Monday, September 21, 2015

UTEUZI WA MWENYEKITI NA WAJUMBE WA BODI YA MAMLAKA YA USIMAMIZI WA WANYAMAPORI TANZANIA (TAWA)

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
 TAARIFA KWA UMMA
UTEUZI WA MWENYEKITI NA WAJUMBE WA BODI YA MAMLAKA YA USIMAMIZI WA WANYAMAPORI TANZANIA (TAWA)

Wizara ya Maliasili na Utalii inapenda kuujulisha umma kuwa, Bodi mpya ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania  (Tanzania Wildlife Authority -TAWA),  imeteuliwa rasmi kuanzia tarehe 09 mwezi  Septemba, 2015.
Katika uteuzi huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemteua  Meja  Jenerali (Mstaafu) Hamis Rajabu SEMFUKO kuwa Mwenyekiti wa Bodi hiyo.

Wajumbe wengine  wa Bodi hiyo ambao wameteuliwa na Waziri wa Maliasili na Utalii  ni Dkt. Simon Mduma – Mkurugenzi Mkuu - TAWIRI,  Dkt. Fred Manongi – Mhifadhi  Mkuu - NCAA,  Suzane Charles Ndomba – Mwanasheria – ATE,  Bw. Gerald Bigurube – Meneja wa Program   Frankfurt Zoological Society – SERENGETI, Dkt. David Manyanza (Mstaafu)  Mtaalam wa Maswala ya Wanyamapori , Bw. Benson A. Shallanda – Kamishna wa Sera – HAZINA, Jenerali  Samweli Ndomba – Mnadhimu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Winfrida Nshangeki – Mkurugenzi wa Uratibu wa Sera – TAMISEMI, Abdulrahman Kaniki – Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania , Allan J. Kijazi – Mkurugenzi Mkuu  TANAPA, Mr. Herman W. Keraryo –Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori , Abdul Rajab Mhinte – Mkuu wa Idara ya Usalama   na Atakayeteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka.
 
Bodi hii, itaongoza Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania kwa kipindi cha miaka  mitatu kuanzia tarehe ya uteuzi.
                                                     Imetolewa na

                                Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikali
                                        Wizara ya Maliasili na Utalii
21/09/2015

No comments: