Wednesday, September 23, 2015

MFUMO MPYA WA USAJILI NA UHIFADHI WA TAKWIMU ZA MATUKIO MUHIMU YA BINADAMU KUANZISHWA TANZANIA BARA

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Maimuna Tarishi akitoa hatuba ya ufunguzi rasmi wa kikao cha wadau wa Usajili na Utunzanji wa Takwimu za Matukio Muhimu ya Binadamu nchini kilichofanyika katika ukumbi wa hoteli ya New Africa, Dar es Salaam.
 Mtakwimu Mkuu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Emilian Karugendo, akifafanua jambo wakati wa uwasilishaji wa mada iliyohusiana na hatua za kuandaa Mkakati wa Usajili na Uhifadhi wa Takwimu za Matukio Muhimu ya Binadamu wakati wa kikao cha wadau kilichofanyika katika ukumbi wa hoteli ya New Africa, Dar es Salaam.
 Meneja wa Usajili kutoka RITA Angela Anatory akiwasilisha rasimu ya Mkakati wa Usajili na Uhifadhi wa Takwimu za Matukio Muhimu ya Binadamu katika kikao cha wadau kilichofanyika katika ukumbi wa hoteli ya New Africa, Dar es Salaam.
 Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Maimuna Tarishi (katikati) akifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na mmoja wa watoa mada wakati wa kikao cha wadau wa Usajili na Uhifadhi wa Takwimu za Matukio Muhimu ya Binadamu kilichofanyika katika hoteli ya New Africa, Dar es Salaam. Kushoto kwake ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa RITA, Emmy Hudson na kulia kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa.


No comments: