Friday, July 22, 2016

DK. TULIA AKSON AONGOZA MBIO ZA KILOMITA 5 MJINI DODOMA

TU1
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Tulia Akson akiongoza Mbio za Tulia Marathon KM 5 zilizofanyika leo asubuhi kuanzia Bungeni Mpaka Nyerere Square zikishirikishwa wabunge mbalimbali wakuu wa wilaya na vijana kama juhudi za kuunga mkono Juhudi za Rais John Pombe Magufuli katika kuwaletea wananchi maendeleo nchini kushoto ni Anthony Mtaka Rais wa Chama cha Riadha Nchini RT.
Baada ya mbio hizo walikwenda kutoa msaada wa vitu mbalimbali katika kituo cha Watoto Yatima kiitwacho kijiji cha Matumaini kilichopo nje kidogo ya mji wa Dodoma.Wakati wa kutoa msaada huo Dkt Tulia alisema kuwa ni vvema kila Mkoa ukawa na vikundi mbalimbali kikiwemo cha Wazalendo wakafanya shughuli za Kijamii kusaidia makundi mbalimbali
TU3Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Tulia Akson akiwa na Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde Rais wa Chama Cha Riadha Tanzania RT Bw. Anthony Mtaka , Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Mbeya Mary Majelwa wakishiriki katika mbio hizo leo asubuhi.
TU4Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Tulia Akson akipiga makofi kama ishara ya kushukuru mara baada ya kufika mwisho wa mbio hizo zilizoishia Nyerere Square , kushoto ni Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde.
TU5
Vijana wakipasha mara baada ya kufika kwenye viwanja vya Nyerere Squre.
TU6Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda kulia na Mbunge wa jimbo la Chalinze wa pili kushoto wakishiriki katika mbio hizo pamoja na vijana mbalimbali .

No comments: