Friday, September 29, 2017

ZIARA YA MJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI WA NHC KATIKA JENGO LA UBIA -MWANZA



Mkurugenzi wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa, Injini Kesogukewele Msita akijadiliana jambo na Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa mkoa wa Mwanza Injinia Benedict Kilimba alipokuwa akikagua Jengo la ubia katika kiwanja Na 94/S Mtaa wa Nyerere jijini Mwanza linavyoonekana. Jengo hilo limepewa jina la SEIF PLAZA kwa kuwa mbia wa NHC anaitwa Mr. Seif.
 Mkurugenzi wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa, Injini Kesogukewele Msita akijadiliana jambo na Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa mkoa wa Mwanza Injinia Benedict Kilimba alipokuwa akikagua Jengo la ubia katika kiwanja Na 94/S Mtaa wa Nyerere jijini Mwanza linavyoonekana. Jengo hilo limepewa jina la SEIF PLAZA kwa kuwa mbia wa NHC anaitwa Mr. Seif.
Jengo hilo limepewa jina la SEIF PLAZA kwa kuwa mbia wa NHC anaitwa Mr. Seif.

Injinia Msita akipokea maelezo kutoka kwa Mbia aliyejenga jengo hilo Mr .Seif ndani ya duka lake linalouza vifaa vya ujenzi.

JAFO AWATAKA WATENDAJI MANYONI KUSIMAMIA MIRADI IPASAVYO

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akiwa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Ikungi Miraji Mtaturu wakikagua chumba cha kuhifadhia maiti katika kituo cha Afya Kintinku wilayani Manyoni.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua magodoro katika wodi ya wagonjwa kwenye Kituo cha Afya Kintinku wilayani Manyoni.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua chumba cha dawa katika Kituo cha Afya Kintinku wilayani Manyoni.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua Kituo cha Afya Kintinku wilayani Manyoni.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akisisitiza jambo alipokuwa akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua Kituo cha Afya Kintinku wilayani Manyoni.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo akikagua mradi wa maji Kintinku wilayani Manyoni.



NAIBU waziri wa Nchi ofisi Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Selemani Jafo amefanya ziara katika kituo cha Afya cha Kitinku kilichopo wilayani Manyoni mkoani Singida na kueleza dhamira ya serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya kwa kuboresha na kujenga miundombinu.

Akizungumza katika ziara hiyo JAFO amesema uboreshaji wa kituo hicho unatarajia kugharimu kiasi cha Sh.Milioni 500 na kwamba tayari serikali imeshaingiza kiasi hicho cha fedha.

Jafo amesema uboreshaji huo utajumuisha ujenzi wa chumba cha upasuaji,chumba cha kuhifadhia maiti,wodi ya kisasa ya akina mama na maabara na kuwataka viongozi wa halmashauri hiyo kuhakikisha hadi desemba 30, mwaka huu ujenzi huo uwe umekamilika.

“Awamu ya kwanza zimeingizwa shilingi milioni 500 kwa ajili ya miundombinu na baada ya ujenzi kukamilika serikali itaweka vifaa vyenye thamani ya shilingi milioni 220,nataka ujenzi huu uende kwa kasi atakayeleta masihara atajuta,”alisema Jafo.

Amewataka watendaji kutimiza wajibu kwa kusimamia malighafi zitumike vizuri na mafundi wajenge majengo kwa ubora na kusisitiza kuwa mafundi wa kujenga majengo hayo watatoka wilayani humo.

Naibu Waziri Jafo amemtaka Mganga Mkuu wa wilaya Dk.Nelson Bukuna kuhakikisha anawajibika ipasavyo kwa kutembelea mara kwa mara kwenye zahanati na vituo vya afya badala ya kusubiri hadi kiongozi afike.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Miraji Mtaturu na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Charles Fussi wameahidi kuhakikisha wanatekeleza maagizo yote yaliyotolewa na serikali na ujenzi wake utafanyika kwa viwango vinavyotakiwa.

Katika hatua nyingine, Jafo ametembelea mradi wa maji wa Kitinku na kumuagiza mkurugenzi wa halmashauri ya Manyoni Charles Fussi kuhakikisha anasimamia timu yake ili azma ya serikali ya kuhakikisha wanamtua ndoo mama ndoo ya maji kichani inafanikiwa kama Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM)inavyosema.Jafo amesisitiza uaminifu na kufanya kazi kwa kasi ili wananchi wapate huduma ya maji wanayotarajia.

“Katika utekelazaji wa miradi hii wakandarasi wengi sio waaminifu,Mkurugenzi hii ni sehemu ya kupima performance yako,usilale hakikisha watu wanapata maji,”amesema Jafo.Kwa upande wake mhandisi wa maji wilaya Gasto Mbondo amesema mradi huo hadi kukamilika kwake utagharimu shilingi bilioni 9.9 na utahudumia wananchi elfu 45,417 wa vijiji 11.

“Mradi huu unatekelezwa kwa awamu tano,na changamoto kubwa tunayokabiliana nayo ni upungufu wa wataalamu wa maji,ukosefu wa gari la kubebea mizigo ya maji na ukosefu wa fedha za kuendesha ofisi,”amesema Mbondo.Naye kaimu Mkuu wa wilaya hiyo, Miraji Mtaturu amepongeza na kumhakikishia Naibu waziri huyo kuwa atasimamia utekelezaji wa mradi huo na kwamba wilaya yake imeweka utaratibu wa kupokea taarifa kwa kina kuhusu miradi ya maji kila mwezi.

Kwa upande wake, Mbunge wa jimbo la Manyoni Mashariki Daniel Mtuka ameishukuru serikali kwa jitihada zake za kutatua kero ya maji katika jimbo hilo na kwamba kwa muda mrefu wananchi wake wamekuwa wakikabiliwa na changamoto hiyo.

MTENDAJI MKUU WA TFS, PROF. DOS SANTOS SILAYO AFANYA ZIARA WILAYANI MKURANGA KWA AJILI YA KUIMARISHA UHIFADHI NA KUJADILI MIKAKATI YA KUZUIA WAVAMIZI KWENYE MISITU WA HIFADHI

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof. Dos Santos Silayo alimpomtembelea jana Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga ofisini kwake akimuonesha baadhi ya maeneo kwenye ramani jinsi vyanzo vya maji vilivyoharibika kutokana na tabia ya baadhi ya wananchi kuvamia kwa kuanzisha shughuli za kibinadamu katika Hifadhi za Misitu. Mwingine ni Meneja Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania wa Wilaya ya Mkuranga Christina Mohamed
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof. Dos Santos Silayo akiteta neno na Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga wakati wa ziara ya kujionea jinsi wananchi walivyovamia na kuanzisha shughuli za kibinadamu katika Hifadhi za Msitu wa Vikindu.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof. Dos Santos Silayo kuu akisaini jana kitabu cha wageni mara alipotembelea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga ikiwa lengo la ziara hiyo ni kujadili mikakati ya kuzuia wavamizi kwenye msitu wa hifadhi
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga akimuonesha Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof. Dos Santos Silayo baadhi ya maeneo ya Hifadhi yaliyovamiwa na kuanzishwa shughuli za kibinadamu katika Hifadhi ya Msitu wa Vikindu. Lengo la ziara Mtendaji Mkuu wa TFS hiyo ilikuwa ni kuimarisha uhifadhi kwa kujadili mikakati ya kuzuia wavamizi kwenye msitu wa hifadhi

Thursday, September 28, 2017

MPANGO WA TAIFA WA DAMU SALAMA WAKABIDHI CHUPA ZA DAMU 300 HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI

 Mpango wa Taifa wa Damu salama kanda ya mashariki Dar es Salaam jana ulikabidhi chupa za Damu 300 kwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.  Akizungumza wakati wa makabidhiano Afisa uhusino Mpango wa Taifa wa Damu Salama Bw. Rajab Mwenda alisema chupa hizo za Damu zitasaidia kuokoa maisha ya wahitaji hospitali na zimepatikana kutokana na kampeni ya kukusanya Damu ambayo imeanza wiki hii ambapo mkoa wa Dar es Salaam mpaka jana ulikuwa umeisha kusanya zaidi ya  chupa za damu 500.  
 Bw. Rajab alitumia fursa ya makabidhiano kuwashukuru Jumuiya ya Khoja shia kwa mwitikio wao mkubwa wa kuchangia Damu kwa hiari siku ya Ashura 24/9/2017.  Siku ya Ashura ni siku ambayo Jumuiya ya Khoja shia kila mwaka huwa wanaadhimisha kifo cha Imam Hussein kwa kuchangia Damu. Pia alitoa wito kwa wananchi wajitokeze kwa wingi kuchangia damu kama Ishara ya kuunga mkono jitihada za Mpango kuhamasisha jamii kuchangia Damu ili kupunguza vifoo vinavyoweza sababishwa na uhaba wa Damu
Mwakilishi wa Hospitali ya Muhimbili Bw. Hamisi Shabani Kubiga alishukuru Mpango wa Taifa wa Damu salama kwa kugawia Hospitali ya muhimbili kiasi hicho cha chupa za Damu, chupa hizo zitasaidia kutibu kina Mama na watoto wenye uhitaji wa Damu, Majeruhi wa ajali na magonjwa mengine alisema Bw. Hamisi

WATEJA WA CBA BENKI WAENDELEA KUNUFAIKA NA PROMOSHENI YA"WEKA AMANA USHINDE"

  Mkuu wa Idara ya Huduma za Kibenki wa Benki ya CBA kwa wateja binafsi, Julius Konyani, akizungumza na waandishi wa habari, wakati wa kuchezeshwa droo ya tatu ya ya promosheni ya akiba inayojulikana kama ‘Weka amana ushinde’ zaidi ya milioni 20 zinaendelea kushindaniwa na wateja wa benki hiyo, Dar es Salaam jana. Kulia ni Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Abdallah Hemedi na kushoto ni Mkuu wa Mauzo na Mahusiano ya Kibenki wa CBA, Godson Biyengo.
 Mkuu wa Idara ya Huduma za Kibenki wa Benki ya CBA kwa wateja binafsi, Julius Konyani, akibonyeza kitufe cha kompyuta kwa ajili ya kuchezesha droo ya kuwapata washindi wa promosheni ya akiba inayojulikana kama ‘Weka amana ushinde’ zaidi ya milioni 20 zinaendelea kushindaniwa na wateja wa benki hiyo , Dar es Salaam jana. Kulia ni Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Abdallah Hemedi na kushoto ni Mkuu wa Mauzo na Mahusiano ya Kibenki wa CBA, Godson Biyengo.
 Mkuu wa Mauzo na Mahusiano ya Kibenki wa CBA, Godson Biyengo, akimuonesha Mkuu wa Idara ya Huduma za Kibenki wa Benki ya CBA kwa wateja binafsi, Julius Konyani (katikati) na Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Abdallah Hemedi, mshindi wa droo ya tatu ya ya promosheni ya akiba inayojulikana kama ‘Weka amana ushinde’ zaidi ya milioni 20 zitashindaniwa na wateja wa benki hiyo, mara baada ya kuchezeshwa, Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Idara ya Huduma za Kibenki wa Benki ya CBA kwa wateja binafsi, Julius Konyani, akizungumza na mmoja wa washindi aliyejishindia kitita cha shilingi Milioni 2/- kwenye droo ya tatu ya ya promosheni ya akiba inayojulikana kama ‘Weka amana ushinde’ zaidi ya milioni 20 zinashindaniwa na wateja wa benki hiyo, Dar es Salaam jana. Kulia ni Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Abdallah Hemedi na kushoto ni Mkuu wa Mauzo na Mahusiano ya Kibenki wa CBA, Godson Biyengo.

JUMIA TRAVEL YAUNGANA NA DUNIA KUADHIMISHA SIKU YA UTALII

Mnamo mwaka 2015, Mkutano Mkuu wa Baraza la Umoja wa Mataifa uliutangaza mwaka 2017 kama Mwaka wa Kimataifa wa Utalii Endelevu kwa Maendeleo. Na hivyo kuifanya kauli mbiu ya mwaka huu kuwa ni ‘Utalii Endelevu kwa Maendeleo.’

Maeneo matano ambayo yanaangaziwa na kufanyiwa kazi mwaka huu ni; Ukuaji wa uchumi endelevu na wa pamoja; Ujumuishwaji wa jamii, ajira na kupunguza umasikini; Ufanisi wa rasilimali, utunzaji wa mazingira na mabadiliko ya hali ya hewa; Amali za kiutamaduni, utofauti na urithi; na Maelewano ya pamoja, amani na usalama.

Katika kuunga mkono maadhimisho haya, Jumia Travel ikiwa ni mdau wa masuala ya utalii Tanzania na Afrika kwa ujumla imekuwa ikifanya jitihada za kukuza ufahamu juu ya maeneo na vivutio mbalimbali vya utalii nchini.

Hivi sasa kuna kampeni inayoendelea kwa jina la ‘Destinations Campaign’ ikiwa inalenga kukuza ufahamu juu ya maeneo tofauti nchini ambayo watanzania hawafahamu kama ni vivutio vya kitalii.

Tanzania imebarikiwa kuwa na maeneo mengi lakini hayapewi kipaumbele wala kutangazwa vilivyo. Na endapo ikiwa yanatangazwa, sio yote yanayopata fursa sawa kama vile Zanzibar, Mlima Kilimanjaro na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo watu wengi nchini na duniani wanayafahamu.

Jumia Travel imeamua kuitumia fursa ya kufanya kazi na maelfu ya hoteli nchini na Afrika kuyaangazia maeneo hayo na sehemu ambazo wageni wanaweza kulala. Kikubwa kinachofanyika ni kuwafahamisha watanzania juu ya shughuli tofauti wanazoweza kuzifanya pindi wakitembelea maeneo hayo. Mbali na hapo wamiliki na mameneja wa hoteli huhojiwa juu ya masuala wanayoona yanaweza kuwavutia wateja kwenye hoteli zao.

Jitihada za kukuza ufahamu na kutangaza maeneo mbalimbali nchini zinafanywa pia na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB). Bodi ya Utalii imekuja na mkakati na mbinu mpya kwa kuyatenga maeneo ya usimamizi wa wanyama tofauti na ya kawaida yaliyozoeleka na watalii wengi.

Kwa mfano, hivi sasa TTB inafanya jitihada kubwa za kukuza maeneo matano yaliyomo kwenye mpango wa usimamizi huo ambayo ni Burunge ipo Wilaya ya Babati Mkoa wa Manyara, Randilen ipo Wilaya ya Monduli mkoa wa Arusha, Ikona ipo katika Wilaya ya Serengeti mkoa wa Mara jirani na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Ipole ipo katika Wilaya ya Sikonge mkoa wa Tabora na Mbomipa ambayo ni muunganiko wa vijiji zaidi ya 21 vya tarafa  za Idodi na Pawaga vinavyozunguka Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.
Kwa kufanya hivyo inatoa fursa kwa watalii kuwa na machaguo ya sehemu za kutembelea tofauti na yaliyozoeleka. Kwa sababu hata kwenye maeneo haya watalii wanaweza kukidhi haja zao kwa kuwaona wanyama na kufanya shughuli nyinginezo za kitalii.

Kwa mujibu wa ripoti ya utalii ya mwaka 2016 iliyotolewa na Shirika la Umoja wa Kimataifa la Utalii Duniani, Mwaka 2016 umethibitisha kuwa ni mwaka mwingine wa mafanikio katika sekta ya utalii kimataifa licha ya changamoto kadhaa. Idadi ya watalii kimataifa imekuwa kwa mwaka wa saba mfululizo na kufikia bilioni 1.2, idadi ya ukuaji ambayo haijawahi kutokea tangu miaka ya ‘60’ (1960). Ukuaji mkubwa zaidi umeonekana kwenye sehemu za Afrika, Asia na Pasifiki.
Tunakukaribisha katika kuungana nasi na kusherehekea Mwaka wa Kimataifa wa Utalii Endelevu kwa Maendeleo 2017.

Na Jumia Travel Tanzania


Kila ifikapo Septemba 27 ya kila mwaka dunia huadhimisha siku ya utalii duniani. Maadhimisho hayo hufanywa na kila nchi ambapo kunakuwepo na shughuli kadhaa zikiongozwa na malengo na kauli mbiu tofauti zilizoazimiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani (UNWTO).

SERIKALI YAIPONGEZA COSTECH-OFAB KWA KUANDAA TUZO ZA WAANDISHI WA HABARI ZA SAYANSI 2017

Mwandishi wa Habari wa gazeti la Guardian, Gerald Kitabu akipeana mkono na Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia , Profesa Joyce Ndalichako baada ya kukabidhiwa tuzo ya mshindi wa kwanza kwenye kuandika na kuelimisha umma kuhusu matumizi ya sayansi, Teknolojia na ubunifu hususani Bioteknolojia katika kuendeleza kilimo katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam juzi. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dk. Hassan Mshinda
Washindi wa tuzo hizi wakisubiri kutangazwa.
Wageni waalikwa wakiwa kwenye hafla hiyo.
Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), Jim Yonaz akitoa hutuba katika hafla hiyo.
Mratibu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAB), Philbert Nyindondi akielezea tuzo hizo
Mkurugenzi Mkuu wa COTECH, Dk.Hassan Mshinda akizungumzia tuzo hizo
Waziri Ndalichako akihutubia katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Dk.Ayoub Rioba akizungumza kwenye hafla hiyo.
Mshindi wa tuzo hizo kutoka mkoani Kagera, Benson Eustace wa Clouds Media kikabidhiwa cheti chake.
Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), Jim Yonaz akikabidhiwa cheti kutokana na mchango mkubwa wa vyombo hivyo katika kuandika habari za sayansi.
Mwakilishi wa TBC, akikabidhiwa cheti kutokana na mchango wa kuandika habari za sayansi.
Ofisa Mawasiliano wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha SUA ambaye pia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu Kujiendeleza (ICE), Bujaga Inzengo Kadago akipokea cheti kutokana na mchango wa vyombo vya habari vya chuo hicho wa kuandika habari hizo.
Mwanahabari wa gazeti la Habari Leo, Lucy Ngowi akikabidhiwa cheti.
Mwanahabari Hellen Kwavava akikabidhiwa cheti.
Mwanahabari wa Gazeti la Nipashe mkoani Kagera, Restuta Damian akipokea cheti.
Mwanahabari wa gazeti la Guardian, Daniel Simbei akipokea cheti.
Mwanahabari Calvin Gwabara kutoka SUA akipokea cheti.
Mwanahabari wa gazeti la Daily News, Fatma Abdul akipokea cheti.
Mwanahabari Elias Msuya wa Gazeti la Mwananchi akikabidhiwa cheti.
Mwanahabari wa RFA kutoka Mwanza, Coleta Makulwa akipokea cheti
Mwanahabari wa gazeti la Habari Leo, Shadrack Sagati akikabidhiwa cheti.
Mwanahabri Dino Mugunde wa Star TV Mwanza akipokea cheti.
Waziri Ndalichako akiwa katika picha ya pamoja na washindi. 
Mshindi wa kwanza wa tuzo hizo, Gerald Kitabu akitoa shukurani zake. 
Mwanahabari Calvin Gwabara kutoka SUA, akipongezwa na dada yake huku akionesha vyeti vyake.



Na Dotto Mwaibale

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amewataka waandishi wa habari nchini kutumia taaluma zao kuelimisha jamii kuhusu habari za sayansi na teknolojia ili kuleta maendeleo nchini.

Akizungumza wakati wa utoaji tuzo za umahiri katika uandishi wa habari za Sayansi zilizoandaliwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknlojia (COSTECH) kwa kushirikiana na Jukwaa la Bioteknojia (OFAB), Waziri Ndalichako alisema tuzo hizo iwe ni chachu za kuandika habari za sayansi kwa undani ili kuwajengea uelewa wananchi wa.kawaida.

Alisema ufundi wa waandishi katika.kuandika habari za sayansi utasaidia kutangaza ubunifu na kuongeza tija thamani katika teknolojia mbalimbali."Wananchi wanahitaji teknolojia za kisasa katika kurahisisha utendaji kazi hivyo uandishi wenu utasaidia kuinua sekta ya kilimo na mifugo ambayo ndio kundi.muhimu katika jamii hasa katika kuelekea uchumi wa viwanda,"alisema Ndalichako.

Aliwataka Costech na taasisi nyingine kuendelea kushirikiana na wanahabari kuelimisha jamii katika masuala ya sayansi.Ndalichako alipongeza COSTECH na OFAB kwa kuandaa tuzo hizo kwani zitaongeza mori kwa wanahabari wa kuandika habari za sayansi.

Akielezea ushiriki wa.waandishi katika shindano hilo lililoanza Januari hadi Agosti mwaka hii, Mkurugenzi Mkuu wa COTECH, Dk.Hassan Mshinda alisema, shindano hilo hapa nchini sasa ni mara ya tisa kufanyika na kwa upande wa Afrika ni la kumi.

Alisema katika shindano hilo jumla ya makala 200,vipindi vya radio 20 na televisheni 15 vilishindaniwa.Mshindi alisema watalaam waliobobea ambao walifanyakazi ya.kutafuta washindi ambao walipata dola 250, 750, 1,000 na 1,500.Kwa upande wake, Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), Jim Yonaz aliwataka waandishi kuwa daraja kati ya wana sayansi na jamii.

Alisema wana sayansi wana lugha ngumu hivyo kupitia waandishi na aina ya uandishi wao wamesaidia jamii kuelewa habari mbalimbali za sayansi."Katika kuchangia uchumi wa viwanda waandishi wanakazi kubwa kuhakikisha wanatoa elimu ya sayansi na kilimo ili kuelimisha jamii,"alisema Yonaz.

Yonaz pia aliiomba Serikali kuhakikisha inawawezesha waandishi kwa kuwajengea uwezo wa ufahamu ili waweze kuelewa zaidi sababu zinazowafanya kuandika habari mbalimbali.Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Dk.Ayoub Rioba alisema, wana sayansi wana jukumu la kuboresha maisha ya jamii kwa kuhakikisha wanatumia zana zilizoboreshwa kiteknolojia.Alisema kwa sababu ya lugha itumikayo na wana sayansi upo umuhimu wa wanahabari kuandika.habari nyingi za sayansi.

Rioba pia aliitaka taasisi ya Costech pamoja na taasisi nyingine kuendelea kufanya kazi za kuelimisha jamii kwa kushirikiana na wana habari ili kujenga jamii yenye uelewa wa masuala ya sayansi.Miongoni mwa waliopata tuzo za umahiri wa habari za Sayansi ni pamoja na mshindi wa jumla Gerald Kitabu (Guardian), Shedrack Sagati(Habari Leo), Elias Msuya (Mwananchi), Calvin Gwabara, Fatma Abdul (Daily News) na Dino Mugunde.

Wengine ni Lucy Ngowi, Hellen Kwavava, Coleta Makulwa, Daniel Simbei, Benson Eustace na Restuta Damian.