Wednesday, July 06, 2016

MKURUGENZI WA NHC BW. NEHEMIA MCHECHU AZUNGUMZIA MIRADI YA SHIRIKA HILO KATIKA MAONYESHO YA SABASABA


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akizungumza na waandishi wa habari wakati wa maonyesho ya TANTRADE Sabasaba yanayoendelea katika viwanja hivyo vilivyopo barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam ambapo ameelezea uendelezaji na uuzaji wa nyumba katika maeneo mbalimbali unaoendelea katika miradi yao iliyopo nchi nzima.Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu  akifafanua jambo kuhusu mipango ya shirika hilo wakati akizungumza na wanahabari katika banda la maonyesho ya Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya TANTRADE barabara ya Kilwa.
Clara Lumbanga Ofisa Maendeleo ya Biashara NHC akimuangalia mmoja wa wananchi waliotembelea katika banda hilo wakati alipokuwa akisaini kitabu cha wageni.

Clara Lumbanga Ofisa Maendeleo ya Biashara NHC akimuangalia mmoja wa wananchi waliotembelea katika banda hilo wakati alipokuwa akisaini kitabu cha wageni.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akifurahia jambo na baadhi ya wateja waliotembelea katika banda hilo.
Clara Lumbanga Ofisa Maendeleo ya Biashara NHC akitoa maelezo kwa wananchi mbalimbali waliotembelea katika banda la Shirika la Nyumba la Taifa NHC.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu  akizungumza moja kwa moja na  wageni mbalimbali waliofika katika banda hilo ili kujionea shughuli mbalimbali za shirika hilo.
Afisa Mauzo Mwandamizi wa Shirika la Nyumba la  Taifa,  Joseph Haule akizungumza na Mkurugenzi wa Blogu ya Fullshangweblog Bw. John Bukuku wakati alipotembelea katika banda la NHC.

Wafanyakazi wa shirika la NHC wanaoshiriki katika maonyesho ya TANTRADE yanayofanyika kwenye uwanja wa Sabasaba jijini Dar es salaam katika barabara ya Kilwa wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu.

No comments: