Wednesday, September 09, 2015

TANZANIA YAHIMIZA USHIRIKIANO KATIKA KUWASAIDIA WAKIMBIZI

 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon,  akizungumza wakati wa  Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu dhana ya wajibu wa kuwalinda raia, ambapo alisema licha ya kuasisiwa kwa dhana hiyo dunia bado imeendelea kushuhudia  maisha ya watu wasiokuwa na hatia yakiendelea kupotea  kwa sababu tu Jumuiya ya Kimataifa inashindwa kutumiza wajibu wake kwa wakati.
 Balozi Tuvako Manongi akizungumza wakati wa Majadiliano ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu  dhana ya kuwalinda raia (R2P) majadiliano yaliyojielekeza katika kutathimini mafanikio na changamoto za utekelezi wa dhana hiyo ikiwa ni miaka kumi tangu kuasisiwa  kwake.
 Picha hii  ya maktaba ni ya  wakimbizi  katika kambi moja nchini Tanzania,  ambao jana  jumanne akizungumza katika Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,  Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika UN Balozi Tuvako Manongi amesema kutoka na wimbi kubwa linaloendelea la wakimbizi  kukimbilia mataifa mengine kutafuta usalama wao. Jumuiya ya kimataifa haina budi kushirikiana na bila  kubagua katika  kuwalinda na  utoaji wa huduma na misaada ya kibinadamu kwa wakimbizi.

Na Mwandishi Maalum,  New York
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  imetoa wito kwa   Jumuiya ya Kimataifa wa kushirikiana katika  wajibu wa kuwalinda na kuwapatia misaada ya kibinadamu, wakimbizi wanaokimbia machafuko, vita na  migogoro katika nchi zao.
Wito huo  umetolewa   siku  ya jumanne na Balozi Tuvako Manongi,Mwakilishi wa Kudumu  wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,   wakati  Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,  lilipokutana  kwa majadiliano  ya  siku moja kuhusu utekelezaji wa dhana juu ya wajibu wa kulinda raia (R2P) mafanikio na changamoto zake.

Dhana  ya wajibu wa kuwalinda raia  dhidi ya  mauaji ya kimbari, uhalifu wa kivita,  mauaji ya kikabila na uhalifu dhidi ya  binadamu   ilianzishwa mwaka 2005 wakati  wa mkutano wa Kimataifa  uliofanyika mwaka huu, ambapo viongozi wakuu  wa  nchi na serikali walikubaliana kwamba wajibu wa kwanza wa kuwalinda raia  dhidi ya udhalimu wa aina yoyote ile ni wa serikali yenyewe husika.


No comments: