Sunday, July 03, 2016

KAPUMZIKE KWA AMANI MPIGANAJI MWENZETU OMAR MASOUD

Sehemu ya Waombolezaji waliojitokeza kumsindikiza Mpiganaji mwenzetu aliekuwa Mpiga picha wa Kampuni ya Azam Tv, Marehemu Omar Masoud aliefariki Dunia jana kwa ajali ya pikipiki aliyoipata eneo la Makongo Jijini Dar es salaam wakati akielekea kazini. Mazishi yamefanyika mchana huu kwenye Makaburi ya Boko, jijini Dar.
Marehemu Omar Masoud enzi za uhai wake.
Ibada ya mazishi ya ndugu yetu Omar Masoud ikiendelea kwenye Makaburi ya Boko, Jijini Dar es salaam mchana huu.
Waombolezaji.
Waumini wa Kiislam wakiuswalia Mwili wa Marehemu kabla ya kwenda kuuhifadhi kwenye nyumba yake ya Milele kwenye Makaburi ya Boko, Jijini Dar es salaam.

Innalilahi wa inna ilaihi rajiun

No comments: