Friday, July 22, 2016

JK NA UJUMBE WAKE WAKAGUA UKUMBI UTAKAOTUMIKA WAKATI WA MKUTANO MKUU MAALUM WA CCM MJINI DODOMA


Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Dkt Jakaya Kikwete akiwa sambamba na Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye wakipita kukagua ndani ya ukumbi wa mikutano wa CCM, Dodoma Conversion Center uliopo nje kidogo ya mji wa Dodoma leo, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCM utakaofanyika Julai 23, 2016. 
Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Dkt Jakaya Kikwete akiwa sambamba na Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi (kushoto) na wajumbe wengine wakipita kukagua ukumbi wa mikutano wa CCM, Dodoma Conversion Center uliopo nje kidogo ya mji wa Dodoma, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCM utakaofanyika Julai 23, 2016.
Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Dkt Jakaya Kikwete akifafanua jambo kwa Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi walipokuwa wakipita kukagua ukumbi wa mikutano wa CCM, Dodoma Conversion Center uliopo nje kidogo ya mji wa Dodoma, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCM utakaofanyika Julai 23, 2016.
Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM Dkt Jakaya Kikwete akitoa ufafanua wa jambo kwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi,anaefuta ni Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana
Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana akimuonesha Mwenyekiti wa CCM Dkt Jakaya Kikwete moja ya alama ya wajumbe watakaokuwa wamefika kutoka mikoa mbalimbali. 


Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Dkt Jakaya Kikwete akiwa sambamba na Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rajab Luhwavi wakiwasili kwenye ukumbi wa mikutano wa CCM, Dodoma Conversion Center uliopo nje kidogo ya mji wa Dodoma kuukagua leo Julai 21, 2016, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCM utakaofanyika Julai 23, 2016.

Baadhi ya Vyombo vya habari pia vitarusha matangazo ya moja kwa moja,likiwemo shirika la Utangazaji Taifa TBC,Azam TV kama ambavyo magari yake yaonekanavyo katika viunga vya ukumbi huo tayari kwa kwenda Live siku ya mkutano huo.PICHA NA MICHUZI JR-DODOMA.

No comments: