Wednesday, March 09, 2016

RAIS WA VIETNAM, MHE. TRUONG TAN SANG AWASILI TANZANIA

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikianowa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Augustine Mahiga (kushoto)
akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki wakati wa
kumpokea Rais wa Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang katika Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Julius K. Nyerere 08 Maachi, 2016 Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano
wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Augustine Mahiga (kushoto), Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki (katikati) pamoja na Mkuu wa Wilaya
ya Kinondoni Paul Makonda wakiteta jambo wakati wa kumpokea Rais wa Vietnam,
Mhe. Truong Tan Sang katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius K. Nyerere 08
Maachi, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Kampuni ya Simu ya Halotel wakiwa tayari kumpokea Rais wao wa Vietnam Mhe. Truong Tan Sang akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius K. Nyerere 8 Machi, 2016  Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ziara yake ya siku tatu.
Vikundi vya burudani ya matarumbeta na ngoma vikitumbuiza katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius K. Nyerere 8 Machi, 2016 Jijini Dar es Salaam wakati wa kumpokea Rais wa Vietnam aliyewasili nchini kwa ajili ya ziara ya siku tatu akiwa amefuatana na ujumbe wake.
Ndege iliyombeba Rais wa Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang ikiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius K. Nyerere 8 Machi, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Ndege
iliyombeba Rais wa Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang ikiwa imewasili katika Uwanja
wa Ndege wa Kimataifa wa Julius K. Nyerere 8 Machi, 2016 Jijini Dar es
Salaam.
Baadhi ya viongozi mbalimbali wa Serikali ya Vietnam na Tanzania wakiwa tayari kumpokea Rais wao Mhe. Truong Tan Sang akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius K. Nyerere 8 Machi, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (wa pili kulia) akielekea kumpokea Rais wa Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang mara alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius K. Nyerere 8 Machi, 2016 Jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Augustine Philip Mahiga.
Rais wa Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang (kushoto) pamoja na mkewe wakiwapungia mkono viongozi mbalimbali waliokuja kumpokea mara alipowasili katika Uwanja Ndege wa Kimataifa wa Julius K. Nyerere 8 Machi, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang (kushoto) pamoja
na mkewe wakishuka kutoka kwenye ndege mara
walipowasili katika Uwanja Ndege wa Kimataifa wa Julius K. Nyerere 8
Machi, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa
(mwenye tai nyekundu) akimkaribisha Rais wa Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang (katikati)
mara alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius K.
Nyerere akiongozana na mkewe 8 Machi, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang (wa pili kulia) akisalimiana na baadhi ya viongozi waliokuja kumpokea mara alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius K. Nyerere 8 Machi, 2016 Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa
Rais wa Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang (wa tatu kulia) akiwasalimia baadhi ya Watanzania na Wavietnam waliokuja kumpokea mara alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius K. Nyerere 8 Machi, 2016 Jijini Dar es Salaam. Wa pili kulia ni Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa.
Rais wa Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang (wa pili kulia) akiangalia vikundi vya ngoma vikivyotumbuiza uwanjani mara alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius K. Nyerere 8 Machi, 2016 Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa.
Rais wa Vietnam, Mhe. Truong Tan Sang akiwapungia mkono wacheza ngoma na matarumbeta waliokuja kumpokea mara alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius K. Nyerere 8 Machi, 2016 Jijini Dar es Salaam.
(Picha zote na Benedict Liwenga-Maelezo)

No comments: