Monday, December 21, 2015

WAZIRI KITWANGA AKUTANA NA VIONGOZI WAKUU WA JESHI LA POLISI, WAWEKA MKAKATI WA KUKABILIANA NA UHALIFU NCHINI

NGA1
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu wakati alipokuwa anawasili Makao Makuu ya Jeshi hilo, jijini Dar es Salaam kwa ziara ya kikazi. Waziri Kitwanga alifanya mazungumzo na Viongozi Wakuu wa jeshi hilo na kukubaliana kuweka mikakati zaidi ya kukabiliana na uhalifu nchini. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.,
NGA2
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu akitoa taarifa mbalimbali za shughuli zinazofanywa na jeshi hilo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati), wakati Waziri huyo alipofanya ziara Makao Makuu ya Jeshi hilo, jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuzungumza na Viongozi Wakuu wa jeshi hilo, ambapo walikubaliana kuweka mikakati zaidi ya kukabiliana na uhalifu nchini.
NGA3
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya kumaliza mazungumzo na Viongozi Wakuu wa Jeshi la Polisi nchini. Waziri Kitwanga aliwaambia waandishi wa habari kuwa, wamekubaliana na Viongozi Wakuu wa jeshi hilo kuweka mikakati zaidi ya kukabiliana na uhalifu nchini. Wapili kushoto meza kuu ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu. Wapili kulia meza kuu ni Naibu IGP, Abdulharam Kaniki. Kulia ni Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo wa Jeshi hilo, Paul Chagonja. Kushoto meza kuu ni Kamishna wa Polisi Jamii nchini, Mussa Ali Mussa. Kushoto ni Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina wa Jeshi la Polisi, Suleiman Kova.
NGA4
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati waliokaa), Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu (watatu kulia waliokaa) wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Wakuu wa Jeshi la Polisi nchini mara baada ya kikao chao kilichofanya katika Ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Jeshi hilo kumalizika. Waziri Kitwanga alifanya mazungumzo na Viongozi hao na kukubaliana kuweka mikakati ya kupambana na uhalifu.
NGA5
Msafara wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga ukiwasili katika lango Kuu la Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Viongozi Wakuu wa Jeshi hilo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.,

No comments: