Wednesday, December 09, 2015

Koffi Olomide apagawisha wakazi wa Dar

Mzee wa selfee akicheza pamoja na wanenguaji wake.
IMG_2906Muimbaji wa Koffi Olomide, Cindy akifanya yake.
IMG_2934IMG_3040….Wakilishambulia jukwaa.2…Akipiga Selfee na baadhi ya mashabiki zake walioweza kucheza vizuri staili ya wimbo huo.3Muimbaji wa Muziki wa Dansi Bongo, Christian Bella, akitumbuiza jukwaani.4Msanii wa filamu Bongo, Jacob Steven ‘JB’, akisakata muziki.5Baadhi ya watangazaji wa redio na TV Clouds Media Group wakiwa katika pozi ndani ya Ukumbi huo.6Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (kulia), akifuatilia kwa makini burudani hizo.7Mchezaji wa zamani wa timu ya Coastal Union ya Tanga na Simba, Tippo Athuman (watatu kutoka kushoto), akiwa katika pozi na baadhi ya marafiki zake.8Mkurugenzi wa Mgahawa wa Break Point, Daudi (wa pili kushoto), akiwa kwenye shoo hiyo na baadhi ya marafiki zake.9DJ Ziro (kushoto), akiwa katika pozi na rafiki yake.
10Mtangazaji wa kipindi cha Kambi Popote cha Clouds TV Antony Karugezi akipozi katika shoo hiyo.11Baadhi ya mashabiki waliohudhuria kwenye shoo hiyo.
MWANAMUZIKI kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Koffi Olomide, usiku wa kuamkia leo aliwapagawisha vilivyo mashabiki wake waliohudhuria katika onesho lake liitwalo ‘16 Selfie’ lililofanyika ndani ya Ukumbi wa Escape One Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Katika shoo hiyo iliyokuwa na mashabiki wengi ilitawaliwa na shangwe kutoka kwa wapenzi wa muziki wa Dansi ambao walijitokeza mapema kwa ajili ya kumshuhudia nguli wa muziki huo akifanya makamuzi yake ya kwanza jijini Dar siku chache tu baada ya kuachia albam yake mpya ya Selfie.
Shoo hiyo ilisindikizwa na baadhi ya wanamuziki wa hapa nchini akiwemo Christian Bella na Ruby.
(Habari/Picha: Musa Mateja/GPL)

No comments: