Friday, July 22, 2016

ZIARA YA RAIS WA BENKI YA EXIM KWENYE KITUO CHA KUHIFADHIA KUMBUKUMBU.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa kwanza kulia) akizungumza kumshukuru Rais wa Benki ya Exim ya nchini China Bw, Liu Lian’ge (hayupo pichani) mara baada ya kukagua kituo mahiri cha kutunza kumbukumbu (Internet Data centre) kilichopo eneo la kijitonyama Dsm.


Rais wa Benki ya Exim ya nchini China Bw, Liu Lian’ge (wa kwanza kushoto) akizungumza mara baada ya kukagua kituo mahiri cha kuhifadhia kumbukumbu ambacho kilijengwa kwa ufadhili wa Benki ya Exim ya nchini china. 
Rais wa Banki ya Exim ya nchini China Bw, Liu Lian’ge (wa pili kutoka kulia) akizungumza na Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa kwanza kulia) wakati wakikagua kituo mahiri cha kuhifadhi kumbukumbu (Internet Data centre) kilichopo eneo la kijitonyama Dsm. 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa kwanza kushoto) akishuka ngazi wakati wa kukagua kituo mahiri cha kutunzia kumbukumbu (Internet Data centre) kilichopo eneo la kijitonyama, (wa kwanza kulia) ni Rais wa Benki ya Exim ya nchini China Bw. Liu Lian’ge.

No comments: