Showing posts with label Msiba. Show all posts
Showing posts with label Msiba. Show all posts

Tuesday, October 22, 2013

Marehemu Julius Nyaisangah aagwa Leaders, Makamu wa Rais aongoza shughuli


Sehemu ya waombolezaji waliojitokeza kumuaga marehemu Nyaisanga, katika Viwanja vya Leaders Club.Picha Zote na Ofisi ya Makamu wa Rais

Godwin Gongwe na Ruge Mutahaba waliokaa katikati

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lenye mwili wa aliyewahi kuwa mtangazaji wa Redio Tanzania, ITV na Redio One na Redio Aboud, marehemu Julius Nyaisanga, aliyefariki dunia mwishoni mwa wiki iliyopita huko mjini Morogoro kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu. Marehemu Nyaisanya ameagwa leo katika viwanja vya Leaders Club Kinondoni na anasafirishwa leo hii kuelekea Tarime kwa ajili ya maziko.



Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi akisalimiana na Makamu wa Rais Dk. Gharib Bilal
Menyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP  Dkt. Reginald Mengi, akizungumza machache....

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda (kulia) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Chadema na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe, wakati wa shughuli hiyo Viwanja vya Leaders.

Leah Nyaisanga, ambaye ni mke wa marehemu wa aliyewahi kuwa mtangazaji wa Redio Tanzania, ITV na Redio One na Redio Aboud, marehemu Julius Nyaisanga, akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu mumewe, aliyefariki dunia mwishoni mwa wiki iliyopita huko mjini Morogoro kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa shinikizo la damu, wakati wa shughuli za kuagwa mwili huo zilizofanyika kwenye viwanja vya Leaders Club Kinondoni na anasafirishwa leo hii kuelekea Tarime kwa ajili ya maziko.

  



Msafara wa Magari ambao moja wapo (la mbele) likiwa limebeba jeneza lenye mwili wa marehemu Julius Nyaisanga ukiingia kwenye viwanja vya leaders muda huu kwaajili ya wakazi wa jiji la Dar kuweza kutoa heshima zao za mwisho kwa Mwili wa Marehemu Julius Nyaisanga kabla ya Kusafirisha Kwao Tarime Mkoani Mara




Baadhi ya Ndugu, Jamaa na marafiki wakibeba jeneza lenye Mwili wa Marehemu Julius Nyaisanga Kwaajili ya kupeleka sehemu husika tayari kwa kutoa heshima za mwisho kwa wakazi wa jiji la Dar waliofika katika viwanja vya leaders muda huu

Sehemu Jeneza lenye Mwili wa Marehemu Julius Nyaisanga litakapowekwa kwaajili ya wakazi wa jiji la dar kuweza kutoa heshima zao za mwisho kabla ya kusafirishwa kwenda Tarime Mkoani Mara.

Baadhi ya wakazi wa jiji la dar waliojitokeza katika viwanja vya leaders muda huu



Baadhi ya Wakazi wa Jiji la Dar wakisubiria Kutoa Heshima zao za Mwisho kwa Mwili wa Marehemu Julius Nyaisanga Kabla haujasafirishwa kupelekwa Kwao Tarime Mkoani Mara.

Thursday, December 18, 2008

Herry Makange afariki dunia




HAYATI HERRY MAKANGE

Habari tza kusikitisha tulizozipoke hivi punde kutoka kwa issamichuzi.blogspot.com zinasema kuwa HERRY MAKANGE, MPIGANAJI WA CHANNEL TEN NA DTV, HATUNAYE TENA BAADA YA KUFARIKI KATIKA AJALI HAPA DAR JANA MCHANA.

HABARI ZILIZOPATIKANA JANA USIKU NA KUTHIBITISHWA ASUBUHI HII NI KWAMBA HERRY ALIKUTWA NA MAUTI AKIELEKEA MJINI KUTOKEA KAWO KIBAHA AKIWA ANAENDESHA PIKIPIKI. ALIKUWA NDIO KWANZA AMEREJEA TOKA TABORA KIKAZI NA ALIKUWA AKIENDA KURIPOTI KAZINI.
IKUMBUKWE KWAMBA HERRY ALIKUWA MMOJA WA WAPIGANAJI WALIONUSURIKA KATIKA AJALI YA GARI HUKO KIBITI ILIYOMHUSISHA PIA MPIGANAJI ATHUMANI HAMISI AMBAYE HADI LEO YUKO SAUZI AKITIBIWA SHINGO NA MGONGO. KURASA YA AJALI HIYO YA KIBITI BOFYA HAPA
TUTAENDELEA KUFAHAMISHANA KILA KINACHOJIRI BAADAYE IKIWA NI OAMOJA NA MIPANGO YA MAZISHI.
MUNGU AILAZE ROHO YA MPIGANAJI MWENZETU MAHALI PEMA PEPONI
-AMINA

Wednesday, August 20, 2008

Rais Mwanawasa afariki kweli


RAIS wa Zambia Levy Mwanawasa (59), amefariki dunia nchini Ufaransa ambako amekuwa akipatiwa matibabu baada ya kupata mstuko.
Kifo cha Mwanawasa ambaye ni kipenzi cha nchi za Magharibi kutokana na msimamo wake katika mapambano dhidi ya ufisadi, kimetokea miezi takriban miwili baada ya kuzushiwa kifo.
Makamu wa Rais wa Zambia, Rupia Banda, amenukuliwa na Shirika la Habari la Uingereza (Reuters) akithibitisha kutokea kwa kifo cha Rais Mwanawasa.
Banda alifafanua kwamba kutokana na kifo hicho cha Rais Mwanawasa, nchi itakuwa katika maombelezo ya siku saba za msiba huo mzito.
Mwanawasa pia atakumbukwa kutokana na msimamo wake wa kuwa mmoja wa viongozi wa Afrika wanaomkosoa Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, kutokana na matendo yake ya ukiukaji demokrasia na utawala bora.
"Ndugu zangu wananchi, kwa majonzi na masikitiko makubwa napenda kuarifu watu wa Zambia kwamba, Rais wetu Dk Levy Patrick Mwanawasa, amefariki leo asubuhi (jana)," alisema Makamu wa Rais Banda kupitia televisheni ya taifa ya nchi hiyo na kuongeza:
"Pia ningependa kuarifu kwamba, maombelezo ya kitaifa ya kifo cha Rais yatafanyika kwa muda wa siku saba."
Kwa mujibu wa Katiba ya Zambia, Banda ndiye ambaye anatarajiwa kukaimu madaraka hayo ya Rais hadi utakapoitishwa uchaguzi.
Mwanawasa aliweza kujijengea heshima miongoni mwa Wazambia, baada ya kuwezesha utajiri wa madini ya shaba kunufaisha raia wake wengi.
Pia anaheshimiwa na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na nchi fadhili za Magharibi, ambazo ziliamua kuongeza msaada wa mabilioni ya dola kwa nchi hiyo ya Kusini mwa Afrika.
Uamuzi wa IMF na nchi fadhili za Magharibi kuongeza msaada kwa Zambia, unatokana na juhudi nzito za Mwanawasa katika kuendesha kampeni nzito dhidi ya ufisadi, ikiwa ni za kwanza tangu nchi hiyo ipate uhuru mwaka 1964 kutoka kwa Waingereza.
Miongoni mwa watu waliokumbwa na operesheni hiyo ya ufisadi, ni Rais aliyemrithi Frederick Chiluba.
Hivi karibuni, baada ya kutokea hali ya tete ya nchini Zimbawe baada ya kuvurugika kwa duru ya kwanza ya uchaguzi, Mwanawasa alimshutumu Mugabe akisema anataka kuleta balaa jingine la machafuko barani Afrika.

Historia fupi ya Mwawasa

Mwanawasa alizaliwa Mufurira, eneo la Ukanda wa Shaba, Septemba 3,1948 na kuanza kuibuka katika siasa wakati akiwa Makamu wa Rais wa Chama cha Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Zambia, ambacho kilifanya maandamano kadhaa kuunga mkono harakati za ukombozi wa nchi ya Afrika Kusini.
Baada ya kuhitimu chuo mwaka 1973, taratibu Mwanawasa alianza kujiimarisha kama mwanasheria anayeshimika katika kipindi cha miaka 20 iliyofuata.
Katika moja ya kesi maarufu, alifanikiwa kumtetea makamu wa zamani wa rais, Christon Tembo na wenzake walioshtakiwa kwa makosa ya uhaini mwaka 1989, akiwa amewaokoa katika hukumu ya kifo kama wangepatikana na hatia.
Akiwa mmoja wa waasisi wa chama cha Movement for Multi- Party Democracy (MMD), Mwanawasa alimsaidia Frederick Chiluba kumshinda Rais Kenneth Kaunda katika uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi nchini Zambia mwaka 1991.
Mwishoni mwa miaka ya 1991 aliteuliwa kuwa Makamu wa Rais wa Zambia, lakini akajiuzulu miaka mitatu baadaye kutokana na kushindwa kuvumilia matumizi mabaya ya ofisi na rushwa iliyokuwa imekithiri wakati wa utawala wa Chiluba.
Wakati akiendelea kuwa mwanachama wa MMD, Mwanawasa aliendelea na shughuli zake kwenye jumuiya ya wanasheria hadi mwaka 2001.
Mwanawasa alinusurika katika ajali ya gari Desemba mwaka 1991 na akalazwa hospitalini kwa miezi mitatu. Ajali hiyo mbaya ilimfanya atembee kwa kuchechemea na kuzungumza kwa shida.
Baada ya kuitwa kurejea MMD kwa kutumia vikao vya pembeni na Chiluba, Mwanawasa aligombea urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2001.
Kwa mshangao wa kila mtu, Mwanawasa alikorofishana na Chiluba mara baada ya kuapishwa na akaanza kampeni ya kusafisha rushwa, kampeni ambayo ilidaiwa kuwa ya kutafuta mchawi dhidi ya serikali ya zamani.
Mwezi Aprili, 2006, Mwanawasa alikumbwa na kiharusi, lakini akapona mapema baada ya kutibiwa nchini Uingereza.
Miezi mitatu baadaye, alimshinda mpinzani wake wa kisiasa Michael Sata na kurejea madarakani kwa kipindi cha pili, akiwa ameshinda kwa kura chache.
Tofauti na aliyemtangulia, Mwanawasa alipata mafanikio makubwa katika maendeleo. Chini ya utawala wa Mwanawasa, Zambia imekuwa na maendeleo makubwa ya kiuchumi, huku wawekezaji wa nje wakiwekeza mabilioni ya fedha.
Mwanawasa alikuwa mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika mwaka 2007 na alisifiwa kwa juhudi zake zisizo na kikomo katika kujaribu kumaliza mgogoro wa kisiasa ulioibuka nchiniZimbabwe baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Machi 2008.
Mwanawasa ameacha mke Maureen Luchendo Mwanawasa na watoto sita.
- Reuters

Friday, August 01, 2008

Hatimaye Chacha Wangwe azikwa



ALIYEKUWA Mbunge wa Tarime (Chadema), Chacha Wangwe amezikwa jana kwenye makaburi ya kijijini kwao Kimakorere baada ya familia kuridhika na uchunguzi wao uliofanyika na daktari wao.

Wangwe alizikwa jana majira ya saa 12 jioni huku kukiwa na hali tata, wakati baadhi ya ndugu wakigoma na wengine kukubali.

Mazishi hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na vyama vya siasa nchini ambao pia walikuwapo katika uchunguzi uliofanyika kabla.

Akizungumza kabla ya mazishi kwa niaba ya familia muda mfupi baada ya kutoka ndani ya chumba cha uchunguzi, Prof Samwel Wangwe alisema jana kuwa uchunguzi walioutaka familia umekamilika na kwamba sasa wameridhika kuwa mbunge huyo alikufa kwa ajali na si vinginevyo. Habari ya Fredrick Katulanda.

Kapteni Mazula afariki dunia


Rubani mkuu wa atc kepteni george mazula amefariki dunia nyumbani kwake mtaa wa nyumbu, mikocheni, dar leo asubuhi baada ya kusumbuliwa na matatizo ya kupumua.

msemaji wa familia, dk. charles lugora, amesema kwamba marehemu kepteni mazula alikuwa nchini india kiasi cha wiki tatu zilizopita alikokwenda kupatiwa matibabu ya athma na ali;porejea alikuwa anaendelea vyema hadi hali ilipobadilika ghafla asubuhi ya leo ambapo alifariki dunia milango ya saa nne unusu asubuhi.

Dr. Lugora amesema mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwake na ratiba kamili itatolewa kesho.

marehemu mazula aliyefariki akiwa na umri wa miaka 59, ameacha mke na watoto wawili (brian na george). mtoto wake wa tatu, walter, aliuwawa huko marekani septemba 2006, ambapo yeye na mchumba wake vonetha nkya waliuwawa kikatili na watu wasiojulikana.

mola aiweke roho ya marehemu pahala pema peponi,

Msiba wa Wangwe noma

Jamaa wako na mabango wakielezea hisia zao.
Panoja na kuwapo kwa polisi lakini vijana wanaleta vurugu nyingi kiasi kwamba tumepata taarifa kuwa kuna wengine wanaletwa kw amagari nadhani sasa siasa inakolea msibani!!!!!

Wednesday, July 30, 2008

gari lililomuua Wangwe

Chacha enzi za uhai wake baada yakunyoa rasta



Gari lililohitimisha maisha ya Chacha Wangwe Mbunge wa Tarime anayetarajiwa kuzikwa kesho likiwa limeharibika vibaya, aisee maswali sasa yapo kibao, jamaa wanadai kuwa kauawa sababu hakuwa akiendesha yeye, kalikuwa kakiendesha kaijana kanakoitwa Mallya ambako ni kanajeshi kalikohitimu huko Libya. Picha za Faraja Tranquilino wa Dodoma.

Wednesday, June 11, 2008

MAwaziri wafa ajalini

Lorna Laboso1961 — 2008.
Kipkalya Kones: 1952 — 2008.

Ms Aurelia Langat, a sister-in-law of Assistant minister Lorna Laboso overcome by grief on receiving the news of her death

Prime Minister Raila Odinga consoles the family of Roads Minister Kipkalya Kones at their home in Nairobi, on Tues


NDEGE ndogo ya abiria aina ya Cessna 210 imeanguka nchini Kenya na kusababisha vifo vya watu wanne, akiwemo Waziri wa Barabara Kipkalya Kones na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Lorna Laboso.

Ajali hiyo ambayo ilitokea kilomita 120 (maili 75), Magharibi mwa jiji la Nairobi pia imesababisha kifo cha Ofisa wa Polisi, Kenneth Bett na Rubani Schner Christopher.

Vifo vya mawaziri hao kutoka Chama cha Orange Democratic Movement (ODM), vimefanya hadi sasa chama hicho kupoteza wabunge wanne tangu kufanyika Uchaguzi Mkuu wa Desemba mwaka jana ambao ulifuatiwa na ghasia kabla ya mkataba wa amani kusainiwa Februari 28 mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka gazeti la Daily Nation na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) na Shirika la Habari la Uingereza (Reuters), ndege hiyo iliyokuwa na namba 5Y BVE ilianguka katika Wilaya ya Narok.

Taarifa kutoka gazeti la Daily Nation ambazo zilinukuuu duru za vyombo vya usalama nchini humo, zilisema ndege hiyo ilikuwa ikienda Kericho ndipo ajali ilipotokea mnamo saa 9 alasiri jana. Hebu soma cheki East Africa Standard

Friday, May 23, 2008

Mazishi Rasmi ya Daudi

Daudi Timothy Said Ballali
Viewing: PrivateService: May 23, 2008 @ 10AM
Location: St. Stephen The Martyr
Daudi Timothy Said Ballali On May 16, 2008 of Washington, D.C.
Husband of Anna Ballali
Mass of Christian Burial will be offered on May 23, 2008 at 10AM at St. Stephen,Washington, D.C.Interment Gate of Heaven Cemetery
View the guest book for Daudi Timothy Said BallaliSign the guest bookhttp://www.devolfuneralhome.com/index.asp?sid=6&formid=102&serviceid=960
R.I.P
*Courtesy-Chemi-Chemponda

Wednesday, May 21, 2008

Balali kafariki dunia




MAMBO ni ya ajabu ajabu kuhusiana na taarifa za Dk Daud Balali, wengine wanasema Mzee Daudi Balali (pichani) amefariki, wengine wanasema amejificha Boston au Washington D.C. huko Marekani!

Kuna habari iliyotoka jana kwenye African Baraza kuwa Mzee Balali anasakwa na wapepelezi kuhusiana na wizi wa dola $133 milioni kutoka Benki Kuu ya Tanzania.

Wakati huo huo imethibitishwa hapa Bongo kwa Balali, amefariki dunia.Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Patrick Mombo, alithibitisha kifo hicho baada ya kupata taarifa rasmi kutoka Balozi wa Tanzania Ombeni Sefue.

Balozi Mombo aliliambia gazeti hili jijini Dar es Salaam kwamba, Balozi Sefue alipata taarifa hizo juzi saa 4:00 usiku kwa saa za Marekani.kwa taarifa zaidi soma mwananchi kesho.

Wednesday, April 23, 2008

Kwaheri Ditopile





Kikwete aongoza mazishi ya Ditopile

RAIS Jakaya Kikwete jana aliongoza mamia ya waombolezaji katika mazishi ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Marehemu Ukiwaona Ditopile Mzuzuri (60) yaliyofanyika kwenye makaburi ya familia yao huko Kinyerezi, jijini Dar es Salaam.

Marehemu Ditopile alifariki dunia ghafla Aprili 20 katika Hoteli ya Hilux, iliyopo mkoani Morogoro mwishoni mwa wiki iliyopita.

Akimwelezea marehemu, msemaji wa famili ambaye ni mdogo wa marehemu, Abdallah Ramadhani Ditopile alisema kaka alikuwa ni nguzo ya familia yao kwa kipindi chote cha uhai wake hivyo kifo chake kimeacha pengo kubwa lisiloweza kuzibwa.

Akitoa salamu za Chama Cha Mapinduzi (CCM), Katibu wa chama hicho ambaye pia ni Waziri wa Michezo na Utamaduni, Kapteni George Mkuchika alisema mbali na kumfahamu marehemu wakiwa shuleni, alimfahamu zaidi kutokana na uadilifu wake kazini katika nyadhifa mbalimbali alizoshika.

Katika uhai wake, Ditopile aliwahi kuwa mbunge wa Ilala kwa miaka 10, Katibu Mwenezi wa CCM, Mkuu wa Mkoa Dar es salaam, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mkuu wa Mkoa Pwani, Naibu wa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mkuu wa Mkoa wa Lindi na Mkuu wa Mkoa wa Tabora.

Wakati wa dua ya kumuombea marehemu inasomwa nyumbani kwake, viongozi mbalimbali wa serikali walihudhuria wakiongozwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda pamoja na Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete.

Hata hivyo, msiba huo ulitawaliwa na utani wa hapa na pale kati ya kabila la Wandengereko ambalo ni kabila la marehemu na kabila la Wanyamwezi na wasukuma ambao ni watani wa kabila hilo.

Katika hali hiyo ya utani, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya na aliyekuwa Waziri wa Miundombinu Andrew Chenge waliombwa kwenda kula chakula cha watani ulioandaliwa kwa niaba yao msibani.

Baada ya hapo mwili wa marehemu ulipeleka katika Msikiti wa Tambaza kwa ajili ya kumuombea kuswaliwa na ilipomalizika swala hilo, ulipelekwa hadi katika makaburi Kinyerezi kwa kupitia barabara ya Umoja wa Mataifa, Morogoro, Mandela na Tabata Segerea.

Wakiwa katika makaburi hayo, mamia ya waombolezaji waliongozwa na Rais Kikwete waliweka mchanga katika kaburi la marehemu. Pichani Rais Jikwete, Bilionea Chenge na waombelezaji wengine wakijumuika.

Sunday, April 20, 2008

Ditopile afariki dunia

Hii ya Braza Dito ilipigwa sioku nyingi zilizopita na Faza Kidevu.

Taarifa zilizotufikia hivi sasa zinasema kuwa Mwanasiasa machachari Ukiwaona Ramadhani Mwishehe Ditopile Mzuzuri amefariki dunia huko Morogoro akiwa anaangalia Televisheni katika hoteli akisumbuliwa na maradhi ya kisukari pichani mwili wa aliyekuwa mkuu wa mkoa wa tabora,Ditopile Mzuzuri ukipakiwa katika gari tayari kupelekwa katika chumba cha kuifadhia maiti cha hospitali ya mkoa wa Morogoro. Picha na Juma Ahmedi, Morogoro) taarifa zaidi mtaendelea kuzipata kadri tunavyozipata.

Sunday, April 06, 2008

Mwandishi Mkongwe afariki dunia



Marehemu John Mndolwa

MWANDISHI Mwandamizi na Mratibu waHabari na Matukio wa televisheni yaITV na Radio One, John Mndolwa (46),amefariki dunia leo alfajiri majira ya saa 10 baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Kwa mujibu wa habari zilizotolewa naMkurugenzi Mtendaji wa ITV na Radio One, Joyce Mhaville, marehemu Mndolwa alilazwa hospitali ya Kairuki kwa wiki moja. Kifo chake kimesababishwa na shinikizo la damu.

Mndolwa ambaye alizaliwa Novemba 9,1962 mkoani Tanga alianza kazi za uandishi mwaka 1980 katika Idara ya Habari ya Radio Tanzania (RTD) na aliajiriwa na ITV na Radio One Julai 1994.
Mipango ya mazishi inaendelea kufanyika. soma zaidi habari hii ya kuhuzunisha kwa kwenda lukwangule.blogspot.com

Mungu ailaze mahala pema roho ya marehemu - AMINA/AMEN

Saturday, January 26, 2008

Msiba huko Houston, Texas


Wananchi,
On behalf of the family and Tanzanians living in Houston, I sadly announce the death of our brother Felix Chambi (aka Felix Makene) pictured above.

Felix passed away on Thursday morning (24/1/08) after having a stroke on Monday night (21/1/08). Felix leaves behind his wife Maryam and young son Baraka. Condolences can be offered to Felix’s family at their home on8618 Rose Garden, Houston, TX, 77083.

You can also call: Maryam (wife) on 832 865 3366 or 314 369 2338
Alfred (brother) on 314 584 9708
Mchuma (sister) on 314 489 3248
The community of Tanzanians living in Houston is making plans to transport Felix from Houston to Tanzania next week.

CONTRIBUTIONS:
As we all know, the costs of transporting Felix’s body from Houston to Tanzania will be high.We have estimated the total cost of this process to be $22,400. While any amount you donate will be greatly appreciated, we are recommending that Tanzanians living in Houston contribute around $100 each.
The Tanzanian Community in Houston will conduct a fund raiser on Saturday (1/26/08).
The fundraiser will begin at 4pm and will be held at:Safari Party Hall (Kwa Inno) 8951 Bissonnett, Houston TX 77036. Like always, men should bring drinks and women food to the fundraiser. Ladies can get in touch with Nuru Mazola and gentlemen with Alex Tibaigana for further information on our needs.

If all goes well, we plan to pay our last respects to Felix on Sunday (1/27/08).
You will receive more information on this as it becomesavailable.
If you have any questions please feel free to contact thepeople below.

BANK: Washington Mutual Bank

NAME: Jadi malumbo

ACCT #: 4213965100

ROUTING#: 111993776
BANK ADDRESS

10850 Bellaire BlvdHouston,

TX, 77072281.498.2233

Miraji Malewa 713 373 6525
Nuru Mazola 832 630 8090
Anita Massawe 832 721 3832
Rosemary Mlekwa 832 867 2140
Muddy Chamshama 713 203 4629
Jadi Malumbo 713 419 6803
Karim Faraji 713 702 9050

Monday, October 29, 2007

Safari ya mwisho ya Mbatia









Safari ya mwisho duniani ya Naibu waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Salome Mbatia ilivyohitimishwa katika makaburi ya Kanisa Katoliki Parokia ya Mbokomu na kuhudhuriwa na mamia ya waombolezaji. Picha kwa hisani ya ofisi ya Waziri Mkuu.

Friday, October 26, 2007

uwanjani Kilimanjaro

Kijana wa kiume wa mama mbatia akisindikizwa na baadhidhi ya Waombolezaji wakitoka katika uwanja wa KIA baada ya kuupokea mwili wa Salome Mbatia picha ya mdau Ally Sonda wa Moshi.

BILIONI 51 KUTUMIKA UJENZI WA BARABARA, MASOKO NA STENDI JIJINI ARUSHA

Mradi wa Uendelezaji wa Miji na Majiji Tanzania (TACTIC) unatekeleza miradi yenye thamani ya shilingi bilioni 51 katika Jiji la Arusha ikiwa...