Friday, November 28, 2008

Barabara



Picha ya kwanza ni mto unaokatisha barabara ya kuunganisha kijiji cha Uwiro na Ngerenanyuki wilayani Arumeru ukiwa umejaa maji na hivyo kusababisha kero kubwa kwa wakazi wa kata ya Ngarenanyuki kutokana na kutokuwa na daraja kwa miaka mingi sasa. picha na Mussa Juma

Thursday, November 27, 2008

ADB imemwaga bilion 192.9/- kwa ajili ya bajeti


Treasury Permanent Secretary Gray Mgonja exchanges documents with African Development Bank Resident Representative Ms Sipho Moyo after signing 192.9 billion Tshs for the General Budget Support in Dar es Salaam today.

ADB imemwaga bilion 192.9/- kwa ajili ya bajeti


Treasury Permanent Secretary Gray Mgonja exchanges documents with African Development Bank Resident Representative Ms Sipho Moyo after signing 192.9 billion Tshs for the General Budget Support in Dar es Salaam today.

East African artists for Nairobi Concert

Word in town is that there will be a mega concert in Nairobi on 6th December 2008, during which the curtain will be pulled off a fresh and new movement for the young folks which is causing a huge buzz in Nairobi. We have established that the movement known as Generation Jipange has attracted the interest of top performers from Uganda and Tanzania.

Generation Jipange, is the latest craze in town, a new culture for the youth, that youngsters are positioning themselves to be part of this phenomenon which promises to change their lives and will redefine the youths lifestyle as we know it today.

This one of a kind music concert will be held in Nairobi at Uhuru Gardens, Langata road. The concert kicks off at 9 am till 6pm and it is FREE FOR ALL. No gate charges.

Some of the local Kenyan artists who will be performing at the concert include Mejja, Jimwat, Maddtraxx, award winning Juacali, MTV Africa Music Awards winner Wahu, Wyre, Big Pin, and recent Channel O music awards nominees Nameless and Amani, M.O.G., Sarakasi and Sina X..

Tanzania will be represented by TMK Wanaume, THT Dance Group and Professor J, while the eccentric Bebe Cool will be in Nairobi to share the stage wtih Klear Kut also from Uganda.

We have confirmed that the top cream of Nairobi’s hottest DJ’s are not missing this one. They will be playing in the all day long music fest among them M.O.B., HomeBoyz, CodeRED, Black Supremacy and the Dohty Family

To keep the concert rocking and kicking all day long and to tell you more about the Jipange, MCs Big Tedd, Porgie, KJ, Kriss Darling and Eve D'Souza will take turns at the microphone to liven up the day as the coolest guys join Generation Jipange.

Tuesday, November 25, 2008

Mramba, Daniel Yona kizimbani kwa ufisadi







MAWAZIRI wawili waliowahi kuongoza wizara mbalimbali ikiwamo nyeti ya fedha katika serikali ya awamu tatu, Basil Mramba na Daniel Yona wamefikishwa kortini kwa matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya Sh11.7 bilioni.

Mramba na Yona walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana mbele ya Hakimu Hezron Mwankenja saa 5.40, wakasomewa mashtaka na baadaye kupelekwa rumande kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.

Vigogo hao walifikishwa mahakamani baada ya uvumi wa tukio hilo kudumu kwa takribani majuma mawili.

Wakati wakiingia mahakamani jana Mramba ambaye ni mtuhumiwa wa kwanza katika kesi hiyo namba 1200 ya mwaka huu, alisikika akiwahoji waandishi iwapo wamefurahi kufikishwa kwao mahakanai hapo, huku akidai kuwa watapiga picha

Sunday, November 23, 2008

Mambo ya ngorongoro





Kuna mambo makubwa huko Ngorongoro mdau Alphan Mlacha alikuwapo huko kwa takribani wiki nzima akiwa katika ziara ya kikazi iliyomwezesha yeye na wadau wengine wa habari ambapo walipata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya hifadhi hiyo ya taifa ambayo ina umaarufu mkubwa duniani, juu kabisa waweza kuwaona wamasai wakiwa karibu kabisa na maboma yao, kisha picha zinazofuata zinaonyesha uoto wa wa asili na maboma mengine hii ziara mdau mlacha aliifanya juzi tuu.

Monday, November 17, 2008

msimu wa machungwa


Mfanyabiashara katika eneo la mnada wa Sabasaba Manispaa ya Morogoro akipanga machungwa chini ya ardhi huku akipingana na utaratibu wa kutofanya biashara ya matunda katika mnada huo. machungwa hayo alikuwa akiuza kwa fungu sh 300. (Picha na Juma Ahmadi, MSJ).

mgomo wa walimu noma


PPichani wanafunzi wa shule ya msingi, Kiranyi na Unyuata wilayani Arumeru wakiwa wanacheza ovyo baada ya walimu wao kuanza mgomo jana.
picha na mussa juma


Wednesday, November 12, 2008

Uingereza yabana masharti ya viza

KWA wale wanaotaka kwenda Uingereza bila ya mipango ya muda mrefu, sasa wanatakiwa kujipanga upya; Uingereza imeongeza masharti mapya na magumu ya viza duniani kote.

Watanzania wanaokadiriwa kuwa kati ya 8,000 na 9,000 huomba visa ya kuingia taifa hilo kongwe kila mwaka, lakini masharti hayo mapya yanaweza kufanya idadi hiyo kupungua.

Moja ya masharti hayo ni lile linalomtaka Mtanzania yeyote anayetaka kuingia Uingereza, kama ilivyo kwa raia wengine wote wasio Waingereza duniani kote, sasa anapaswa kuwasilisha maombi ya viza wiki sita kabla ya siku ya safari.

"Ubalozi wa Uingereza hautakuwa tena na uwezo wa kuwezesha upatikanaji wa viza, ikiwa mwombaji atatoa taarifa ya muda mfupi," alisema afisa habari wa ubalozi wa Uingereza nchini, John Bradshaw.

Chuo Kikuu watimuliwa









UONGOZI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kampasi ya Mlimani umewasimamisha masomo wanafunzi wa shahada za kwanza kwa muda usiojulikana.

Hatua hiyo imekuja baada ya wanafunzi hao kukaidi amri ya chuo pamoja na ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Prof Jumanne Maghembe, iliyowataka kusitisha mgomo na kurudi madarasani wakati wizara ikishughulikia madai yao.

Kufuatia hatua hiyo, Rais wa Serikali ya wanafunzi wa chuo hicho, Anthony Machibya, aliwatangazia wanafunzi wenzake juu ya kusimamishwa huko na kusisitiza kuwa, pamoja na kufukuzwa chuoni hapo, lakini watakaporudi wataendeleza harakati za kudai haki yao mpaka watakapoipata.

Tuesday, November 11, 2008

Miriam Odemba akuna wengi Miss Earth


MWAKILISHI wa Tanzania katika mashindano ya Miss Earth, Miriam Odemba ameibuka mshindi wa nafasi ya pili katika kinyangíanyiro hicho kilichofanyika Jumapili usiku kwenye ukumbi wa Clark Expo Amphitheater, Angeles City, Pampanga nchini Philippines.

Hii ni mara ya kwanza tokea kuanzishwa kwa mashindano hayo kwa Mtanzania kumaliza katika nafasi ya juu na ni mara ya pili katika Afrika kushika nafasi hiyo ya juu kabisa katika mashindano hayo.

Nyota ya Odemba ilianza katika mashindano ya awali ambapo alifanikiwa kutwaa tuzo ya Miss Aficionado. Ameibuka mshindi wa kipengele cha masuala ya mazingira kinachohusu hali ya hewa.

Mrembo wa Kenya, Winfred Omwakwe alishinda taji la Miss Earth mwaka 2002 mjini Manila na kuweka historia kuwa msichana wa kwanza kutwaa taji hilo duniani.

ìNina furaha kubwa kutwaa nafasi hii, niliandaliwa kushinda na nimeshinda, namshukuru Mungu na pia mwandaaji wangu, Sarungi (Maria) kwa kunipa nafasi hii ya kuiwakilisha taifa na kufanikiwa kutwaa nafasi hii, nawashukuru Watanzania wote walionipa sapoti kubwa kabla ya mashindano,î alisema Odemba kwa njia ya simu jana baada ya kuisha kwa mashindano hayo.

Alisema kuwa ushindi huo ni sifa kwake, kwa Kampuni ya Compass Communication chini ya Maria Sarungi na Tanzania nzima kwani lengo lilikuwa kuipromoti Tanzania nje ya mipaka na lengo limetiamia.

Kwa mujibu wa Odemba, mashindano hayo yalikuwa magumu sana na alijitahidi na kutumia uwezo wake wa kimataifa kufanya vyema.

Katika mashindano hayo, mrembo wa Philippines Karla Henry, 22, alifanikiwa kutwaa taji hilo kwa kuwashinda warembo 84 kutoka nchi mbalimbali duniani.

Miss Mexico, Abigail Elizalde alishinda nafasi ya tatu wakati ya nafasi ya nne ilichukuliwa na mrembo wa Brazil, Tatiane Alves.

Warembo nane bora wa mashindano hayo ni Mariana RodrÌguez (Colombia), Adriana ReverÛn (Hispania), Nasanin Nuri (Uswisi) na Daniela Torrealba wa Venezuela.

Warembo 16 bora wa mashindano hayo ni Hana Svobodov· (Jamhuri ya Czech), Seo Seol-hee (Korea), Uko Ezinne (Nigeria), Karolina Filipkowska (Poland), Ruxandra Popa (Romania), Anna Mezentseva (Russia), Piyaporn Deejing (Thailand), Jana Murrell (Marekani)

Habari hii ni kwa mujibu wa Majuto Omary wa The Citizen

R.I.P Miriam Makeba


A South African singer Miriam Makemba died 76.

She was an amazing icon.
A strong woman who took African music to the next level.

Not only South Africa, but the all Africa continent will always be proud of you.

May Lord rest her soul in peace. Amen!
(March 4, 1932-November 9,2008)

Monday, November 10, 2008

Msanii kutoka nchini Marekani Kat De Luna











Msanii kutoka nchini Marekani Kat De Luna usiku wa kuamkia leo alikonga nyoyo za wabongo katika tamasha kubwa la Fiesta 2008’ Jirambe’ baada ya kupiga shoo ya kufa mtu na kuwafanya wanazi wa burudani waliokuwa wamefurika katika viwanja vya Leaders Club Jijini Dar es Salaam kumshangilia muda wote. Vibao vyake vya Am I Dream’ng na Run the Show ndivyo vilivyowadatisha wengi na kuwafanya mashabiki hao kuimba naye sambamba.

Sambamba na mwanadada huyo, pia kijana kutoka Dodoma ‘East Zuu’ Albert Mangwea ‘Ngweair’ akiwa sambamba na msela wake Mchizi Mox waliwakimbiza vilivyo mashabiki. Wasanii wengine waliokamua ni Ali Kiba, Mr.Blue, Profesa Jay, Nakaaya,Q Jay, Q Chief, Mwasiti, J-Moe, Bushoke, makundi ya TMK Wanaume Family na Halisi, bendi ya FM Academia ‘Wazee wa ngwasuma’ na wengine kibao waliofanya mashabiki kujiramba.

Thursday, November 06, 2008

Vurugu chuo kikuu




Unaona hapa ni kama vile kuna vita, wala si watu wengine bali ni wanafunzi wa Chuo KIkuu cha Dar es salaama wakipambana wao kwa wao ambapo wamewajeruhi wenzao kwa mawe na chupa katika harakati za kuwaondoa wengine madarasani.

Tukio hilo lilisababishwa na vurugu kati ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliogoma wakitaka wapewe asilimia 100 ya mikopo inayojumlisha fedha za kujikimu na ada za masomo na baadhi yao ambao walipinga mgomo huo, baada ya waliogoma kuwalazimisha wenzao kutoka madarasani.

Wanafunzi wawili wamelazwa katika zahanati ya chuo ambao ni Makala Simon mwanafunzi wa mwaka wa tatu wa Chuo cha Uhandisi na Teknolojia ambaye amepigwa jiwe na kujeruhiwa shavu la kushoto.

Pia yupo Benedict Edward aliyejeruhiwa kichwani baada ya kupigwa chupa ya soda kichwani ambaye hali yake ilizidi kuwa mbaya na akapelekwa hospitali ya Misheni Mikocheni kwa matibabu zaidi.

Wednesday, November 05, 2008

Obama Rais wa Marekani




WASHINGTON – His name etched in history as America's first black president, Barack Obama turned from the jubilation of victory to the sobering challenge of leading a nation worried about economic crisis, two unfinished wars and global uncertainty.
"The road ahead will be long. Our climb will be steep," Obama cautioned.
Young and charismatic but with little experience on the national level, Obama smashed through racial barriers and easily defeated Republican John McCain to become the first African-American destined to sit in the Oval Office, America's 44th president. He was the first Democrat to receive more than 50 percent of the popular vote since Jimmy Carter in 1976.
"It's been a long time coming, but tonight, because of what we did on this date in this election at this defining moment, change has come to America," Obama told a victory rally of 125,000 people jammed into Chicago's Grant Park.
Obama scored an Electoral College landslide that redrew America's political map. He won states that reliably voted Republican in presidential elections, like Indiana and Virginia, which hadn't supported the Democratic candidate in 44 years. Ohio and Florida, key to Bush's twin victories, also went for Obama, as did Pennsylvania, which McCain had deemed crucial for his election hopes.
With just 76 days until the inauguration, Obama is expected to move quickly to begin assembling a White House staff and selecting Cabinet nominees.
Campaign officials said Illinois Rep. Rahm Emanuel was the front-runner to be Obama's chief of staff. The advisers spoke on a condition of anonymity because the announcement had not yet been made.
Democrats expanded their majority in both houses of Congress. In the Senate, Democrats ousted Republicans Elizabeth Dole of North Carolina and John Sununu of New Hampshire and captured seats held by retiring GOP senators in Virginia, New Mexico and Colorado. Still, the GOP blocked a complete rout, holding the Kentucky seat of Senate Minority Leader Mitch McConnell and a Mississippi seat once held by Trent Lott — two top Democratic targets.
In the House, with fewer than a dozen races still undecided, Democrats captured Republican-held seats in the Northeast, South and West and were on a path to pick up as many as 20 seats.

Sunday, November 02, 2008

Rais Kikwete



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisisitiza jambo wakati alipokutana na mawaziri wa mambo ya nje wa Uingereza Bwana David Miliband(kushoto) and Waziri wa Mambo ya nje wa Ufaransa Bwana Bernard Kouchner ikulu jijini Dar es Salaam kujadili hali ya vita nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo na juhudi za kimataifa kutatua mzozo huo.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akijadili jambo na Mawaziri wa Mambo ya nje wa Uingereza David Miliband(kushoto) na Bernard Kouchner(katikati) wakati mawaziri hao walipomtembelea Rais Kikwete ikulu jijini Dar es salaam leo asubuhi na kujadili hali ya mapigano Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo(DRC)