Tuesday, December 29, 2015

Naibu Waziri, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Angelline Mabula astukizia Baraza la Ardhi Kinondoni


 Naibu Waziri, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Angelline Mabula (Mb), akiangalia mafaili ya kesi mbalimbali katika Baraza la Ardhi na Nyumba la Kinondoni, jijini Dar es salaam, alipofanya ziara ya kushtukiza katika Baraza hilo, kulia kwake ni karani wa baraza hilo, Bahati Rashidi.
 Naibu Waziri, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Angelline Mabula (Mb), akitazama utunzwaji wa mafaili katika masijala alipofanya ziara ya kushtukiza katika Baraza la Ardhi na Nyumba la Kinondoni, pembeni yake ni karani wa baraza hilo; Bahati Rashidi
Naibu Waziri, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Angelline Mabula (Mb), akiongea na Wananchi wa King’azi Juu A, alipofika katika eneo hilo ambalo limekuwa na mgogoro wa ardhi kati ya wilaya ya Kinondoni, Kisarawe na Ilala

No comments: