Wednesday, July 06, 2016

WAZIRI JANUARY MAKAMBA ASHIRIKI SWALA YA EID EL FITRI JIJINI TANGA

 
Waziri wa Nnchi ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano, mazingira) Mh.January Makamba  (wanne kushoto) akishiriki swala ya Eidd na Waumini wengine wa Dini ya Kiislam waliojumuika kwenye msikiti wa Ijuma mjini Tanga,ikiwa ni kusherehekea kumalizika kwa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.

Waumini wa dini ya Kiislam wakiwa katika swala ya Eid El Fitr iliyoswaliwa kwenye msikiti wa Ijumaa,mjini Tanga leo, ikiwa ni kusherehekea kumalizika kwa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan. 
Mh.January Makamba akisilisikiliza Mawaidha mara baada ya Swala

Mh.January Makamba Akepeana mkono wa Iddi na Baadhi ya Wauumini waliokuwepo msikiti baada ya Ibada.
Mh.January Makamba Akipiga picha ya ukumbusho baada ya swala ya Eid El Fitr iliyoswaliwa kwenye msikiti wa Ijumaa,mjini Tanga leo, ikiwa ni kusherehekea kumalizika kwa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.

No comments:

RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA UJUMBE WA JUKWAA LA MABUNGE LA NCHI ZA MAZIWA MAKUU (FP-ICGLR) IKULU NDOGO TUNGUU, ZANZIBAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Kiongozi wa Jukwaa la Mabunge la...