Wednesday, December 16, 2015

PROFESA MWANSOKO AWAAGA WATUMISHI WA IDARA YA MAENDELEO YA UTAMADUNI

 Mkurugenzi wa maendeleo ya Utamaduni Profesa. Hermas Mwansoko akipokea zawadi ya picha inayoonyesha maisha ya kijijini wakat wa hafla kumugaa jana jijini Dar es Salaam.anayemkabidhi zawadi hiyo ni Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya Utamaduni sehemu ya Sanaa Bibi. Leaha Kihimbi . Mkurugenzi huyo anastaafu rasmi kuanzia tarehe 25 Desemba 2015.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni Profesa. Hermas Mwansoko akiwa katika picha ya pamoja na baadhi watumishi wa Idara ya Maendeleo ya Utamaduni wakati hafla ya kumuaga rasmi Mkurugenzi huyo anayemaliza muda wake jana ofisini kwake. 

 Mkurugenzi wa maendeleo ya Utamaduni Profesa. Hermas Mwansoko akizungumza na watumishi wa Idara ya Maendeleo ya Utamaduni wakati akiwaaga rasmi jana ofisini kwake. Mkurugenzi huyo anastaafu rasmi kuanzia tarehe 25 Desemba 2015.
 Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya Utamaduni sehemu ya Sanaa Bibi. Leaha Kihimbi akielezea jambo wakati wa hafla ya kumuaga Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni anayemaliza muda wake Profesa Hermas Mwansoko (kulia) jana jijini Dar es Salaam.

 Afisa Utamaduni wa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Msami akitoa neno kwa niaba ya watumishi wa Idara ya Utamaduni wakati wa hafla ya kumuaga Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni anayemaliza muda wake katika utumishi wa umma Profesa. Hermas Mwansoko jana jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya watumishi wa Idara ya Utamaduni wakifuatilia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea wakati wa hafla ya kumuaga Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni anayemaliza muda wake katika utumishi wa umma Profesa. Hermas Mwansoko jana jijini Dar es Salaam.


Picha na Frank Shija,WHVUM

No comments: