Monday, October 28, 2013

JAMAL MALINZI ASHINDA URAIS (TFF) KWA KISHINDO KIKUU, WALLACE KARIA MAKAMU WAKE


1Leodger Tenga Rais wa Shirikisho la Mpira wa miguu aliyemaliza muda wake akimkabidhi Mpira Jamal Malinzi Rais Mpya w
a shirikisho hilo mara  baada ya kumshinda mpinzani wake aliyekuwa makamu wa Kwanza wa shirikisho hilo Bw. Athman Nyamlani kwa kura 73 kwenye uchaguzi ulifanyika katika ukumbi wa Water Front jijini Dar es salaam na kumalizika usiku huu, Katika uchaguzi huo Mgombea wa umakamu wa wa rais Walace Karia amefanikiwa kuwashinda wapinzania wake Imani Madega na Ramadhan Nassib. PICHA NA KUKOSI KAZI CHA FULLSHANGWE WATER FRONT DAR ES SALAAM1aJamal Malinzi Rais Mpya wa shirikisho la mpira wa miguu nchini Tanzania  TFF akizungumza na wajumbe wa kamati ya utendaji mara baada ya kutangazwa mshindi katika uchaguzi huo usiku huu , kulia ni Wallace Karia Makamu wa Rais wa TFF2Leodger Tenga Rais wa Shirikisho la Mpira wa miguu aliyemaliza muda wake akizungumza na kumpongeza Jamal Malinzi Rais Mpya wa shirikisho3Baadhi ya wafuasi wa Rais Mpya wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF Bw. Jamal Malinzi wakishangilia na kupongezana mara baada ya kusikia matokeo ya uchaguzi huo yakionyesha Jamal Malinzi ameshinda.4Baadhi ya wafuasi wa Rais Mpya wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF Bw. Jamal Malinzi wakishangilia na kupongezana mara baada ya kusikia matokeo ya uchaguzi huo yakionyesha Jamal Malinzi ameshinda.5Mmoja wa wajumbe wa kamati ya utendaji Bw. Mvela kutoka Iringa hali ilibadilika kutokana na furaha jambo lililopelekea kupata mshtuko hapa akisaidiwa kutolewa nje ya ukumbi na wajumbe wenzake.6Kutoka kulia ni Leodger Tenga Rais wa TFF aliyemaliza muda wake mwakilishi wa FIFA Ashford Mamelodi na Henry Tandau wakiwa katika chumba cha uchaguzi huo.7Jamal Malinzi Rais Mpya wa shirikisho la mpira wa miguu nchini Tanzania  TFF akimpongeza makamu wake wa Rais Bw. Wallace Karia mara baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo.8Leodger Tenga Rais wa Shirikisho la Mpira wa miguu aliyemaliza muda wake akimpongeza  Jamal Malinzi Rais Mpya w
a shirikisho hilo mara  baada ya kumshinda hapa siyo kwamba walikuwa wanalia bali walikuwa wakipongezana mara baada ya kazi kubwa ya kusaka ushindi.

No comments: