Friday, October 04, 2013

WATANZANIA KUMIMINIKA KUMSIKILIZA MBUNGE WA IRAMBA MAGHARIBI NA NAIBU KATIBU MKUU WA CCM MWIGULU NCHEMBA JIJI LA LEICESTER UINGEREZA.

Mbunge wa Iramba-Magharibi na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Mwigulu Nchemba.
--- 
Watanzania nchini Uingereza wamejitayarisha kuhudhuria mkutano wa wazi siku ya Jumamosi mchana ili kumsikiliza Mbunge wa Iramba Magharibi Ndugu Mwigulu Nchemba. Huu ni mwendelezo wa ziara alizofanya Ndugu Nchemba na ujumbe wake akitokea Marekani alipopokewa na mamia ya watanzania na makada wa CCM nchini huko.

Aidha katika ziara zake nje ya nchi ndugu Nchemba ameweka bayana msimamo wa CCM na Serikali yake katika hatua za makusudi za kuhakikisha watanzania nje ya nchi wanatambulika katika mipango madhubuti ya kitaifa na kwamba wakati umefika wa rasilimali za wanadiaspora kuanza kutumika kujenga nchi yao bila uwoga.

Uchunguzi wetu umefanya mawasiliano na kubaini kuwa watanzania toka majiji mbalimbali ya hapa Uingereza watasafiri kuhudhuria mkutano huo ili kujua serikali imeandaa mbinu gani mpya za kutatua kero za watanzania wanaoishi diaspora. Mkutano huo ambao utaambana na meza ya vyakula na vinywaji itakayoandikwa na mpishi maarufu wa kitanzania na baadaye kufuatiwa na muziki utafanyika katika ukumbi  maarufu  na wa kisasa wa St. Patrick's 100, Beaumont. Leys Lane. 

Leicester. LE4 2BD.
Na Leyla Shomari,
Tanzania Now:  Freelance Observers: Slough. St.Marys Road. SL3

No comments:

NHC YAKABIDHI MSAADA KWA WATU WENYE ULEMAVU UBUNGO

  Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kupitia kwa Afisa wake Mkuu wa Habari, Yahya Charahani, limekabidhi msaada wa vifaa vya kusaidia watu we...