Friday, July 22, 2016

DKT JAKAYA AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU MJINI DODOMA LEO

Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete akifungua Mkutano wa Kamati Kuu ya CCM kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma Julai 21, 2016. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mtarajiwa, Rais John Magufuli, Wapili kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM , Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein, kuliani ni Makamu Mwenyekiti wa CCM , Bara, Philip Mangula na wapili kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana. 
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akimkaribisha Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete kwa ajili ya kufungua Mkutano wa Kamati Kuu ya CCM kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma Julai 21, 2016 pamoja na wajumbe wa mkutano huo. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mtarajiwa, Rais Dkt John Magufuli, Wapili kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM , Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein, kuliani ni Makamu Mwenyekiti wa CCM , Bara, Philip Mangula na wapili kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana. Kamati kuu hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya kupendekeza jina la Dkt John Pombe Magufuli kuwa Mwenyekiti na baadae kuliwasilisha jina hilo kwenye Halmashauri kuu ya Taifa kwa ajili ya kupeleka kwenye mkutano unaotarajiwa kufanyika Julai 23,2016.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo kabla ya kuanza kwa kikao chao kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akimkaribisha Mwenyekiti wa CCM Dkt Jakaya Kikwete
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akimpokea Makamu Mwenyekiti wa CCM , Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein pamoja na Mwenyekiti mtarajiwa,Rais Dkt Jonh Magufuli nje ya ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma Julai 21, 2016.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana kabla ya kuanza kwa kikao chao kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma Julai 21, 2016.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akimpokea Mwenyekiti Mtarajiwa wa CCM,Rais Dkt John Pombe Magufuli walipokuwa wakiwasili kwenye ukumbi wa Sekretarieti, katika jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma, leo.Kamati kuu hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya kupendekeza jina la Dkt Magufuli kuwa Mwenyekiti na baadae kuliwasilisha jina hilo kwenye Halmashauri kuu ya Taifa kwa ajili ya kupeleka kwenye mkutano.
Mwenyekiti Mtarajiwa Dkt John Pombe Magufuli akiwasalimia baadhi ya wanachama na wafuasi wa chama cha CCM nje ya ukumbi wa ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma Julai 21, 2016. 

No comments: