vikosi vya usalama na ulinzi katika maeneo ya vituo vya uandikishaji wakiwemo hata askari wa barabarani kama alivyoonekana huyu jana Julai.

Wazee wakiwa wamejipanga chini kusubiri zamu zao za kuandikishwa katika daftari la kudumu la wapiga kura kwenye kituo cha skuli ya Wingwi, wilaya ya Micheweni Pemba leo. Picha kutoka kwa salim said, Pemba

Tuesday, July 14, 2009

Gesi kuanza kutumika kwenye magari


Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja (wa pili kulia) akikata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mtambo wa kushindilia gesi asili uliofanyika leo huko Ubungo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo Ethur Mwakapugi na kushoto kwa waziri ni Meneja Mkuu wa PanAfrican Energy (T) Ltd Pierre Raillard.

Mfanyakazi wa PanAfrican Energy (T) LTD ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja akimuonyesha Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja (kushoto) jinsi ya kuweka gesi katika gari maalum wakati wa uzinduzi wa mtambo wa kushindilia gesi asili uliofanyika leo huko Ubungo jijini Dar es Salaam. Aliyesimama kulia kwa waziri ni Meneja Mkuu wa PanAfrican Energy (T) Ltd Pierre Raillard.

Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja (kulia) akimsikiliza mkazi wa Ubungo Maziwa ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja kuhusiana na maombi yao ya kulipwa fidia ili waweze kahama eneo hilo na kupisha ujenzi wa mitambo kupeleka gesi majumbani, kwenye taasisi na kwenye magari. Waziri Ngeleja alifika katika eneo hilo leo kwa ajili ya uzinduzi wa mtambo wa kushindilia gesi asili uliofanyika.

Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja (kushoto) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Yona Killagane wakati wa uzinduzi wa mtambo wa kushindilia gesi asili uliopo Ubungo jijini Dar es Salaam.Picha na Anna Nkinda - Maelezo

Msitu wa Nyumbanitu




Kijiji cha jadi cha Nyumba Nitu kilichopo Kata ya Mdandu Wilaya ya Njombe. Kijiji hiki ni muhimu sana kwa utalii na ni muhimu sana kwa utunzaji wa mimea na hifadhi ya mazingira.
Msitu huu ni wa maajabu sana kwani miti yake na mimea yake iko pale kwa karne nyingi na hata wanafunzi wetu wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine huenda pale kwa kujifunza aina za mimea.
Mbali ya msitu kuna kuku weusi wa ajabu na kuna mapango makubwa pale Nyumbanitu ambayo watu zaidi ya mia moja wanaweza kuishi kwenye mapango hayo yalikuwa yanatumika wakati wa vita. Maajabu hayo ni sawa kabisa kama yalivyo nchini Japan. Picha imepigwa na mdau Tumaini Msowoya aliyekuwapo ndani ya msitu huo kwa siku nzima amenieleza mambo mengi kuhusu msitu huu si mchezo.

Monday, July 13, 2009

Irene Uwoya mambo safiii



Hamad Ndikumata akitia saini shahada ya ndoa huku bibie Irene Uwoya akishuhudia kwa makini mkubwa

Mitaa ya Mbauda



Mambo ya Arusha hayo hebu cheki wakazi wa vitongoji vya Mbauda, Mianzini na Sanawari wakipata shule kuhusu namna ya kupanga uzazi iliyoandaliwa na Shirika lisilo la Kiserikali linalotoa Elimu ya Afya kwa jamii nchini (PSI-Tanzania), Shirika hilo la kimataifa kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii linaendesha programu ya matumizi ya uzazi wa mpango. Picha kwa hisani ya PSI.

Daftari la kudumu la wapiga kura


Akinamama wa Wingwi wasioona wakiwa katika hali ya kukata tamaa baada ya kufukuzwa kutoka kituo cha kuandikisha kura huko mitaa ya Wingwi baada ya kukosa vitambulisho vya Mzanzibari Mkazi. Picha ya Salim Said.

Friday, July 10, 2009

Kempinski nyingine yazinduliwa


President Jakayas Mrisho Kikwete and the owner of the Bilila Lodge Kempinski Mr.Ali Al Bwardy unveils the plaque to signal the official opening of the Bilila Lodge Kempinski in Serengeti this morning(picture by Freddy Maro)

President Jakaya Mrisho Kikwete delivers his speech during the official opening of the world class five star Bilila Lodge Kempinski located in Serengeti National park.The hotel can accomodate up to 160 guests in the 80 rooms.

Across section of the invited guests who particpitated in the ceremonies for the official opening of a five star Bilila lodge Kempinski in Serengeti,Mara Region this morning.

Morogoro leo




Mfanyabiashara wa kuuza machungwa katika Manispaa ya Morogoro akitayarisha machungwa kwa kumenya maganda huku mteja akirufuhaia kula tunda hilo katika eneo la uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Mchuuzi wa kuuza nguo za mitumba mjini Morogoro akifurahia jambo huku mteja wake wakati akichagua nguo hicho alizoweka katika beka jirani na stendi ya daladala mjini hapa. (Picha na Juma Mtanda.

Wednesday, July 08, 2009

Mtoto wa Michael Jackson aliza wengi


Mwili wa mfalme wa muziki wa Pop Michael Jackson ukiwa kwenye jeneza lenye kuta za dhahabu uliagwa na maelfu ya washabiki wake waliohudhuria kwenye ukumbi wa Staples Center wakati mamilioni ya washabiki wake wengi duniani walifuatilia tukio hilo kwenye luninga na internet. Picha za hafla ya kuuaga mwili wa Michael Jackson mwisho wa habari hii.
Akiongea kwa mara ya kwanza mbele ya halaiki ya watu, mtoto wa kike wa Michael Jackson , Paris, mwenye umri wa miaka 11 aliwaliza watu wengi pale alipopewa nafasi ya kuongea.

"Tangia nilipozaliwa, baba amekuwa ni baba bora ambaye hana mfano, ningependa kusema kwamba nampenda sana" alisema Paris na kuanza kuangua kilio huku akikumbatiwa na shangazi yake Janet Jackson.

Awali akiongea katika hafla hiyo ya kuuaga mwili wa Michael Jackson, mchungaji Al Sharpton aliwaambia watoto watatu wa Michael Jackson kuwa wasijali habari mbaya zinazosambazwa juu ya baba yao.

"Nataka watoto watatu wa Michael Jackson wajue kwamba baba yao alikuwa si mtu wa ajabu kama anavyoandikwa" alisema Sharpton na kuongeza "Vitu vya ajabu ni vile ambavyo baba yenu ilimbidi avikabili".

Safari ya Michael Jackson ilianzia kwenye nyumba ya kuhifadhia maiti ya Forest Lawn ambapo familia yake na ndugu zake walikusanyika kwa maombi na kulichukua jeneza lake tayari kwa safari ya kuelekea kwenye ukumbi wa Staples Center ambako watu 20,000 walikuwa wakisubiri.

Baada ya hapo jeneza la dhahabu la Michael Jackson lilipandishwa kwenye gari la kifahari huku helikopta 20 za waandishi wa habari zikifuatilia tukio kutoka angani.

Msafara wa magari mengi ya kifahari ulianza kuelekea kwenye ukumbi wa Staples Center ambako familia , marafiki na watu maarufu walijumuika na washabiki wa Michael Jackson ambao walibahatika kushinda bahati nasibu ya tiketi za kuhudhuria hafla hiyo.