Sunday, December 26, 2010

Rais Kikwete amteua Jaji Mkuu mpya


TAARIFA YA IKULU
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, amemteua Jaji Mohamed Chande Othman kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania, kuanzia tarehe 28 DIsemba, 2010.

Jaji Othman anachukua nafasi ya Jaji Augustino Ramadhani anayestaafu kwa mujibu wa sheria tarehe 27 DIsemba, 2010.
Kwa sasa Jaji Othman ni Jaji wa Mahakama ya Rufaa na pia ni mtaalamu binafsi juu ya hali ya Haki za Binadamu huko Kusini mwa Sudan, hadi mwezi Agosti 2011.

Jaji Othman alizaliwa tarehe 1 Januari, 1952, ana shahada ya kwanza ya Sheria (LLB) ya Chuo Kikuu cha Dar-Es-Salaam na Shahada ya Uzamili (MA) kutoka katika Chuo Kikuu cha Webster, Geneva-Uswisi.

Amewahi kuwa Makamu wa Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Rwanda huko Arusha na amewahi kushika nafasi sawa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali huko Timor Mashariki.

Jaji Othman pia, amewahi kufanya kazi ndani na nje ya nchi katika Mashirika mbalimbali ya Kitaifa na Kimataifa kama vile Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP) na Shirika la Msalaba Mwekundu.

Jaji Othman ataapishwa kesho tarehe 27 Disemba, 2010 katika viwanja vya Ikulu saa 4:00 asubuhi.

Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi
Ikulu
Dar es Salaam
26 Disemba, 2010

Makazi mapya ya Spika Makinda

Spika wa Bunge Mhe. Anna Makinda akisikiliza maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa makazi ya Spika kutoka kwa Maafisa wa Bunge pamoja na wakandarasi kutoka Wakala wa Ujenzi (TBA).. Picha zote na Owen Mwandumbya wa Bunge.

Jengo la Makazi ya Spika linavyoonekana kwa sasa

Thursday, December 23, 2010

Profesa Ndullu akabidhi fedha mpya kwa JK



The Governor of Bank of Tanzania Prof. Benno Ndulu, today presented the new Tanzanian shilling currency note to President Dr. Jakaya Kikwete at Dar es Salaam State House this evening. The New Currency Note will be in circulation from January next year and they will be used alongside with the current bank notes. In the Picture The Central Bank Governor Prof. Ndulu (left) presents a special album with new Tanzanian shilling currency notes to President Dr. Kikwete while the Minister for Finance Mustafa Mkullo,(right) looks on.

Wednesday, December 22, 2010

Michuano ya Netball

Mfungaji wa Morogoro Zuhura Twalibu akimiliki mpira dhidi ya wachezaji wa Mwanza wakati wa mechi ya nusu fainali ya kombe la Taifa la netiboli iliyofanyika viwanja vya shule ya sekondari Filbert Bayi Kibaha mkoani Pwani jana. Picha na Silvan Kiwale

Mfungaji wa Morogoro Zuhura Twalibu akiwa kwenye hekaheka ya kufunga huku akiwa kwenye ulinzi wa wachezaji wa Mwanza. Mfungaji wa Morogoro Zuhura Twalibu (kulia) akifunga goli wakati wa mechi
ya nusu fainali ya kombe la taifa la netball dhidi ya Mwanza iliyochezwa kwenye uwanja wa Filbert Bayi Kibaha mkoani Pwani jana. Picha zote za Silvan Kiwale.

Tuesday, December 21, 2010

Mary apata shahada ya uzamivu




Mkuu wa United Graduate College and Seminary, Clyde Rivers,(kulia) akimkabidhi Shahada ya Uzamivu ya Masuala ya Jamii katika Kuthamini Utu, Mary Mwanjelwa, (wapili kushoto) kutoka kushoto ni askofu,Dkt,Arthun Kitongo wa Association of Evangelicals in Africa, Joe Mzunda na Prof Nathan Kabara.

Saturday, December 18, 2010

Mariam Mohammed ndiye mshindi Bongo Star Search



Mwanadada Mariam, aliyejipatia umaarufu katika BSS 2010 kwa umahiri wake wa kuimba miondoko ya Taarabu, usiku wa kuamkia leo ametangazwa kuwa mshindi wa shindano hilo liliofanyika katika ukumbi wa Mlinami City jijini Dar es salaam na kushudiwa na Waziri wa habari, Michezo na Vijana, Emmanuel Nchimbi.
Pichani, Mariam akishangilia ushindi wake baada ya kukabidhiwa zawadi yake ambayo ni shilingi za bongo milioni 30 na zawadi nyingini kibao! kwa taarifa zaidi ingia http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/marim-ndiye-mshindi-bss-2010

Monday, December 13, 2010

Kifo hakina huruma kimemchukua Dk Remmy




Mwanamuziki mkongwe na kipenzi cha watu wengi nchini, Ramazani Mtoro Ongala au maarufu kama Dokta Remmy amefariki dunia usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake Mbezi.

Habari zilizopatikana katika eneo la msiba leo asubuhi zinasema msiba wa mwanamuziki huyo utakuwapo nyumbani kwake Sinza kwa Remmy jijini Dar es Salaam. Taarifa zaidi za mipango za mazishi tutawaleteeni baadaye.

Dk Remmy Ongala ni mmoja wa wanamuziki waliojipatia umaarufu nchini Tanzana tangu miaka ya 1980 kutokana na umahiri wake katika masuala ya muziki.

Ongala, mwanamuziki mwenye asili ya Kikongo, alizaliwa mwaka 1947 Kisangani huko Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo (DRC), wakati huo ikijulikana kama Zaire, na ndiko alikoanza kujihusisha na muziki wa dansi.

Alisema kwamba alianza kuupenda muziki tangu akiwa mtoto kwa sababu ni moja ya fani iliyokuwa damuni, pia anaamini Mungu ndiye aliyempatia kipaji mpaka kufikia kupendwa na wapenzi wengi wa muziki.

Mnamo mwaka 1964 ndio alianza rasmi masuala ya muziki akiwa DRC na bendi ya Grandmike.

Mwaka 1967 alijiunga na kundi lingine lililojulikana kama Sakses Bantu ambalo pia lipo hukohuko DRC.

Ongala alikuja nchini katika miaka ya 1970 na kufanikiwa kuendelea na muziki ambapo alianzisha bendi yake ya Super Matimila na kutoa albamu kadhaa kama "Kilio cha Samaki" na nyinginezo.

Mkongwe huyu anakumbukwa na nyimbo zake zilizotikisa ulimwengu wa muziki wa dansi kama 'Mambo kwa Soksi', 'Kifo Hakina huruma', 'Mambo Mbele kwa mbele' na nyinginezo nyingi zilizomfanya ajipatie umaarufu nchini na nje ya nchi.

Sunday, December 12, 2010

KILIMANJARO STARS MABINGWA WAPYA WA CECAFA


Timu ya Taifa Stars imenyakua ubingwa wa kombe la Tusker Cecafa, Challenge Cup baada ya kuibwaga Ivory Coast kwa bao moja kwa bila katika mchezo wa fainali ya michuano hiyo iliyomalizika muda mfupi uliopita katika uwanja wa taifa.

Mfungaji wa bao hilo alikuwa nahodha wa timu hiyo ya taifa Shadrack Nsajigwa kwa njia ya penati ambapo alikung’uta mkwaju mkali ulioingia wavuni na kumwacha kipa wa timu ya Ivory Coast akigaragara, hiyo ilikuwa dakika ya 31.

Mara baada ya kufunga bao hilo uwanja uliripuka kwa furaha na vifijo, Ushindi huo umekuwa zawadi kuu kwa mgeni rasmi wa shughuli hiyo makamu wa kwanza wa rais wa Zanzibar, Maalim Seifa Shariff Hamad. Mshindi wa tatu ni timu ya Uganda ambayo imemrambisha Ethiopia bao 4-3.

Saturday, December 11, 2010

DONDOO KUHUSU MATONYA



Jina lake halisi ni Paulo Mawezi

Jina Matonya ni la utotoni

Ni mume wa wake watatu

Ni baba wa watoto wawili, Elizabeth na Ernest

Aliishi Kilimatinde, Singida miaka 30 iliyopita

Sasa ni mkazi wa Bahi Sokoni, Dodoma

Alianza 'kazi' ya ombaomba kabla ya uhuru

Hukusanya kati ya sh 4000 na 7000 kwa siku

Alitoroka kambini Moro, akapandishwa kizimbani

Kuila Krisimas 2010 jijini Dar es Salaam

Friday, December 10, 2010

Mkutano wa kukabili uharamia


Waziri ya Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha (kushoto) akikaribishwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP , Saidi Ali Mwema leo asubuhi katika hoteli ya Moven Pick Hotel wakati wa ufunguzi wa programu ya mkutano wa kanda wa wakuu wa polisi kuzungumzia suala la uharamia. kulia ni Kamishna wa Polisi , Paul Chagonja. (picha na Hassan Mndeme- Police Force).



Wednesday, December 08, 2010

Bambaga kuzikwa Musoma kesho



MAZISHI ya aliyekuwa mchezaji wa zamani soka wa Tanzania, Nico Bambaga yanatarajia kufanyika kesho nyumbani kwao Musoma mkoani Mara.

Bambaga alifariki dunia usiku wa Jumatatu katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo jijini Dar es Salaam, alikuwa akisumbuliwa na homa ya mapafu.

Msemaji wa familia ya marehemu alisema jijini Dar es Salaam leo kuwa utaratibu wa mazishi ya mwanasoka huyo yalikuwa yakiendelea vizuri na mwili wake ulitarajiwa kusafirishwa jana kwa maziko ambayo yatafanyika kwa taratibu maalumu nyumbani kwao mjini Musoma.

"Kifo cha mpendwa wetu kwa kweli kimetushtua sana sisi kama wanafamilia na alikua na mchango mkubwa hivyo ameacha pengo kubwa kwetu ambalo si rahisi kuzibika kwa sasa.

Msiba huu si pengo kwetu tu bali kwa wanafamilia wote wa soka nchini kwani Nico alikuwa mchezaji wa kutumainiwa na ambaye aliweza kuichezea pia na timu ya taifa,"alisema.

Wakati wa uhai wake, Bambaga alizichezea Pamba ya Mwanza kabla ya kuhamia Yanga na baadaye Simba, Malindi ya Zanzibar, wakati huo akiichezea pia Taifa Stars. Imeandikwa na Jessca Nangawe.

Tuesday, December 07, 2010

Mshindi wa pili wa Shindano la Tusker Project Fame awasili






LICHA ya Mganda Davis Ntare kutwaa taji la Tusker Project Fame 2010, jopo la majaji kwa pamoja na uongozi wa chuo cha mafunzo cha shindano hilo wamekiri kwamba mshiriki wa Tanzania, Peter Msechu, ana kila sababu ya kuwa ndiye mshindi wa shindano.

Kila mtu kwa wakati wake, majaji Ian, Hermes Joachim na Juliana Kanyomozi, walimtaja Msechu kuwa ni mwanamuzikii maarufu anayejiamini sana na kujiweza jukwaani, na pia mbunifu.

Sifa hizo ndizo zinazotakiwa kwa mwanamuziki wa karne hii iliyojaa utandawazi, walieleza majaji.

Msechu ambaye kete yake ya mwisho aliitupa kwa kutumia kwa kibao cha Kilwa Jazz aliudhihirishia tena umma wa wengi katika Afrika Mashariki kwamba anaweza kuwainua kwenye viti na kuwaimbisha muda wowote anaotaka.

Msechu, huku akionyesha kujiamini kwamba muziki ni njia pekee ya kueleza hisia zake kwa jaji huyu kwani, angepata wapi nafasi nyingine ya kumwambia.

"Ningemuita nikamwambia nina maongezi naye angekuja?", alisema Msechu katika mkutano na waandishi wa habari mara baada ya onyesho hilo kwisha na washindi kutajwa katika maeneo ya Ruaraka, jijini Nairobi, eneo ambapopia yapo makao makuu ya East African Breweries, watengenezaji wa bia ya Tusker.

Akizungumza na Mwananchi, Msechu ambaye ameshinda mkataba wa mwaka mmoja wa wa kurekodi na Kampuni ya Africa Sound yenye makao makuu nchini Kenya alisema anaamini kuwa yeye ni mshindi, ila zawadi kubwa amechukua Davis, na atalithibitisha hilo atakapoanza rasmi kazi yake ya muziki, mashabiki wataendelea kufurahi kumsikiliza na kumuona jukwaani.

Monday, December 06, 2010

Teknolojia ya digitali yatinga mahakamani



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Mohamed Gharib Bilal, akizinduwa mfumo wa kurekodi mashauri mahakamani kwa kompyuta na Tovuti ya Mahakama katika ukumbi wa Mahakama Kuu jijini Dar es salaam leo.

******************************************************



HATIMAYE Mahakama ya Tanzania imeanza rasmi kutumia teknolojia ya kisasa katika kuendesha shughuli zake, baada ya kuzindua mfumo mpya wa kuweka kumbukumbu za mashauri mbalimbali kwa kutumia kompyuta.
Mfumo huo wa digitali ulizunduliwa jana na Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib Bilal kwenye ukumbi wa Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.
Sambamba na mfumo huo, mahakama pia imezindua tovuti yake ambayo itakuwa na taarifa mbalimbali kuhusu sheria zinazotumika nchini, hukumu za kesi za kuanzia mwaka 1979 na taarifa nyingine kuhusu kesi zinazoendelea mahakamani.
Kutokana na kuzinduliwa kwa mfumo huo sasa majaji wa Mahakama Kuu na wa Mahakama ya Rufani hawatalazimika kuchukua kumbukumbu za mwenendo wa kesi mbalimbali kwa kuandika kwa mikono na badala yake kazi hiyo itafanyika kwa kutumia kompyuta maalum.
Katika mfumo huo mwenendo wa kesi utakuwa unaingia kwenye kifaa maalumu cha kuhifadhia sauti kwenye kompyuta na baada ya dakika tatu sauti hizo huanza kuchapwa na wataalumu na kuwekwa katika maandishi.
Kwa kuanzia, mfumo huo utaanza kutumiwa na majaji wa Mahakama ya Rufani na wa Mahakama Kuu Dar es Salaam kabla ya kuziunganisha kanda nyingine 14 ikiwa ni pamoja na mahakama za chini.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mfumo huo, Dk Bilal alisema matumizi ya teknolojia hiyo yataharakisha usikilizaji wa kesi, lakini yatajenga mazingira mazuri kwa wawekezaji nchini.
Dk Bilal alisema ni matakwa ya haki na katiba ya nchi kuwa kesi zimalizike katika muda muafaka, lakini zimekuwa hazimaliziki mapema na kusababisha mahakama kulalamikiwa kwa kuchelewesha kumaliza kesi mbalimbali.
Aliitaka mahakama kutumia sheria kwa ufanisi na kwamba kasi katika kuhitimisha kesi imaanishe upatikanaji wa haki badala ya kuzua mashaka.
Badala ya kuahirisha kesi mara kwa mara, Dk. Bilal aliitaka mahakama kuhakikisha kuwa kesi zinaeneshwa kwa kasi, kwa wakati ikiwa ni pamoja na kuhitimishwa kwa haki na usawa.
“Wafanyabiashara na wawekezaji wanavutiwa kuwekeza katika nchi ambazo utekelezaji wa mikataba ni rahisi kwa maana kwamba gharama za kufungua mashauri ni za chini na kesi kuendeshwa kwa haraka,” alisema Dk. Bilal .
Alisema matarajio ni kwamba kampuni ambazo zina matatizo ya kisheria katika shughuli zake za kibiashara, lazima yaweze kutatuliwa haraka ili kuwezesha uzalishaji wa bidhaa na utoaji wa huduma wa kampuni hizo.
Dk. Bilal alisisitiza kwamba haki za binadamu na katiba yetu zimejenga mazingira ya haki na usawa katika usikilizwaji wa mashauri na kwamba mahakama ndio yenye jukumu hilo.
Akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, Jaji Mkuu Agustino Ramadhani alisema mahakama imekuwa ikilalamikiwa kwa kuchelewa kumaliza mashauri kutokana na kutumia zaidi mfumo wa uchukuaji wa kumbukumbu unaotegemea kuandika kwa mkono tu.
Alisema kuzinduliwa kwa mfumo huo mpya wa kiteknolojia kutawawezesha majaji kuepukana na mfumo wa kizamani na hivyo kuharakisha uhitimishwaji wa kesi.
Jaji Ramadhani alisema faida kubwa ya mfumo huo ni kumwezesha Jaji Mkuu na Jaji Kiongozi kujua kila kinachofanywa na kila jaji wa Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu.
Imeandikwa na James Magai wa Mwananchi

Wednesday, December 01, 2010

Happy Birthday Dear First Lady Salma Kikwete



Rais Dk Jakaya Mrisho Kikwete akilicharaza gitaa wakati alipowaongoza wanafamilia nyumbani kwake kumpongeza mkewe Mama Salma Kikwete wakati wa sherehe yake ya kuzaliwa na kutimiza miaka 47 jana.

Kumbe mgomo wa Ustawi wa jamii ni kanyaboya


SERIKALI ya wanafunzi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii imesitisha mgomo wao mara tu baada ya raisi wa chuo hicho kuitwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda ofisini kwake na kumuahidi kushughulikia matatizo ya chuo hicho ndani ya wiki moja.

Hata hivyo habari tulizozipata kutoka katika chanzo chetu cha habari zinaeleza kuwa tatizo la chuo hicho linasabababishwa na mpasuko uliopo ndani ya uongozi wa chuo kwa kudai kuwa na makundi mawili mbayo yanavutana ili kuharibiana sifa.

“Hapa chanzo cha tatizo ni Baraza la Usajili wa vyuo vya Ufundi ya kati(NACTE) ambayo ilileta muongozo na sifa zinazotakiwa kwa baadhi ya watu wanaotakiwa kuwa ndani ya uongozi wa chuo,” kilisema chanzo hicho.
Kilisema kuna watu ambao wapo katika nafasi nyeti za uongozi wa chuo na hawana sifa zilizotajwa na NACTE ivyo basi wameamua kutumia wanafunzi ili waweze kukamilisha lengo lao.
“Wanafunzi wanatumiwa kama chambo tu lakini wao hawajui chuki imejengwa na watu kutoka juu na mtu huwezi kulazimisha kukaa mahali wakati huna sifa za kuwa na cheo kuwa na mdaraka serikalini sio sababu ya kuweka mizigo katika sekta muhimu kama hizi,” kilisema chanzo hicho.
Hata ivyo raisi wa serikali ya wanafunzi ya chuo hicho jana aliitwa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii ili kuweza kupata ufumbuzi wa tatizo lao.