Friday, July 22, 2016

TANZANIA NA CHINA ZATILIANA SAINI HATI YA MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO (MOU) UJENZI WA RELI YA KATI KWA KIWANGO CHA KIMATAIFA

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile (aliyeipa mgongo kamera), akizungumza jambo kabla ya kutia saini Hati ya makubaliano ya ushirikiano wa ujenzi wa miradi mbalimbali ukiwemo ujenzi wa Reli ya Kati katika kiwango cha Kimataifa (Standard gauge) na Benki ya Exim ya China, Jijini Dar es salaam.
FED2Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile (Kulia) akiteta jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dkt. Leonard Chamuriho (katikati) kabla ya kutia saini Hati ya makubaliano ya ushirikiano wa ujenzi wa miradi mbalimbali ukiwemo ujenzi wa Reli ya Kati katika kiwango cha Kimataifa (Standard gauge) na Benki ya Exim ya China, Jijini Dar es salaam Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James.
FED3Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile (Kushoto) akitoa maelezo kwa mmoja wa maafisa wa Benki ya Exim-China,  kabla ya kutia saini Hati ya makubaliano ya ushirikiano wa ujenzi wa miradi mbalimbali ukiwemo ujenzi wa Reli ya Kati katika kiwango cha Kimataifa (Standard gauge), na Benki ya Exim ya China, Jijini Dar es salaam.
FED4Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile na Naibu Meneja Mkuu (Mikopo Nafuu) wa Benki ya Exim ya China, Zhu Ying, wakitia saini Hati ya Makubaliano ya  Ushirikiano wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ukiwemo ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (Standard gauge), Jijini Dar es salaam.
FED5Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius Likwelile akipeana mkono na Naibu Meneja Mkuu (Mikopo Nafuu) wa Benki ya Exim ya China, Zhu Ying, mara baada ya kutia saini Hati ya Makubaliano ya  Ushirikiano wa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ukiwemo ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (Standard gauge), Jijini Dar es salaam.
FED6Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip I. Mpango (Mb) (kushoto), akizungumza na Rais wa Benki ya Exim-China, Liu Liange, katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa JK Nyerere jijini Dar es salaam kabla ya Rais huyo aliyekuwepo nchini kwa ziara ya kikazi kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli. Kulia ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa.
FED7Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip I. Mpango (Mb) (kulia), akipeana mkono na  Rais wa Benki ya Exim-China, Liu Liange, katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa JK Nyerere jijini Dar es salaam kabla ya Rais huyo aliyekuwepo nchini kwa ziara ya kikazi kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, kuondoka nchini.
FED8Rais wa Benki ya Exim kutoka China, Liu Liange (kulia) akiwa katika Uwanja wa ndege wa  Kimataifa  wa JK Nyerere, muda mfupi kabla ya kuondoka nchini kurejea China baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi nchini ambapo Benki yake imeahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania kutekeleza Miradi Kadhaa ya Maendeleo ukiwemo ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha kimataifa (Standard gauge)
FED9Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip I. Mpango (Mb) (kulia), akiagana na  Rais wa Benki ya Exim-China, Liu Liange, katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa JK Nyerere jijini Dar es salaam kabla ya Rais huyo aliyekuwepo nchini kwa ziara ya kikazi kwa mawaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli. 

No comments: