Saturday, October 19, 2013

JUKWAA LA WAHARIRI LAKABIDHIWA HUNDI YENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 12 KUTOKA VODACOM



Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Umma na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Joseline Kamuhanda, akiongea na waandishi wa Habari(hawapo pichani)wakati wa kukabidhi hundi yenye thamani ya Shilingi Milioni kumi na mbili, itakayotumika kwa ajili ya mkutano mkuu wa mwaka wa wahariri wa vyombo vya habari utakaofanyika Iringa hivi karibuni, wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Mkuu wa kitengo cha mfuko wa kusaidia jamii wa Vodacom Tanzania (Vodacom Foundation) Bw.Yessaya Mwakifulefule na Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri nchini Bw. Absalom Kibanda.

Mwenyekiti wa jukwaa la wahariri nchini, Bw.Absalom Kibanda (kushoto)akikabidhiwa hundi yenye thamani ya Shilingi Milioni kumi na mbili na Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Umma na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Joseline Kamuhanda, kwa ajili ya mkutano mkuu wa mwaka wa vyombo vya habari utakaofanyika Iringa hivi karibuni Anaeshuhudia katikati ni Katibu Mkuu wa jukwaa hilo Bw. Neville Meena.

No comments:

MAMA NEEMA MWIGULU AHIMIZA TAASISI KUUNGA MKONO JUHUDI ZA SERIKALI KUPITIA UWAJIBIKAJI KWA JAMII

Mwenza wa Waziri Mkuu, Mama Neema Mwigulu Nchemba, amehimiza taasisi za umma na binafsi kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kub...