Thursday, October 31, 2013

MKUU WA MKOA WA RUKWA NA WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU (TFS) WATEMBELEA HIFADHI NA MAPOROMOKO YA LUANJI NA KALAMBO FALLS MKOANI RUKWA



Maporomoko ya Mto Kalambo (Kalambo Falls)
Maporomoko ya asili ya Luanji (Luanji Falls) yaliyopo Wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akiwa na baadhi ya wafanyakazi wa Wakala wa Hifadhi ya Misitu Tanzania (TFS) wakizungumza na wanakijiji wa Kapozwa Wilayani Kalambo juu ya umuhimu wa kuhifadhi mazingira yanayowazunguka ukiwemo msitu wa Kalambo na Maporomoko ya Mto Kalambo (Kalambo Falls) yenye urefu wa mita 225.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akiwa na baadhi ya wafanyakazi wa Wakala wa Hifadhi ya Misitu Tanzania (TFS) wakizungumza na wanakijiji wa Kapozwa Wilayani Kalambo juu ya umuhimu wa kuhifadhi mazingira yanayowazunguka ukiwemo msitu wa Kalambo na Maporomoko ya Mto Kalambo (Kalambo Falls) yenye urefu wa mita 225.
Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Moshi Chang'a akionyesha kwa kidole msitu wa hifadhi wa Luanji yanapopatikana maporomoko ya asili ya mto luanji (Luanji Falls). Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa na wengine ni Wakala wa Hifadhi ya Misitu Tanzania walipotembelea hifadhi hiyo kwa ajili kuiendeleza. 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akionyeshwa kushangazwa na staili ya nywele ya mmoja ya watoto wa kijiji cha Kapozwa Wilayani Kalambo alipofika katika kijiji hicho na Wakala wa Hifadhi ya Misitu Tanzania kwa ajili ya kuona hifadhi ya Msitu wa Kalambo na maporomoko ya mto Kalambo (Kalambo Falls). 
Picha ya pamoja kati ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Stella Manyanya katikati waliokaa, Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Salum Chima kushoto waliokaa, watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Rukwa na Wakala wa Hifadhi ya Misitu Tanzania (TFS) ofisini kwa Mkuu huyo wa Mkoa.Picha na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa

No comments: