



……………………………………………………………………………………………………….
Waziri waNchi, OfisiyaRais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. AngellahKairuki (Mb) amewataka Watendaji wa Taasisi za Serikali kusimamia suala zima la watumishi na wadau kupata mrejesho wa barua wanazozituma kwenye taasisi zao.
Mhe. Kairuki ameyasema hayo leo wakati wa kikao kazi na watumishi wa mkoa wa Morogoro kilichofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Morogoro.
Mhe. Kairuki amesema kumekuwa na malalamiko mengi sana ya watumishi na wadau kutopata mrejesho wa barua wanazozituma kwenye taasisi za Serikali na hata wakijibiwa sio kwa wakati.
“Tunataka barua zijibiwe mara tu mzipatapo, hata kukiri kupokea pia ni mrejesho hivyo ni vema tukajibu barua na kwa wakati”Mhe. Kairuki alisisitiza.
Aidha, Mhe. Kairuki amewaagiza Watendaji hao kufanya ufuatiliaji wa mara kwa mara kwenye masija la za ofisi zao ili kuboresha utoaji huduma kwa umma.
Amesema eneo la ofisi za Masijala limekuwa likilalamikiwa kwa kiasi kikubwa kwa majalada kutoonekana na kusababisha watumishi na wadau kutopata mrejesho.
“Tutoe mwongozo kwa watumishi wa Masijala na tusiwaache bila kuwafuatilia kwani eneo hili limekuwa likilalamikiwa sana. Ikiwezekana tufanye kaguzi za kushtukiza ili kuleta ufanisi katika kazi” Mhe. Kairuki aliongeza.
Ameongeza kuwa ufuatiliaji pia ufanyike kwa kila Ofisa ambaye anakaa na jalada kwa muda mrefu bila kutoa mrejesho.
Mhe. Kairuki amekutana na watumishi wa Mkoa wa Morogoro ikiwa ni mwendelezo wa ziara alizozipanga kuzitekeleza mikoani kwal engo la kusikiliza kero za watumishi ili kuweza kuzitafutia ufumbuzi na kuangalia ni namna gani ya kuweza kuboresha utendaji kazi Serikalini.
No comments:
Post a Comment