Wednesday, July 20, 2016

NSSF YACHANGIA MILIONI 50 HARAMBEE YA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI LINDI

Meneja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mkoa wa Lindi, Bi Nour Aziz (kulia) akiwasilisha ahadi ya shirika hilo ya kuchangia milion 50 katika harambee hiyo iliyoongozwa na Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa, mwishoni mwa wiki.
Meneja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mkoa wa Lindi, Bi Nour Aziz akipeana mkono na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimshukuru Mkuu wa Kitengo cha Mafao NSSF, Bw Juma Namuna, baada ya shirika hilo kuahidi kuchangia Milioni 50.
Waziri Mkuu akisalimiana na Mkuu wa Idara ya Uhasibu NSSF mkoa wa Lindi, Jumbe Dona.
Meneja wa NSSF Mkoa wa Lindi, Bi Nour Aziz akisalimiana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Lindi wakati wa Harambee.
Baadhi ya wafanyakazi wa NSSF-Lindi wakisalimiana ba Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
Wafanyakazi wa NSSF Lindi wakiwa na nyuso za furaha baada ya kusalimiana na Waziri Mkuu.
  Wafanyakazi wa NSSF Lindi wakiongozwa na Meneja wa Mkoa wakiwa katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Lindi kwa ajili
ya Harambee Hiyo iliyoendeshwa na Waziri Mkuu.
Baadhi ya wafanyakazi wa NSSF wakiwa katika harambee hiyo.
Mke wa Waziri Mkuu (kushoto) akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendegu.
Mama Salma Kikwete akiwa katika harambee hiyo.
Mke wa Rais mstaafu wa awamu ya nne, Mama Salma Kikwete akiwasilisha mchango wake katika Harambee hiyo huku Taasisi ya WAMA ikitoa ahadi ya kuchangia vitabu vya Shule hiyo.

Shirika la Hifadhi ya Taifa ya Jamii NSSF Makao Makuu ikishirikiana na Ofisi ya Mkoa wa Lindi Imechanga Jumla ya Shilingi
Milioni 50 Kwa Ajili ya Kuchangia Harambee ya Kusaidia Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Lindi iliyoungua Moto Wiki iliyopita.
Kwa Kutambua Umuhimu wa Elimu kwa Watoto Shirika Hilo Kupitia Mkurugenzi Mkuu Wake ,Aliewakilishwa na
Meneja wa Mkoa Bi Nour Aziz Limetoa ahadi hiyo kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Majaliwa Kasim Majaliwa Alieongoza Harambee Hiyo Ambayo Ilihudhuriwa na Wadau Mbali mbali Akiwemo Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya
Nne,Mama Salma Kikwete Katika Harambee Hiyo Jumla ya Shilingi Milioni 80 Taslimu zilichangwa Huku Ahadi na Vifaa vya Ujenzi zikifikia Shilingi Milioni 640 Ambapo Katika Ujenzi Mpya Waziri Mkuu Ameagiza Kujengwa
Jengo la Ghorofa litakalokuwa na Ofisi na  Madarasa.
Katika Tukio Hilo la Moto,Jumla Ya Madarasa 9 na viti na Meza zaidi ya 300,Ofisi 4 na Vyoo Matundu 24
Viliteketea na Moto Uliotokana na hitilafu ya Umeme.
(Picha na Abdulaziz Video, Lindi) 

No comments: