Wednesday, October 30, 2013
DARAJA LA KIKWETE KATIKA MTO MALAGARASI MKOANI KIGOMA LAKAMILIKA
Ujenzi wa Daraja la Kikwete katika mto Malagarasi mkoani Kigoma umekamilika. Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt John Pombe Magufuli akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Kigoma aliweza kutembelea eneo hilo na kujionea magari yakiwa yanapita katika daraja hilo.
Kampuni ya M/S Hanil Engineering and Construction Company Limited kutoka Korea ya Kusini iliingia mkataba na kuanza ujenzi wa daraja hilo mwezi Desemba 2010 na kutakiwa kukamilisha kazi hiyo ifikapo mwezi Desemba 2013. Mradi huo unajumuisha ujenzi wa madaraja matatu yenye jumla ya urefu wa meta 275 pamoja na barabara ya lami yenye urefu wa kilometa 48 kwa gharama ya Dola za Kimarekani milioni 64 ambazo ni sawa na Shilingi bilioni 90 za Kitanzania zilizotolewa na Benki ya Exim ya Korea ya Kusini kwa asilimia 90 na kiasi kilichobaki kikiwa ni fedha za ndani.
Akitoa maelezo ya mradi huo Mhandisi Yu Sing kutoka kampuni ya Hanil Engineering alimfahamisha Waziri Magufuli kuwa, Mradi huo umegawanywa katika sehemu mbili. Sehemu ya kwanza ambayo ndiyo iliyokamilika ni ujenzi wa madaraja matatu yenye urefu wa meta 25, meta 200 na meta 50 pamoja na kilometa 11 za lami. Sehemu ya pili ni ujenzi wa kilometa 37 za lami ambazo ndizo zinazoendelea kukamilishwa kwa sasa.
Sosi: matukio-michuzi: DARAJA LA KIKWETE KATIKA MTO MALAGARASI MKOANI KIGOMA LAKAMILIKA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
WAZIRI NA NAIBU WAZIRI WA ARDHI WASHIRIKI KIKAO CHA KWANZA CHA MKUTANO WA 19 WA BUNGE LA 12 KWA AJILI YA KUJADILI BAJETI YA SERIKALI 2025/2026
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Deogratius Ndejembi (MB), leo tarehe 8 Aprili 2025, ameshiriki kikao cha kwanza cha Mku...
.jpeg)
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
(Picha na Yahya Charahani) Kwa wale waliokulia maeneo haya, hili ni jambo la kawaida ukitoka mjini, shambani sijui hadi wapi kote ni haya h...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
No comments:
Post a Comment