Tuesday, October 15, 2013

MSHINDI WA NYUMBA YA TATU AIRTEL YATOSHA APOKEA CHETI CHA USHINDI

 Meneja Uhusiano wa Airtel, Bw. Jackson Mmbando (katikati) akiongea na wanahabari (hawapo pichani)…
 Meneja Uhusiano wa Airtel, Bw. Jackson Mmbando akimkabidhi cheti mshindi wa tatu wa nyumba ya Airtel Bi. Husnat  John  aliyeibuka mshindi kupitia promosheni ya Airtel inayofahamika kwa jina la Airtel Yatosha, shinda nyumba 3. Kati ni Meneja Uhusiano wa Airtel  Bi, Aneth Muga. Na wa kwanza kushoto ni mtoto wa mshindi huyo Eksher Abby.

 Meneja Uhusiano wa Airtel, Bw. Jackson Mmbando akimkabidhi cheti mshindi wa tatu wa nyumba ya Airtel Bi. Husnat  John  aliyeibuka mshindi kupitia promosheni ya Airtel inayofahamika kwa jina la Airtel Yatosha, shinda nyumba 3. Kati ni Meneja Uhusiano wa Airtel  Bi, Aneth Muga. Na wa kwanza kushoto ni mtoto wa mshindi huyo Eksher Abby.

 Meneja Uhusiano wa Airtel, Bw. Jackson Mmbando (katikati) akiongea na wanahabari (hawapo pichani) kabla ya kumkabidhi cheti mshindi wa tatu wa nyumba ya Airtel Bi. Husnat  John (kushoto) aliyeibuka mshindi kupitia promosheni ya Airtel inayofahamika kwa jina la Airtel Yatosha, shinda nyumba 3. Kulia ni Meneja Uhusiano wa Airtel  Bi, Aneth Muga.



Meneja Masoko wa Airtel, Aneth Muga akizungumza juu ya vifurushi vya Airtel Yatosha Baba Lao iliyoboreshwa ili kumuwezesha mteja wa Airtel kupata dakika 61 kupiga mitandao yote, kutuma ujumbe mfupi wa maneno bila kikomo pamoja na 1.5 GB kwa bei ile ile ya shilingi 999 tu.

 MSHINDI WA NYUMBA YA TATU AIRTEL YATOSHA APOKEA CHETI CHA USHINDI

•    Vifurushi vya yatosha vyaongezwa muda wa kupiga mitandao yote dk 61, 1.5 GB na sms bila kikomo

Dar es Salaam October 15, 2013: Mshindi wa nyumba ya tatu ya Airtel Yatosha, Bi. Husnat Anthony leo amekabidhiwa rasmi cheti chake cha ushindi ikiwa ni uthibitisho maalum  wa ushindi wake.

Mshindi huyo anakuwa ni mshindi wa tatu kuibuka na nyumba kupitia promosheni ya Airtel yatosha shinda nyumba tatu baada ya nyumba ya kwanza na ya pili kuchukuliwa na Sylvanus Juma pamoja na Agnes Lyimo.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhiwa cheti chake, Bi. Husnat alisema “Kweli sikutegemea kama ipo siku naweza nikamiliki nyumba yangu mwenyewe, na hata nilipopigiwa simu sikuamini ila Namshukuru sana Mungu kwa kuniwezesha kuwa mshindi wa nyumba ya Airtel Yatosha”

“Pia nawashukuru sana Airtel kwa zawadi hii na nimeamini kweli Airtel yatosha na inasaidia kupunguza makali ya maisha kwa watanzania,” alisisitiza Bi. Husnat.

Kwa upande wake Meneja Uhusiano wa Airtel, Bw Jackson Mmbando alisema Airtel inayo furaha kumpata mshindi mwingine wa nyumba na haitoacha kutoa huduma bora na zenye manufaa kwa wateja wake nchi nzima na kwa sababu hiyo bado inazidi kuboresha huduma zake na kuzifanya ziwe za kisasa zaidi.

“Airtel hatujaishia tu kwenye utoaji wa nyumba bado tunaendelea kuboresha huduma zetu na kuhakikisha wateja wetu wananufaika zaidi na huduma tunazotoa” Alisema Mmbando.

Airtel imeboresha zaidi huduma zake na sasa hivi ukijiunga na kifurushi cha siku cha 999 unaweza kupata dakika 61, kutuma ujmbe
mfupi wa maneno bila kikomo pamoja na 1.5 GB kwa ajili ya matumizi ya Internet.

Kujiunga na vifurushi mbalimbali vya Airtel mteja anapaswa kupiga *149*99# na kuchagua 1 au 2 kisha aweze kujiunga na kifurushi chochote cha Wiki, Siku au Mwenzi.

Airtel kupitia promosheni ya Airtel yatosha imetoa zawadi ya pesa taslimu shilingi milioni 90 kwa wateja wake na nyumba tatu zenye thamani ya milioni 65 kwa kila moja tayari zilishapata washindi.

No comments: