Friday, September 04, 2015

MAMA SALMA KIKWETE MGENI RASMI KWENYE UZINDUZI WA KAMPENI LINDI MJINI.

2
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi, (CCM) wa Wilaya ya Lindi na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongozana na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Lindi Mjini Ndugu Hassan Suleiman Kaunje wakiwapungia mikino mamia ya wananchi waliohudhuria sherehe ya uzinduzi rasmi wa kampeni kwenye Jimbo kwenye uwanja wa Fisi uliopo Manispaa ya Lindi tarehe 3,9.2015.
7
8
Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC Taifa ya Chama cha Mapinduzi Mama Salma Kikwete akihutubia mamia ya wananchi wa Lindi Manispaa wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Rais, wabunge na Madiwani utakaofanyika tarehe 25.10.2015 
10
Mjumbe wa NEC Taifa ya CCM na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimtambilisha rasmi Mgombea Ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi katika Manispaa ya Lindi Ndugu Hassan Suleiman Kaunje kwa wanachama wa CCM na wananchi wakati akizindua rasmi kampeni hizo kwenye uwanja wa Fisi huko Lindi tarehe 3.9.2015.
11
Mke wa Rais MamaSalma Kikwete akimkabidhi Ndugu Hassan Kaunje ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni hizo tarehe 3.9.2015.
5
Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC Taifa ya CCM anayewakilisha Lindi Manispaa Mama Salma Kikwete akipokea kadi kutoka kwa aliyekuwa mwanachama wa CUF na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mitandi Ndugu Laibu Kaisi aliyeamua kurejea Chama Cha Mapinduzi wakati wa sherehe za uzinduzi rami za kampeni za Chama hicho katika Manispaa hiyo.
34
Baadhi ya wanachama na wananchi katika Manispaa ya Lindi wakishangilia wakati Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC Taifa ya CCM anayewakilisha Manispaa hiyo Mama Salma Kikwete na viongozi wengine wakiingia uwanjani hapo.
     1213
   Baadhi ya vijana wakimshangilia kwa vifijo Ndugu Hassan Kaunje, Mgombea Ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi mara baada ya kumalizika kwa sherehe za uzinduzi rasmi wa kampeni hizo katika Wilaya ya Lindi Mjini tarehe 3.9.2015.
PICHA NA JOHN LUKUWI.

No comments: