Tuesday, September 15, 2015

RAIS KIKWETE AZINDUA MIRADI YA NYUMBA ZA NHC MKOANI KIGOMA


Jengo la Biashara wa Lumumba Complex ambalo ni miongoni mwa majengo machache marefu mkoani Kigoma linavyoonekana kwa mbali mjini Kigoma jana.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe wakati wa uzinduzi wa nyumba za bei nafuu zilizojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa NHC eneo la Mlole mjini Kigoma. Wengine katika picha ni Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.William Lukuvi (wapili kushoto), Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Issa Machibya (wapili kulia), Mbunge  aliyemaliza muda wake wa Kigoma mjini Mh.Peter Selukamba (wanne kjshoto), Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bwana Nehemia Mchechu kulia na kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kigoma Ndugu Walid Aman Kabouru.



Rais Jakaya  Kikwete, Waziri wa Ardhi,  Lukuvi,  Mkurugenzi Mkuu NHC, Mchechu na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Machibya wakifurahi mara baada ya kukata utepe.
 Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kufungua jengo la kitega uchumi la Shirika la Nyumba la Taifa  NHC Lumumba Complex mjini Kigoma Septemba 14, 2015. Wengine katika picha ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete, (watatu kushoto), Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh.William Lukuvi, (wanne kushoto), Mkuu wa mkoa wa Kigoma Issa Machibya, (Wapili kulia), Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC Bwana Nehemia Mchechu (kulia), na kushoto ni Mbunge aliyemaliza muda wake wa Jimbo la Kigoma mjini Mh.Peter Selukamba.


 Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akifunua jiwe katika jiwe kuashiria kufungua rasmi jengo la kitega uchumi la Shirika la Nyumba la Taifa National Housing Lumumba Business Complex mjini Kigoma. Wapili kushoto ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na watatu kushoto ni Mkurugenzi mkuu wa NHC Bwana Nehemia Mchechu.

Rais Jakaya  Kikwete akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Jengo la Lumumba Complex Mjini Kigoma
 Rais Jakaya  Kikwete alipowasili katika jengo la Lumumba plaza ambapo alifungua rasmi jengo  hilo la kitega uchumi la Shirika la Nyumba la Taifa mjini Kigoma. Anayesalimiana naye ni Meneja wa NHC Kigoma, Nistas Mvungi na wanaoshuhudia ni Mkurugenzi wa Usimamizi wa Miliki wa NHC, Hamad Abdallah, Mjumbe wa Bodi ya NHC, Subira Mchumo na kushoto kabisa ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu.
Mkurugenzi wa Uendelezaji Milki Haikamen Mlekio akitoa maelezo  ya mradi wa gharama nafuu NHC Mlole mkoani Kigoma kwa Mh. Rais  Jakaya  Kikwete. Mradi huu wa Mlole, ulianza Novemba 2012 na umeshakamilika. Una nyumba za kuishi familia 36 na zina vyumba viwili na vitatu, jiko na sebule. Nyumba zote zinauzwa kwa wananchi watakaohitaji na zimejengwa kwa utaalamu wa kisasa wa kutumia matofali ya yanayotengenezwa na mashine za hydraform
Rais Jakaya Kikwete akifurahia mara baada ya kufungua Mradi wa nyumba za gharama nafuu Mlole. Wanaoshuhudia ni Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu.
Umati wa wananchi waliohudhuria sherehe hizo.

No comments: