Thursday, September 24, 2015

KAMATI YA KAMPENI YA MGOMBEA URAIS WA CCM DKT MAGUFULI YASHEREHEKEA SIKUKUU YA EID EL HAJJ MKOANI GEITA LEO


 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania na Mjumbe wa Kamati  Kuu ya CCM,Ndugu Abdallah Bulembo ambaye pia ni Kiongozi wa msafara wa kampeni za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM,akiwaongoza baadhi ya viongozi mbalimbali wa chama hicho na wageni waalikwa kutoka Serikali ya Mkoa wa Geita kukata Ndafu  ikiwa ni sehemu ya  kusherehekea sikukuu ya Eid El Hajj kwa pamoja,wakati wa mapumziko ya shughuli za kampeni za Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli,ambapo leo alitarajia kuendelea na kampeni zake mkoani Shinyanga.
Wakati huo huo Mgombea urais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM Dr.John Magufuli ameahirisha mikutano yake ya kampeni aliyokuwa aifanye leo Mkoani Shinyanga ili kupisha sikukuu ya Eid El Hajj,pia amewatakiwa Watanzania wote popote pale walipo sikukuu njema na yenye Baraka mbele za Mwenyezi Mungu na na kuwa tuendelee kuidumisha Amani ya Nchi yetu. 
  Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania na Mjumbe wa Kamati  Kuu ya CCM,Ndugu Abdallah Bulembo ambaye pia ni Kiongozi wa msafara wa kampeni za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM,akizungumza jambo mbele ya baadhi ya viongozi mbalimbali wa chama hicho na Serikali ya Mkoa wa Geita wakati wa mapumziko ya  kusherehekea sikukuu ya Eid El Hajj kwa pamoja,mapema le mchana mkoani Geita
 Ndafu akiwa ameandaliwa tayari kwa kuliwa.
 Ndafu ikikatwa kwa pamoja.PICHA NA MICHUZI JR-GEITA.

No comments: