Tuesday, March 29, 2016

BALOZI HAULE ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO.

 Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. John Haule akitia saini kitabu cha maombolezo ya kifo cha Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) nchini Kenya, Mhe. TADUMI ON'OKOKO, kwenye Ubalozi wa DRC Nairobi leo, Mhe. ON'OKOKO, ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao Kenya, alifariki dunia tarehe 20 Machi 2016 huko Paris, Ufaransa, ambako alikuwa anatibiwa. Anayeshuhudia ni Kaimu Balozi wa DRC, Mhe. Michel Mubare, ambaye alifahamisha kuwa marehemu atazikwa Kinshasa baada ya mipango kukamilika.
 Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. John Haule (Kulia) akimfariji Kaimu Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mhe. Michel Mubare,  baada ya kutia saini kitabu cha maombolezo ya kifo cha aliyekuwa Balozi wa nchi hiyo Kenya, Mhe. Tadumi On'okoko jijini Nairobi leo.

No comments:

RAIS NDAITWAH AONDOKA BAADA YA KUKAMILISHA ZIARA YA KITAIFA YA SIKU TATU NCHINI

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Namibia Mhe. Dkt, Netumbo...