Wednesday, March 07, 2012

CRDB Bank -Customer Information

Greetings.

Kindly note BOT has issued circular recently to commercial Banks, the circular requires clients to update particulars of their accounts.

The forms for updation of customers information can be found in CRDB Bank’s website under resources centre. The dully filled forms can be mailed in a scanned format to customer-hotline@crdbbank.com or send directly to respective branch before 14/03/2012.

I look foward to receiving maximum cooperation and timely filling of the forms.

NB; I have attached the Customer KYC Update Forms with this email and please you may share this information with other Tanzanians.

Regards,

Crispin S

RM-Tanzanite Account

President Kikwete presents Country Assesment Report to APRM team of experts


President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete presents the Tanzania Country Assessment Report to an APRM (Africa Peer Review Mechanism) Lead Panelist Barrister Mr. Akere Muna. during a function held at State House Gardens in Dar es Salaam, this morning. (photo by Freddy Maro).

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi(CCM) Nape Nnauye Akutana na Naibu Mkurugenzi wa Kitengo cha Masuala ya Afrika wa Uingereza

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimfafanulia jambo Balozi Msaidizi wa Uingereza Hapa nchini, Susie Kitchens wakati wa mazungumzo yake na Mkugenzi wa Kitengo cha Masuala ya Afrika wa Uingereza Nick Pyle (hayupo pichani) aliyemtembelea katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba mjini Dar es Salaam.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimkaribisha Naibu Mkurugenzi wa Kitengo cha Masuala ya Afrika wa Uingereza Nick Pyle aliyemtembelea katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba mjini Dar es Salaam. Kushoto ni Balozi Msaidizi wa Uingereza hapa nchini, Susie Kitchens
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na Naibu Mkurugenzi wa Kitengo cha Masuala ya Afrika wa Uingereza Nick Pyle (kushoto) aliyemtembelea katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba mjini Dar es Salaam. Katikati ni Balozi Msaidizi wa Uingereza hapa nchini, Susie Kitchens

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Mkurugenzi wa Kitengo cha Masuala ya Afrika wa Uingereza Nick Pyle (Wapili kushoto) baada ya mazungumzo yao leo, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba mjini Dar es Salaam. Kushoto ni Balozi Msaidizi wa Uingereza hapa nchini, Susie Kitchens

Sunday, February 26, 2012

Wana Tabora Boys wakutana Mbalamwezi Beach

Mwenyekiti wa Mkutano wa Wana Tabora Boys, Edwin Kidiffu wa kwanza kulia ambaye pia ni mwanasheria wa Ewura akimsikiliza kwa makini Makwinya aliyeinua mikono juu akifafanua jambo katika mkutano huo uliofanyika ufukwe wa Mbalamwezi, wanaomsikiliza ni Bina Katikiro mwenye fulana ya bluu


Mzee wa Mshitu akiwapo kwenye mjadala uliokuwa ukiendelea kwa baadhi ya wana Tabora Boys Secondary School waliopata kusoma katika shule hiyo kongwe na yenye sifa tele nchini walipokutana jioni ya jana katika ufukwe wa Mbalamwezi jijini Dar es Salaam, pamoja na mambo mengine ilikuwa ni kukutana, kutafakari na kujadili way forward ya wana Tabora School hao.

Braza Kamtande Sikalwanda (Mchawi wa hesabu) aliyeipandisha chati mno Sekondari ya Tabora enzi hizo (katikati) akijadili jambo na Braza Kipeya wakati wa mkutano huo wa wana Tabora Boys uliofanyika jana katika Ufukwe wa Mabamwezi. Anayewashuhudia kulia ni Danny Lyimo.

Makwinya naye alikuwapo, huyu jamaa enzi hizo akiwa Tabora Boys alikuwa mkoba wa kutumainiwa wa timu ya shule na hasa pale timu ilipoweza kuitandika timu ngumu ya Uyui Sekondari mabao mawili kwa bila jambo lililizua balaa. Hapa jamaa anapiga maji ya mende.


Dokta Mzee Gombo ambaye ni Specialist wa Meno Muhimbili enzi hizo alikuwa PC wa PCB kwa lugha rahisi alikuwa kiranja wa darasa la wakali wa kombinesheni ya PCB akiwa na akina Charles Sebastian na Rahim Mzee, kwa mbali waweza kumuona Second Chief George, ambaye sasa ni daktari wa magonjwa sugu.

Danny Lyimo akishuhudia wakati Makwinya akisalimiana na Luwaga Kizoka (Nyigu) , nyuma yake anaonekana Renasco Mbilinyi. Taarifa na picha zaidi za matukio hayo zitaletwa kwenu na timu ya Mzee wa Mshitu.

Wednesday, February 15, 2012

JK ashiriki ufyatuaji matofali Msoga





Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika hatua mbalimbali za kusaidia kufyatua matofali ya kisasa kwenye kambi ya mafunzo ya ujasiriamali na ujenzi kwa vijana 380 toka wilaya zote za Mkoa wa Pwani za Kibaha mjini Kibaha vijijini, Mafia, Kisarawe, Mkuranga na Rufiji.

Kambi hiyo ya mwezi mmoja iliyo katika kijiji cha Msoga, wilaya ya Bagamoyo, Mkoa wa Pwani, ni moja kati ya kambi kadhaa zinazoandaliwa mkoani humo, ambapo ikimalizika hii ya ujenzi mnamo february 29, itafuatia ya upandaji miti na mazingira itakayokuwa katika Chuo cha Elimu Kibaha. Baada ya Hapo itafuatiwa kambi ya ukulima wa mazao ya mbogamboga wilayani Rufiji.

Rais Kikwete ameusifu mkoa wa Pwani kwa kubuni kambi hizo na kutaka mikoa mingine iige mfano huo ili kuwapa vijana ujuzi wa kuweza kujiajiri wenyewe.

Ameahidi kuendelea kusaidi vikundi vya vijana vya aina hiyo ambavyo amevitaja kama hazina nzuri ya maendeleo na utatuzi wa vitendo wa tatizo la ajira.

Rais Kikwete ametoa mashine za kufyatulia matofali ya kisasa 76 ambapo kila moja kati ya vikundi 38 vilivyopo vitapewa mashine mbili mpya na waliyofanyia kazi wataondoka nayo na kuwa ya tatu. Pia Amewapa vijana hao mifuko 3800 ya saruji (kila kundi mifuko 100), viatu vigumu (gum boots) pamoja na mananasi toka shambani kwake.

PICHA NA HABARI NA IKULU


Monday, January 30, 2012

Jengo jipya la AU






Jengo jipya la Makao Makuu ya Umoja wa Afrika (AU) lililozinduliwa na Rais wa China, Bw Hu Jintao jijini Addis Ababa jana, Januari 29, 2012. Jengo hilo ambalo limegharimu mamilioni ya dola za Kimarekani, limejengwa kwa udhamini wa China. PICHA NA IKULU

Wednesday, November 30, 2011

JK awakubalia CUF kuonana naye sheria ya katiba

Ofisi ya Rais, Ikulu, imepokea barua kutoka Chama cha Wananchi (CUF) kikiomba kukutana na kufanya mazungumzo na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.

Mheshimiwa Rais amekubali ombi hilo la CUF na ameelekeza maandalizi ya mkutano huo yafanyike mara moja.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

Ikulu,

DAR ES SALAAM.

Monday, November 28, 2011

NMB yazindua Kituo cha Biashara Arusha

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mercy Sila, akizindua rasmi Kituo cha Biashara kwa wafanya biashara wadogo, wakati na wakubwa wa Benki ya NMB mkoani Arusha jana. Wengine wanaoshuhudia kutoka kushoto ni CEO wa NMB, Mark Wiessing, Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya NMB, Misheck Ngatunga na Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema. (Picha na Mpigapicha wetu).
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mercy Sila, akipeana mkono wa shukrani na CEO wa Benki ya NMB, Mark Wiessing (kulia) na Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya NMB, Misheck Ngatunga baada ya kuzindua rasmi Kituo cha Biashara kwa wafanya biashara wadogo, wakati na wakubwa wa Benki ya NMB mkoani Arusha jana. Kushoto ni Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema. (Picha na Mpigapicha wetu).
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mercy Sila, akifurahi baada ya kuzindua rasmi Kituo cha Biashara kwa wafanya biashara wadogo, wakati na wakubwa wa Benki ya NMB mkoani Arusha jana. Wengine wanaoshuhudia kutoka kulia ni CEO wa Benki ya NMB, Mark Wiessing, Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya NMB, Misheck Ngatunga na kushoto ni Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema. (Picha na Mpigapicha wetu)

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mercy Sila, akisoma kibao cha uzinduzi mara baada ya kuzindua rasmi Kituo cha Biashara kwa wafanya biashara wadogo, wakati na wakubwa wa Benki ya NMB mkoani Arusha jana. Wengine wanaoshuhudia kutoka kulia ni CEO wa Benki ya NMB, Mark Wiessing, Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya NMB, Misheck Ngatunga na kushoto ni Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema. (Picha na Mpigapicha wetu).

Tamasha la Str8t Music lafana Dar

Fabolous akifanya makamuzi
Sehemu ya nyomi iliyohudhuria
Sehemu ya nyomi iliyohudhuria
Naseeb Abdul ‘Diamond’ akiwajibika. Picha zote ni za Venance Nestory wa Mwananchi.

TAMASHA la Str8Muzik Festival Inter-College Special 2011 la vyuo kwa mwaka 2011 lililofanyika katika viwanja vya Leaders Club, Dar es Salaam, Jumamosi na kuhudhuriwa na maelfu ya watu, limefana vilivyo.

Kwa muda wa saa tano, tamasha hilo lilipambwa na nyota wa Hip Hop wa Marekani, Fabulous aliyewarusha vijana wa kike na kiume wanaopenda burudani kadri muda ulivyoyoyoma.

Kundi la kwanza kutumbuza kwenye tamasha hilo lilikuwa ni Alleluyah lililokuja na free-style, ambalo lilivumbuliwa katika tamasha kama hilo lililofanyika mwaka
jana.

Fabulous alipanda stejini saa nne na kufanya vitu vyake na kuimba ngoma 20 zinazopendwa na mashabiki.

Baadaye ndipo ukaja wakati wa wanamuziki nguli wa Bongo Fleva waliopanda jukwaani kuanza na kundi la Manzese Crew, Inspekta Haroun, Amani Temba 'Mheshimiwa Temba' na Chege nao walikamua kwa ngoma zao.

Elius Barnaba alikuja akiwa na kundi lake la THT
pia Mfalme wa Rhyme, Afande Sele alipata wasaa wake wa kupiga shoo akifuatiwa na Pina wa Kikosi cha Mizinga alikamua ngoma mbalimbali pamoja na ngoma yake ya Umoja ni Nguvu na kuungwa mkono na wapenzi wa muziki waliokuwa wanamshangilia na kudhihirisha kuwa rapu si tu kwa Fabolous, bali hata kwa Wabongo.

Nao wana-Hip Hop kutoka Arusha Nako 2 Nako waliruka stejini na baadaye kupigwa tafu na wakali Jo Makini na Niki wa Pili.

Usiku huo ulipambwa pia na MwanaFa, Shetta,Diamond Platinum, Big Boy Baghad, Juma Nature, Mchizi Mox na Jay Mo walikamua
na kuwapagawisha wapenzi na sauti zao.

Tamasha la StrMuzik lilianzishwa mwaka 2005 na baadaye lilijulikana kama Inter-College Bash, na kufanyika Dar es Salaam na mwaka 2008 lilifika
hadi Mwanza, Morogoro na Dodoma.

Sugu afanya vitu vyake viwanja vya Ustawi wa Jamii


Mr II akiwa jukwaani na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika. Wabunge takribani wanane walisindikiza uzinduzi wake huo ulioenda sambamba na uzinduzi wa kitabu kinachoeleza historia yake katika maendelea ya muziki wa Rap Bongo.
Msanii Mr II Sugu akifanya vitu vyake usiku wa kuamkia jana kwenye viwanja vya Ustawi wa Jamii
Mheshimiwa Mbunge Joseph akiwa anachana mistari jukwaani usiku wa kuamkia jana, nyomi ilikuwa ya kutisha
**********************************

Boniface Meena

MKALI wa muziki wa Hiphop nchini, Joseph Mbilinyi maarufu kama 'Sugu' usiku wa kuamkia jana akisindikizwa jukwaani na wabunge kadhaa, aliteka nyoyo za maelfu wa mashabiki wa sanaa ya muziki waliofurika kushuhudia uzinduzi wa albamu yake mpya iliyopewa jina la 'Anti Virus' kwenye viwanja vya Chuo cha Ustawi wa Jamii, Jijini Dar es Salaam.
Sugu ambaye pia ni mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), alifunika tamasha hilo kwa kuimba nyimbo zake za zilizowateka kimawazo mashabiki wake wengi vijana.
Kivutio kikubwa kwenye onyesho hilo, alikuwa mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, ambaye alipanda jukwaani na kuwasalimia mashabiki: "Oyoooo Oyoooo...nimefurahi kupanda jukwaani kucheza pamoja nanyi."
Katika onyesho hilo lililopambwa na burudani kutoka vikundi mbalimbali vya muziki wa kizazi cha wakati huu (Bongo Fleva), Sugu pia aliimba na kucheza sambamba na wabunge wenzake kama John Mnyika, Joyce Mukya na Regia Mtema na Highness Samson.
"Oyoooo...Oyoooo. Nawashukuruni sana kwa kutuunga mkono, leo nauweka pembeni uheshimiwa na kushusha mawe. Pigeni kelele mpaka walioko Leaders Club wasikie," alisema Sugu.
Baada ya salamu hizo, alianza kwa kuimba wimbo wa 'Sugu Moto Chini' ambao uliwaamsha mashabiki kwa furaha, kisha akachombeza mashairi kadhaa ya wimbo 'Yamenikuta' na kupiga wimbo mwingine 'Kiburi' aliomshirikisha Stara Thomas.
Hakuishia hapo, akaimba wimbo mwingine 'Mambo ya Fedha', 'hayakuwa mapenzi' na mwisho akateremsha wimbo wenye jina la 'Sugu' ambao uliwapa utumwa wa kushangilia bila kuchoka mashabiki wake.
Kabla ya kushuka jukwaani Sugu alisema yuko mbioni kufanya wimbo na kumshirikisha mwenyekiti wake Mbowe.
Katika uzinduzi huo Sugu alisindikizwa na wasanii kama Danny Msimamo, Mabaga Fresh, Adili na Soggy Doggy Hunter, Mgosi Mkoloni, Mapacha, Suma G, Zay B na wengine wengi.

Sunday, November 27, 2011

JK akutana na Chadema

Rais Jakaya Kikwete, akimkaribisha mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, Ikulu jijini Dar es salaam muda mfupi uliopita leo. (picha: K-VIS blog)


Ujumbe wa CHADEMA ukijongea lango la Ikulu

Rais Kikwete anakabidhiwa kabrasha la mapendekezo

Picha ya pamoja ya viongozi wa pande zote mbili
Mbowe na JK

RAIS Jakaya Kikwete jana alikutana na ujumbe wa Chadema kukabidhiwa kabrasha la mapendekezo yao na kujadili mchakato wa utungwaji wa Katiba mpya.

Rais alikutana na viongozi hao majira ya saa tisa na nusu alasiri mpaka saa 12 jioni na kukabidhiwa kabrasha la maoni ya viongozi hao kabla ya viongozi hao walioongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe, kupiga picha za pamoja na Rais wakiwa ndani na baadaye nje ya jengo la Ikulu na hatimaye kuendelea na majadiliano.

Mbowe alilieleza Mwananchi kwamba kikao chao hicho cha majadiliano kilidumu kwa saa tatu na kiliahirishwa saa 12 jioni na kitaendelea kesho asubuhi saa nne.

"Ndugu waandishi wa habari tumekutana na Rais na baadhi ya mawaziri na Wasaidizi wake! Kikao kilianza saa 9:30 mchana na kiliahirishwa saa 12 jioni. Kikao kitaendelea kesho asubuhi saa nne. Taarifa kamili ni baada ya kikao,"alieleza Mbowe katika ujumbe wake kwa vyombo vya habari.

Mbowe aliongozana na wajumbe wa kamati hiyo Makamu Mwenyekiti wa Chadema (Bara) Said Arfi na Makamu Mwenyekiti (Zanzibar) Said Issa Mohamed, Mshauri wa Masuala ya Siasa wa chama hicho, Profesa Mwesiga Baregu, Profesa Abdallah Safari na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani bungeni, Tundu Lisu, ambaye alikuwa Katibu wa Kamati hiyo wakati wa mkutano huo na John Mrema. Katibu Mkuu Dk Willibrod Slaa ambaye ni mjumbe hakuwapo.