Wednesday, July 06, 2016

NORWAY YATOA MSAADA KUSAIDIA WAHITIMU WAHANDISI WANAWAKE KUJIENDELEZA


Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), Mhandisi Profesa. Ninatubu Lema na Balozi wa Norway hapa nchini Mhe. Hanne – Marie Kaarstad wakitia saini makubaliano ya msaada wa Dola za Kimarekani milioni 2 kwa ajili ya kuwawezesha wahitimu wa Kike wa masomo ya Uhandisi nchini kujiendeleza kwa kupata uzoefu na kusajiliwa kuwa Wahandisi kamili. Programu inayoanza 2016 – 2021. Wanaoshuhudia utiwaji wa saini ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Edwin Ngonyani (nyuma kushoto).

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Edwin Ngonyani akizungumza wakati wa hafla fupi ya Kutiliana saini baina ya Bodi ya Usajili wa Waandisi (ERB) na Serikali ya Norway kuhusu msaada wa kuwawezesha wahitimu wa Kike wa masomo ya Uhandisi nchini ili waweze kujiendeleza kwa kupata uzoefu na kusajiliwa kuwa Wahandisi kamili leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Balozi wa Norway hapa nchini Mhe. Hanne – Marie Kaarstad na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Mhandisi Profesa. Ninatubu Lema.
Mwenyekiti wa Bodi hiyo Mhandisi Profesa. Ninatubu Lema(katikati) akizungumza wakati wa hafla fupi ya Kutiliana saini baina ya Bodi ya Usajili wa Waandisi (ERB) na Serikali ya Norway kuhusu msaada wa kuwawezesha wahitimu wa Kike wa masomo ya Uhandisi nchini ili waweze kujiendeleza kwa kupata uzoefu na kusajiliwa kuwa waandisi kamili leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Edwin Ngonyani na kushoto ni Balozi wa Norway hapa nchini Mhe. Hanne – Marie Kaarstad
Msajili wa Bodi ya Usajili wa Waandisi (ERB) Mhandisi Steven Mlote akifafanua jambo wakati hafla fupi ya Kutiliana saini baina ya Bodi ya Usajili wa Waandisi (ERB) na Serikali ya Norway kuhusu msaada wa kuwawezesha wahitimu wa Kike wa masomo ya Uhandisi nchini ili waweze kujiendeleza kwa kupata uzoefu na kusajiliwa kuwa waandisi kamili leo Jijini Dar es Salaam.
Msajili wa Bodi ya Usajili wa Waandisi (ERB) Mhandisi Steven Mlote akiwatambulisha baadhi ya wanawake wahitimu wa Vyuo Vikuu katika fani ya Uhandisi (waliosimama kulia) watakao nufaika na msaada wa kuwawezesha wahitimu wa Kike wa masomo ya Uhandisi nchini ili waweze kujiendeleza kwa kupata uzoefu na kuwawezesha kusajiliwa kuwa Wahandisi kamili leo Jijini Dar es Salaam.

No comments: