Monday, September 21, 2015

MAKAMU WA MHE. DKT. MOHAMMED GHARIB BILAL AHUDHURIA KUWEKWA WAKFU ASKOFU KENEN PANJA MBEYA JANA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Abass Kandoro wakati alipowasili kwenye Uwanja wa ndege wa Songwe mkoani humo jana  Sept 20,2015 kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya kuwekwa wakfu Askofu mteule  wa Kanisa la Morovian Tanzania Jimbo la kusini Mchungaji Kenan Salim Pannja zilizofanyika katika Uwanja wa michezo Tukuyu  Mkoani Mbeya.
 Wasanii wa kwaya ya Kanisa la Morovian Tanzania Jimbo kuu la kusini wakitoa burudani wakati wa sherehe ya kuwekwa wakfu Askofu Kenen Salim Panja iliyofanyika jana  Sept 20,2015 katika Uwanja wa michezo Tukuyu  Mkoani Mbeya.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akisalimiana na kumpongeza Askofu mteule wa Kanisa la Morovian Tanzania Jimbo la kusini Mchungaji Kenan Salim  Panja wakati wa sherehe ya kuwekwa wakfu iliyofanyika jana  Sept 20,2015 katika Uwanja wa michezo Tukuyu Mkoani Mbeya.

No comments: