Wednesday, October 23, 2013

Rais Jakaya Kikwewte Atembelea Eneo Lenye Utajiri wa Chuma la Liganga Wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe

  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akionesha kilele cha Central Liganga hill ambacho ni mojawapo ya sehemu ambazo kampuni ya Sichuan Hongda ya China itachimba mashapu ya chuma na kuyafua katika kiwanda kikubwa cha kufua chuma kitachoajiri watu 32, 000 katika eneo hilo lenye utajiri wa chuma la Liganga wilaya ya Ludewa mkoani Njombe jana  Oktoba 22, 2013. Kampuni hiyo.
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo toka kwa Meneja mradi wa Maganga Matatitu Resource Development limited Bw. Lawrence Manyama kuhusu mlima huo uliosheheni mashapu ya chuma alipotembelea eneo lenye utajiri wa chuma la Liganga wilaya ya Ludewa mkoani Njombe jana Oktoba 22, 2013.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na wawekezaji wa kampuni ya Sichuan Hongda ya China ambao ni wawekezaji katika eneo lenye utajiri wa chuma la Liganga wilaya ya Ludewa mkoani Njombe jana Oktoba 22, 2013. Kampuni hiyo inatarajiwa kujenga kiwanda cha kufua chuma mapema mwakani kitachajiri watu 32,000 kitakapokamilika.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wananchi alipoowasili katika uwanja wa mikutano wa Ludewa ambako alihutubia mkutano wa hadhara. PICHA NA IKULU

No comments: