Thursday, October 31, 2013

BALOZI WA TANZANIA NCHINI DRC ANTHONY CHECHE AONANA NA UONGOZI WA MKOA WA RUKWA KUJADILI MAHUSIANO YA NCHI HIZO MBILI

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akiongoza kikao kati ya balozi wa Tanzania nchini Congo DRC Balozi Anthony Cheche aliyefika ofisini kwake kwa lengo la kujitambulisha na kujadili mambo mbalimbali ya kimahusiano kati ya nchi hizo mbili. Mkuu huyo wa Mkoa alimuomba balozi Cheche kunadi fursa za uwekezaji zinazopatikana Mkoani Rukwa pamoja na kuunganisha nguvu ya nchi hizi mbili katika kuwekeza kwenye usafiri wa majini katika Ziwa Tanganyika. Akizungumzia kuhusu wahamiaji haramu amesema ni bora kujenga ushirikiano mzuri wa kibiashara kwa nchi zote mbili ambapo taratibu maalum zitafuatwa kwa wananchi na wafanyabiashara kuingia na kutoka. 
Balozi Anthony Cheche anayoiwakilisha Tanzania nchini DRC akizungumza Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa leo alipoonana na uongozi wa Mkoa kwa lengo la kujitambulisha na kujadili mambo kadhaa ya mahusiano kati ya Tanzania na Congo DRC. Ameiomba Serikali ya Tanzania kuangalia upya vizuizi vya njiani kwa wafanyabiashara wa nje ikiwemo DRC hususani uwepo wa mizani nyingi barabarani na badala yake ziwepo chache na ziwe mbali kidogo na barabara kuepusha usumbufu kwa wasafiri wengine na wafanyabiashara.
Balozi Anthony Cheche akizungumza katika kikao hicho.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akimuonyesha Balozi cheche toleo maalum katika gazeti la Daily News linaloelezea fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana Mkoani Rukwa kwa ajili ya kuzinadi kwa wawekezaji nchini Congo DRC.
Baadhi ya wakuu wa idara katika Sekretarieti ya Mkoa wa Rukwa wakiteta jambo katika kikao hicho, Kulia ni Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu Ndugu Samson Mashalla, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Idara ya Mipango Ndugu David Kilonzo na Kaimu Katibu Tawala Idar a ya Uchumi na Uwezeshaji Ndugu Respitch Maengo.
Picha ya pamoja.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akiagana na Balozi Anthony Cheche baada kuonana na uongozi wa Mkoa huo mapema leo katika jengo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo. Picha na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa

No comments: