Sunday, July 10, 2016

TAARIFA YA MSIBA WA DADA ELIZABETH MAYEMBA


Uongozi wa Kampuni ya Business Times Limited (BTL), inayozalisha Magazeti ya Business Times, Majira na Spoti Starehe, inasikitika kutangaza kifo cha mfanyakazi wake Elizabeth Mayemba.

Elizabeth Mayemba ambaye ni Kaimu Mhariri wa Michezo Gazeti la Majira alikutwa na mauti Jumamosi ya Julai 9, 2016 saa 2 usiku, akiwa nyumbani kwake Tabata Kisukulu, Dar es Salaam.

Kabla ya kukutwa na mauti, marehemu alifanya kazi zake na majukumu yote ya kila siku bila kuonesha dalili za kuumwa.Akiwa nyumbani kwake saa 2 usiku, alijisikia vibaya na kukimbizwa hospitali ya Amana, akiwa njiani alikutwa na mauti.

Kwa mujibu wa familia ya marehemu, Elizabeth Mayemba atazikwa siku ya Jumanne ya Julai 12, 2016, mkoani Morogoro kwenye Makaburi ya Kola.

Elizabeth Mayemba ataagwa Jumatatu ya Julai 11, 2016 saa 5.00 asubuhi nyumbani kwake Tabata Kisukulu. Baada ya Misa mwili utasifirishwa kwenda Morogoro kwa mazishi.

Taarifa zaidi zitaendelea kutolewa kila mara ili kuwapa nafasi watu wengi wajue ratiba zote zilivyopangwa.

Kampuni imepata pigo kubwa kwa kuondokewa na Elizabeth Mayemba, ambaye mchango wake ulikuwa mkubwa zaidi na ulioonekana kwa kila mtu. Marehemu ameacha mume na watoto watatu wa kiume.

Mungu Ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi. Amina

Meneja Mkuu
Business Times Limited

No comments: