Sunday, September 20, 2015

DR.JOHN POMBE MAGUFULI: SITAKUA DIKTETA NITAFUATA UTAWALA WA SHERIA NITAKAPOKUWA MADARAKANI


  Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha  Mapinduzi (CCM),Dkt John Pombe Magufuli akifafanua jambo kwa msisitizo mkubwa wakati akiwahutubia wakazi wa Chato na vitongoji vyake jioni ya leo kwenye mkutano wa hadhara wa Kampeni uliofanyika uwanja wa shule ya sekondari Chato mkoani Geita.
  Wakazi wa Chato na Vitongoji vyake wakifuatilia na kusikiliza sera za Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akijinadi na kuomba ridhaa mbele yao jioni ya leo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya sekondari chato mkoani Geita.
 Wakazi wa Chato wakishangilia kuonesha kuwa watampa kura za ushindi Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu,kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika katika shule ya sekondari Chato,jioni ya leo mkoani Geita. 

001

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akihutubia mkutano wake wa kampeni kwenye uwanja wa Chato wialayani Chato mkoani Geita ambapo amewaomba wananchi wa Chato ambako ndiko alikozaliwa kumpigia kura za ndiyo ifikapo Oktoba 25 mwaka huu katika uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani.
Dk. Magufuli amesema mara atakapochaguliwa serikali yake itakuwa ni ya Watazania wote bila kujali vyama vyao, Dini zao, Makabila yao wala Itikadi zao atakuwa rais wa watanzania wote na lengo lake kubwa ni kuwatumikia watanzania na kuangalia zaidi na kuboresha hali za watanzania masikini ili nao waweze kukua kiuchumi.
Dk. Magufuli amesema kuna watu wameanza kuwatisha wananchi kwamba yeye ni mkali, Amesema “Si kweli yeye ni mpole sana ila nikiwa madarakani  nitaongoza nchi kwa utawala wa sheria na kuwapa haki watanzania  kulingana na sheria za nchi zanavyoelekeza kuendesha nchi hivyo sitakuwa kiongozi dikteta kama wanavyofikiri wengine”.  Japokuwa ninauchukia uzembe kazini, Wizi  na ufisadi.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-CHATO)
1
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akisisitiza jambo wakati akihutubia mkutano huo mjini Chato leo.
34
Picha mbalimbali zikionyesha umati wa wananchi waliohudhuria katika mkutano huo
567
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiserebeka na msanii Chege wa kundi la TMK Wanaume wakati lilipokuwa likitumbuiza katika mkutano huo.
9
Wasanii Mh. Temba kulia  na Chege kutoka TMK Wanaume wakitumbuiza katika mkutano huo.
10
Msanii Shilole naye akasuuza nyoyo za wananchi waliohudhuria katika mkutano huo.
1112
Kundi la TOT likitumbuiza kwenye mkutano huo006
Mke wa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akiwasalimia wana Chato na kumuombea kura mumewe pamoja na wabunge wa CCMna Madiwani.
13
Mke wa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akiwa amekaa na Mkuu wa mkoa wa Geita Mh. Fatma Mwasa kushoto wakiwa katika mkutano huo.
14
Kikundi cha ngoma kikitumbuiza katika mkutano huo.
1516
Msanii Mr Blue akifanya vitu vyake jukwaani.
17
Kundi la Orijino Kemodi wakionyesha vichekesho vyao jukwaani.
18
Yamoto Band wakifanya vitu vyao jukwani.
1921
Ali Tumbo akapanda jukwaani na Mbuzi akisakata muziki ili mradi burudani tu.
22
Malkia wa Mipasha Khadija Omar Kopa wa TOT akitumbuiza katika mkutano huo.
23
Msanii Fid Q naye akaghani kwa mistari yake migumu ya Ki -HipHop na kushangiliwa vya kutosha.
24
Mwanamuziki Bushoke akiiba wimbo wake katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akimkabidhi ilani ya uchaguzi Dk. Merdad Kalemani  mgombea ubunge wa jimbo la Chato baada ya kumpigia debe.
????????????????????????????????????
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiwapigia debe wagombea ubunge wa mkoa wa Geita kutoka kulia ni Vick Kamata mgombea wa viti maalum mkoa wa Geita na Joseph Kasheku Msukuma mgombea ubunge wa jimbo la Geita vijijini.
????????????????????????????????????
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiondoka kwenye mkutano mara baada ya kuhutubia mkutano wa kampeni mjini Chato leo.
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????
30
Msafara wa mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli ukiondoka kuelekea nyumbani mara baada ya mkutano huo.

No comments: