Thursday, September 10, 2015

KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA MAHAKAMA YA TANZANIA-MKOANI DODOMA


 Mhe. Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania akifungua rasmi kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Mahakama ya Tanzania mapema leo katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gaspar uliopo mjini Dodoma, katika hotuba yake ya ufunguzi Mhe. Jaji Mkuu amewaasa Watumishi wa Mahakama kutimiza wajibu wao wa utoaji haki nchini kwa uadilifu.
  Kundi la baadhi ya Wahe. Majaji na wajumbe wengine wa Baraza la Wafanyakazi wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Baraza la Wafanyakazi linalofanyika katika Hoteli ya St. Gasper mjini Dar es Salaam.
 Mhe. Hussein A. Kattanga, Mtendaji Mkuu, Mahakama ya Tanzania akitoa taarifa ya Maendeleo ya Mahakama katika ufunguzi wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi kinachofanyika mkoani Dodoma.
 Wajumbe wa Baraza wakiwa katika kikao hicho, lengo la kikao cha Baraza la Wafanyakazi ni kuwawezesha Watumishi kuainisha matatizo yanayowakabili na kutafuta njia za kutatua na kuboresha huduma za Mahakama.
Mhe. Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania (katikati), Mhe. Shaban Ali Lila, Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania (wa pili kulia), Mhe. Clarensia Makuru, Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma, Mhe. Haruna Songoro, Kaimu Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Divisheni ya Biashara (wa kwanza kushoto), Bi. Rose Tengu, Katibu Mteule wa Baraza la Wafanyakazi-Mahakama ya Tanzania (wa tatu kushoto) na Wajumbe wengine wa Baraza wakiwa katika picha ya pamoja na Wahe. Wajumbe ya Kikao cha Baraza (waliosimama) wanaowakilisha mikoa mbalimbali. (Picha na Mahakama)

No comments: