Friday, July 01, 2016

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA AIRTEL TANZANIA

Kufuatia kutimiza agizo la uzimaji wa simu bandia, kutokana na agizo elekezi la Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA.

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel inapenda kuwajulisha wateja wake walio nunua simu orijino kutoka kwa watoa huduma ndani ya maduka yetu ya Airtel, endapo baadhi ya wateja simu zao zitazima kutokana na agizo hilo. 

Airtel inawatangazia wateja wote watakaoathirika na zoezi hili kutembelea maduka yetu nchi nzima kwaajili ya kuhudumiwa/kurekebishiwa simu zao wakiwa na simu husika pamoja na risiti za manunuzi ya simu hizo.

Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza kutokana na zoezi hili.

Imetolewa na Idara ya mawasiliano 
Airtel Tanzania

No comments:

RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA UJUMBE WA JUKWAA LA MABUNGE LA NCHI ZA MAZIWA MAKUU (FP-ICGLR) IKULU NDOGO TUNGUU, ZANZIBAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Kiongozi wa Jukwaa la Mabunge la...