Saturday, September 19, 2015

MANJI AIBUKA KIDEDEA TUZO ZA VIONGOZI WA BIASHARA AFRIKA

unnamedBMwenyekiti  wa Makampuni ya Quality Group Limited, Yusuph Manji.

……………………………………………………..
NA MWANDISHI WETU
MWENYEKITI  wa Makampuni ya Quality Group Limited, Yusuph Manji
amenyakua tuzo ya kielelezo cha viongozi wa biashara wa Afrika kwa
mwaka 2015.
Manji ambaye ni Mwenyekiti wa Klabu ya soka ya Yanga, aliwapiku
wafanyabiashara wengine wakubwa akiwemo bilionea namba moja Afrika,Aliko Dangote.
 Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na uongozi Quality Group,
ilisema  tuzo hiyo ilimshtua ‘bosi’ wao kwani hakutarajia na kwamba
itasaidia kuvutia wawekezaji pamoja na kuongeza idadi ya watalii
nchini.
 Tuzo hizo zilitolewa Septemba 16 mwaka huu.
Taarifa hiyo iliongeza  Manji ni chachu kwa vijana kufanya vizuri
kwenye sekta zao na  itasaidia nchi kusonga mbele katika kujikwamua na
umasikini.
 Tanzania inaendelea kujukulikana kimataifa na itasawaidia watanzania
kwa ujumla kufanya kazi ama biashara katika nchi nyingine bila ya
vikwazo visivyo na msingi kupitia tuzo hiyo.
Baadhi ya waliowahi kutwaa tuzo hiyo ni Mwenyekiti wa Emirates Group,
Sheikh Ahmed bin Saeed Al Maktoum inayomiliki kampuni ya Ndege ya
Emirates inayozidhamini timu za Real Madrid, Arsenal, AC Milan na
nyingine kubwa.
Wengine ni Mwenyekiti wa Emmar Properties, Mohammed Alabbar pia
bilionea kutoka India, Ratan Tata anayemiliki kampuni kubwa ya
Emeritus of Tata Sons Ltd.
Pia bilionea aliye tano bora duniani kwa utajiri, Mukesh Ambani ambaye
ni mwenyekiti wa Reliance Industries Ltd. Wengine ni Yingluck
Shinawatra, Waziri Mkuu wa zamani wa Thailand.
Pamoja na ushindi huo wa kishindo wa Manji, pia kampuni yake ya
Quality Group imeshinda kuwa kampuni bora na yenye mpangilio wa
uhakika kwa bara la Afrika ikipewa tuzo ya “Most Iconic Brand 2015”

No comments: